Lukas Sankara ashinda kura za maoni Kalenga

Lukas Sankara ashinda kura za maoni Kalenga

Namtakia pole in advance...

Sisimizi kapewa kazi ya kumsukuma Tembo.
Chris lukosi, umesindwa kugombea kwa vile sio ukoo wa kifalme ww?. pamoja na lengo la kushinda uchaguzi lakini pia chadema wanakuja kuelimisha umma elimu ya uraia. Nashangaa ww umekimbilia ughaibuni kisha unawatia ujinga wahehe wenzio swela winanghani.
Dei
 
Nasita kushauri CDM isigombee uchaguzi wowote kabla daftari ka mpiga kura halijaboreshwa
 
Chris lukosi, umesindwa kugombea kwa vile sio ukoo wa kifalme ww?. pamoja na lengo la kushinda uchaguzi lakini pia chadema wanakuja kuelimisha umma elimu ya uraia. Nashangaa ww umekimbilia ughaibuni kisha unawatia ujinga wahehe wenzio swela winanghani.
Dei
Mimi sijashindwa kugombea bali sina haki ya kugombea kwa sasa kikatiba.

Subiri tu, sio muda mrefu tutapigana vikumbo mtaani.
 
atapata wapi pesa za kuwahonga wajumbe? kugombea ssiem kunahitaji pesa,maskini kama mimi hawana nafasi ccm!
Wakati ukifika nitasimama nakugombea, suala la pesa halina uhusiano na kukubalika.

Mimi sio masikini kwa sababu nina miguu yote na miguu yote na sina ulemavu wowote.

Kila jambo ni wakati
 
Namtakia pole in advance...

Sisimizi kapewa kazi ya kumsukuma Tembo.

Lukosi box3.jpg

Wewe utakuwa umeathiriwa na Mabox kwani akili zako zimekuwa fupi sana na kingine kinachokuathiri ni kuishi kwa kutegemea Dada na ole wako akiachwa tu na wewe ujue umepewa Taraka.
 
Mwanasheria wa Chadema nyanda za juu kusini wakili msomi Kamanda Lukas Sankara ameshinda kura za maoni zakuwania tiketi ya kuwania kiti cha ubunge kwa tiketi ya CHADEMA katika Jimbo la Kalenga baada ya kuwashinda wenzake 12 jioni ya leo.

hope ulikuwa mchakato wa haki na demokrasia ilichukua nafasi yake...
 
[h=3]Feb 12th 2014
ASHINDA KWA KISHINDO HUKU ALIYEKIMBIA KUSHINDWA CCM AANGUKIA PUA CHADEMA
[/h]

[TABLE="class: tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption"]mshindi wa kura za maoni jimbo la kalenga mwanasheria SINKALA MWENDA akipongezwa[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

wajumbe wa mkutano wa kura za maoni jimbo la kalenga wakifuatilia matokeo ya uchaguzi leo
msimamizi mkuu wa uchaguzi huo Bw Benison Kigaila akitoa maelekezo ya chama

kada aliyeshika nafasi ya pili ktika mchakato huo GRACE TENDEGA kushoto akiwa na wagombea wenzake
Kada muuza magazeti Aidani Pungili kushoto akiwa na wagombea wenzake


Mwenda ametangazwa mshindi wa kura za maoni katika uchaguzi uliofanyika leo toka majira ya saa 4 asubuhi na kumalizika majira ya saa 4 usiku katika ukumbi wa St Dominic mjini Iringa .

Uchaguzi huo uliosimamiwa na mjumbe wa kamati kuu ya Chadema Taifa Chiku Abwao na Benison Kigaila wajumbe wa mkutano wa Halmashauri kuu ya Chadema jimbo la kalenga waliumiza vichwa vyao kuwasikiliza wagombea wote 13 kabla ya kuwachuja na kumchangua mwanasheria Mwenda kwa kura 132 dhidi ya kura 122 alizopata mpinzani wake wa karibu Grace Tendega ambae pia alikuwa akipewa nafasi kubwa ya kushinda kutokana na kuwa na historia ya kugombea kupitia chama cha Jahazi Asilia na kutoa ushindani mkali kwa CCM kabla ya kuhamia Chadema.

Mbali ya wapinzani hao wakubwa kuvutana vikali bado kada muuza magazeti maarufu mjini Iringa Aidan Pungili ambae pia alikuwa akipewa nafasi ya kufanya vizuri katika uchaguzi huo aliambulia kura 2 pekee huku mwenzake Daniel Luvanga akipata kura moja ya kufutia machozi .

Wagombea wengine ambao wameonyesha kufanya vema kiasi baada ya kujiunga na Chadema wakitokea CCM ni pamoja na Dr Evaristo Mtitu aliyepata kura 32,Ancent Sambala ambae amepata kuwania ubunge katika kura za maoni CCM kwa zaidi ya mara 2 katika jimbo la kalenga kabla ya kuhamia Chadema pia aliambulia nafasi ya tano kwa kupata kura 22 tofauti na nafasi saba aliyochukua mwaka 2005 akiwa ndani ya CCM kwa kupata kura chini ya 8.

Pia mgombea Akbar Sanga katika uchaguzi huo alipata kura (21),Rehema Makoga (4), Henry Kavina(9), Mussa Mdede(48), Mchungaji Samweli Nyakunga(2) na mwalimu Vitus Lawa akipata kura (14).

Msimamizi mkuu wa uchaguzi huo mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa Chadema, Benson Kigaila aliwataka wajumbe wa mkutano huo kutoshangilia zaidi juu ya matokeo hayo kwani kushinda katika kinyang'anyiro ni mwanzo tu wa safari ya kumpata mteule wa Chadema atakayekabidhiwa bendera ya Chadema kuvaana na CCM katika uchaguzi huo mdogo.

Alisema mgombea sahihi ambae watapaswa kumshangilia na kumtangaza kwa wananchi wa jimbo la Kalenga ni yulev ambae atapitishwa na vikao vya juu vya Chama hicho Taifa tarehe 14 mwezi huu.

Hata hivyo aliwataka wagombea wote 13 walioomba kuwania nafasi hiyo kabla ya kupatikana mshindi huo Mwenda kuanza safari mapema kesho Alhamis asubuhi ya kwenda jijini Dar es salaam kwa ajili ya kwenda kujieleza mbele ya kamati kuu ya Chadema kabla ya kumteua mgombea wa jimbo hilo la kalenga.

"Baada ya matokeo haya ndugu zangu wajumbe nawaombeni makatibu kata wote wa jimbo la Kalenga kubaki hapa ndani na wajumbe kuanza safari ya kurudi majumbani leo hata hatutaruhusu wagombea ama mshindi kuongea chochote .....kwani wote watakwenda kuongea mbele ya kamati kuu ila kuanzia kesho Chadema itaendelea na mikutano yake jimbo la kalenga ya kukitambulisha chama zaidi kwa wananchi na sio kumnadi mgombea kwani bado mgombea wetu hajapatikana kampeni zenyewe zitaanza baada ya mgombea wetu atakayeteuliwa kuchukua na kurejesha fomu ya tume"


Kigaila aliwataka viongozi hao wa Chadema jimbo la kalenga kuanza kukijenga zaidi chama hicho na kuwa mara baada ya kampeni kuanza wana Chadema wilaya zote za mkoa wa Iringa wataingia kazini katika jimbo hilo.




VITUKO VYA WAGOMBEA


mmoja kati ya wagombea walioomba ashindwa kutokea ukumbini atuma mpambe kumsomea maelezo yake huku akieleza kuwa iwapo atapitishwa kuwa mgombea tayari ametenga kiasi cha Tsh milioni 9 kwa ajili ya kampeni zake kitendo cha kutofika ukumbini hapo kilionyesha kuwakwaza wajumbe kuwa hawana shida na pesa zake hivyo kumnyima nafasi hiyo.


Huku kituko namba mbili kutoka kwa wagombea hao ni baada ya mmoja wapo kudanganya kiwango chake cha elimu na kuongopa chuo alichopata elimu yake na kushindwa kutamka vema kiwango cha elimu alicho nacho hivyo wajumbe kushindwa kuamini maelezo yake na kumnyima pia kura.


Kituko kikubwa cha tatu ni pale mmoja kati ya wagombea kutumia CV yake ya kufungwa jela mara kwa mara kama mtaji wa kuombea kura huku wajumbe hao wakishindwa kujua umaarufu wake wa kufungwa na maendeleo ya wana Kalenga vina mahusiano gani hivyo kumpiga chini pia.




[h=3]CHADEMA CHASEMA HAKITASIMAMISHA MGOMBEA DHAIFU KALENGA NI LAZIMA CCM IANZE KUZOEA KUSHINDWA[/h]

[TABLE="class: tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption"]mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa Chadema, Benson Kigaila akizungumza na wajumbe wa mkutano wa Halmashauri kuu ya Chadema jimbo la Kalenga jana huku akionyesha katiba ya Chadema kabla ya wajumbe wa mkutano huo kupiga kura kumchagua mgombea ubunge jimbo hilo kupitia Chadema[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[TABLE="class: tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption"]Wajumbe wa mkutano wa kura za maoni Chadema jimbo la Kalenga wakiwa katika ukumbi wa St Dominic[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

[TABLE="class: tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption"]Viongozi mbali mbali wa Chadema wakiwa meza kuu [/TD]
[/TR]
[/TABLE]

[TABLE="class: tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption"]Mjumbe wa kamati kuu ya Chadema Taifa Bi Chiku Abwao akizungumza katika mkutano huo leo [/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[TABLE="class: tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption"]WAKATI leo wajumbe wa Halmashauri kuu ya chama cha Demokrsia na maendeleo (CHADEMA) jimbo la Kalenga wameshiriki katika zoezi la upigaji wa kura za maoni kuchagua mmoja kati ya wanachama 13 waliojitokeza kurejesha fomu za kuomba kuteuliwa kuwa wagombea wa nafasi ya ubunge jimbo la kalenga kupitia chama hicho ,mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa Chadema, Benson Kigaila amesema chama chake kamwe hakitasimamisha mgombea dhaifu katika kinyang'anyiro hicho na lazima CCM kianze kuzoea kushindwa .


Huku mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa na mjumbe wa kamati kuu ya Chadema Bi Chiku Abwao akiwataka wana Kalenga kujenga imani na Chadema na kuwa haitakuwa tayari kumweka ndugu katika chaguzi hizo na kuwa CCM imeonyesha kuwadharau wana Kalenga kwa kuendekeza siasa za familia katika jimbo hilo jambo ambalo halikubaliki.


Akifungua mkutano huo wa kura za maoni katika ukumbi wa St Dominic mjini Iringa Kigaila alisema kuwa lengo la mkutano huo ni kuanzisha mchakato wa kumpata mgombea wa Chadema na kuwa Chadema ina matumaini makubwa ya kushinda katika jimbo hilo.


" CCM walikuwa wakisikilizia ni nani ambae Chadema itamsimamisha katika jimbo hilo na kuwa walidhani wapo peke yao ila sasa Chadema inatangaza rasmi kuwa mchakato wa kumpata mgombea wake umeanza na ni lazima apatikane mgombea ambae atakuwa ni tofauti na mgombea wa CCM....lazima CCM kwa hapa kilipofika kianze kuzoea kushindwa katika uchaguzi"


Alisema kuwa utaratibu wa kumpata mgombea wa Chadema ni utaratibu ambao hautokani na mtu mmoja ama viongozi pekee wa juu bali ni utaratibu shirikishi ambao baada ya kutoka katika hatua ya kura za maoni kitafuata kikao cha kamati ya utendaji ya jimbo kabla ya kamati kuu ya chama kufanya maamuzi yake Februari 14 jijini Dar es Salaam kwa kumteua mgombea atakayesimama jimbo hilo la Kalenga.


Hivyo aliwataka wana Chadema kuwa makini katika kusikiliza kila mgombea na kuhakikisha wanachagua mgombea ambae atakubalika katika chama hicho na hata vyama vingine kikiwemo CCM na wananchi wote wa jimbo la Kalenga.


Kigaila alisema mchakato wa kuchukua fomu ndani ya chama hicho jumla ya wana Chadema 16 walijitokeza kuchukua fomu ila hadi juzi siku ya mwisho kurejesha fomu ni wanachama 13 ndio ambao walirejesha na kudai kuwa mwitikio huo ni ishara nzuri ya Chadema kuonyesha kukua zaidi katika jimbo la Kalenga.


Hata hivyo alisema kuwa Chadema kina imani kubwa ya kushinda kiti hicho cha jimbo la Kalenga na ushindi huo utakuwa ni mwanzo wa kukiondoa chama tawala madarakani .


Kwa upande wake Abwao alisema kuwa CCM kimewasaliti wananchi wa jimbo la Kalenga kwa kuonyesha kuibeba familia ya aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo Dr Wiliam Mgimwa na kuwaomba wana Kalenga kuunganisha nguvu zao kumchagua mgombea wa Chadema atakayeteuliwa na Chama .


Awali katibu wa Chadema wilaya ya Iringa vijijini Felix Nyondo aliwataja waliojitokeza kuchukua na kurejesha fomu kuwa ni pamoja na Zubery Mwachura , Dr Evaristo Mtitu, Akbar Sanga, Grace Tendega, Rehema Makoga, Sinkala Mwenda, Henry Kavina, Aidan Pungili, Mussa Mdede, Mchungaji Samweli Nyakunga, Daniel Luvanga, Anicent Sambala na Vitus Lawa.


Hata hivyo wagombea 12 ndio waliofika ukumbini hapo huku mgombea mmoja Zubery Mwachura akikosekana kutokana na kuwa nje ya nchi kwa shughuli za kikazi.
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]




source Francis Godwin
 
Naona mmoja aliamua kutumia cv ya kutupwa sero kama viongozi wake.

Chadema wanaharibu sana vijana wetu, mtu afungwe kwa kosa la kuiba vitindi vya ulanzi halafu anatumia kama sifa kwenye kutafuta ubunge?
 
Wakati ukifika nitasimama nakugombea, suala la pesa halina uhusiano na kukubalika.

Mimi sio masikini kwa sababu nina miguu yote na miguu yote na sina ulemavu wowote.

Kila jambo ni wakati

Uzuri wa ndoto kila mtu anaruhusiwa kuota vyovyote. Kila la kheri.
 
Naona mmoja aliamua kutumia cv ya kutupwa sero kama viongozi wake.

Chadema wanaharibu sana vijana wetu, mtu afungwe kwa kosa la kuiba vitindi vya ulanzi halafu anatumia kama sifa kwenye kutafuta ubunge?

Aden Rage??? Na mbunge alokamatwa kwa rushwa u wa chama kipi?
 
Back
Top Bottom