Mtego wa Noti
JF-Expert Member
- Nov 27, 2010
- 2,591
- 1,599
- Thread starter
-
- #41
Kwa mara ya kwanza nimeshuhudia kioja katika ufunguzi wa bunge , leo jioni pale mbunge wa Mtera Livingstone Lusinde maarufu kama Bajaji aliyeangusha Katapila (malecela),
Kasema mambo ya kushangaza yafuatayo:-
1.Baadhi ya wanasiasa wanapotosha umma kwa kusema kwamba Polisi na Serikali wanapiga wananchi mabomu.. ( hapa alikuwa akimaanisha CHADEMA na tukio la Arusha)… akasema kwamba yale sio mabomu bali bi gesi lakini wanasiasa wanapotosha umma kwa makusudi, mabomu ni yale yaliyolipuka pale Mbagala na sio yanayotumiwa na polisi
2. Kampongeza Edward Lowassa kwa kujihudhuru kutoka na uzembe uliofanywa na watendaji wa chini yake katika suala la Dowans na akazidi kusema kuna watu wengine ni wagumu kujihudhuru hata kaika timu zao zinapofanya vibaya na mambo mengine mengine
3.Suala la JK kua mvumilivu kutokana na mambo yanayoendelea , anafikiwa hatua ya kuandikwa vibaya katika vyombo vya habari na kwenye mitandao… akaongeza Hivi najiuliza huyu raisi Kikwete ujeshi wake mbona hauoneshi mbona amekua mpole kiasi hiki na angekua mtu mwingine asingeweza kuvumilia…
Aliongea mengi ambayo hayana maana mbele ya watanzani wanaopigika na maisha ikiwemo gharama za Umeme kua juu, mgao wa umeme, mfumuko wa bei za bidhaa, wanafunzi wa vyuo kikuu kuandamana na kupigana na mapolisi n.k
Note: huyu jamaa nimemuona ni mkurupukaji na anayejipendekeza kwa wakuu wake akitegemea fadhila ya vyeo na madaraka serikalini na CCM, sio mpambanaji wa kweli bali ni mropokaji anayeongea kufurahisha wabunge wenzake wa CCM na anavyoonekena ni mtu anaye danganyika kirahisi, na sio mwakilishi wa kweli pale mjengoni…
Wana JF naomba mmfuatilie vizuri huyu jamaa kila wakati anapoongea halafu baada ya kikao cha bunge kuisha mtaniambia
Kazi tunayo mwaka huu! Kama CCM ina wabunge wa aina hii wengi basi nchi itaendelea kuwa chini ya mafisadi kwa miaka mitano
nazidi kuamini wabunge makini wanatoka chadema pekee..
Mbunge Lusinde wa Mtera anasema anaomba wabunge watangwane bungeni ili madhara ya vurugu yaonekane na isiwe watu kuwatumia wananchi kuwatuma wapigane ili kupata umaarufu wakisiasa!!!
Anasema wafunge milango watwangane halaf ndio watoke nje...kazi kwelikweli!!!
Kwa mara ya kwanza nimeshuhudia kioja katika ufunguzi wa bunge , leo jioni pale mbunge wa Mtera Livingstone Lusinde maarufu kama Bajaji aliyeangusha Katapila (malecela),
Kasema mambo ya kushangaza yafuatayo:-
1.Baadhi ya wanasiasa wanapotosha umma kwa kusema kwamba Polisi na Serikali wanapiga wananchi mabomu.. ( hapa alikuwa akimaanisha CHADEMA na tukio la Arusha) akasema kwamba yale sio mabomu bali bi gesi lakini wanasiasa wanapotosha umma kwa makusudi, mabomu ni yale yaliyolipuka pale Mbagala na sio yanayotumiwa na polisi
2. Kampongeza Edward Lowassa kwa kujihudhuru kutoka na uzembe uliofanywa na watendaji wa chini yake katika suala la Dowans na akazidi kusema kuna watu wengine ni wagumu kujihudhuru hata kaika timu zao zinapofanya vibaya na mambo mengine mengine
3.Suala la JK kua mvumilivu kutokana na mambo yanayoendelea , anafikiwa hatua ya kuandikwa vibaya katika vyombo vya habari na kwenye mitandao akaongeza Hivi najiuliza huyu raisi Kikwete ujeshi wake mbona hauoneshi mbona amekua mpole kiasi hiki na angekua mtu mwingine asingeweza kuvumilia
Aliongea mengi ambayo hayana maana mbele ya watanzani wanaopigika na maisha ikiwemo gharama za Umeme kua juu, mgao wa umeme, mfumuko wa bei za bidhaa, wanafunzi wa vyuo kikuu kuandamana na kupigana na mapolisi n.k
Note: huyu jamaa nimemuona ni mkurupukaji na anayejipendekeza kwa wakuu wake akitegemea fadhila ya vyeo na madaraka serikalini na CCM, sio mpambanaji wa kweli bali ni mropokaji anayeongea kufurahisha wabunge wenzake wa CCM na anavyoonekena ni mtu anaye danganyika kirahisi, na sio mwakilishi wa kweli pale mjengoni
Wana JF naomba mmfuatilie vizuri huyu jamaa kila wakati anapoongea halafu baada ya kikao cha bunge kuisha mtaniambia