Luhaga Mpina: Nimepiga hesabu ya hasara kwenye ripoti ya CAG, ni zaidi ya Trilioni 30

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Jan 29, 2021
573
2,554
Katika mjadala unaoendelea Bungeni kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 11, Kikao cha 4 jioni ya leo April 11, 2023 Mbunge wa Kisesa Luhaga Mpina amesema katika uchambuzi wa ripoti ya CAG anaoendelea kuufanya, amebaini kuwa zaidi ya Trilioni 30 zimepotea.

IMG_6697.jpeg


Ameonesha masikitiko yake kuwa wabadhirifu hawa bado wapo serikalini na Mamlaka haziwachukulii hatua.

Amesema, “Mhe. Naibu spika, kwa summary tu hapa, ubadhirifu wote huu wa CAG ambao mimi nimeainisha na bado naendelea kuainisha ni zaidi ya trilioni 30, trilioni 30. Sasa mkishakuwa na ubadhirifu wa trilioni 30, unakaa kwenye bajeti kufanya nini, yaani unathibitisha pesa zote zikagawanwe?”

Amemalizia “Lazima tuchukue hatua kali Mhe. Naibu spika, kwa watu hawa wanaofanya haya mambo”

UPDATE:
Jenesta Mhagama ameomba mwongozo wa takwimu hizo ambazo kwa maelezo yake amedai zikiachwa kama zilivyo zinaweza kuleta sintofahamu kubwa kwa Taifa kuanzia leo.

Naibu spika Mussa Azzan Zungu amesema Serikali imepewa siku 21 kujibu hoja za CAG hivyo ametoa amri ya kuondoa kwenye Hansard za Bunge maneno ya Mbunge Luhaga Mpiga.
 
Katika mjadala unaoendelea Bungeni kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 11, Kikao cha 4 jioni ya leo April 11, 2023 Mbunge wa Kisesa Luhaga Mpina amesema katika uchambuzi wa ripoti ya CAG anaoendelea kuufanya, amebaini kuwa zaidi ya Trilioni 30 zimepotea.

Ameonesha masikitiko yake kuwa wabadhirifu hawa bado wapo serikalini na Mamlaka haziwachukulii hatua.

Amesema, “Mhe. Naibu spika, kwa summary tu hapa, ubadhirifu wote huu wa CAG ambao mimi nimeainisha na bado naendelea kuainisha ni zaidi ya trilioni 30, trilioni 30. Sasa mkishakuwa na ubadhirifu wa trilioni 30, unakaa kwenye bajeti kufanya nini, yaani unathibitisha pesa zote zikagawanwe?”

Amemalizia “Lazima tuchukue hatua kali Mhe. Naibu spika, kwa watu hawa wanaofanya haya mambo”
Mhagama ameshaomba mwongozo

Imefutwa hiyo
 
Muheshimiwa rais imependekezwa ujiuzulu na kuukana uanachama ugombee upya

 
Naibu Spika atuambie, vipi baada ya hizo siku 21 ikibainika ni kweli hiyo hasara imepatikana, bunge litarudisha hayo maneno kwenye Hansard? au litaendelea kuwa mtumwa wa serikali?

Very sad, bunge haliaminiki. Kama tumeambiwa wizara moja tu ya Ujenzi wamekula trillion 2, kwanini nisimuamini Mpina aliyepiga hesabu za jumla?

Lakini pia kwasababu hao jamaa hawajawahi kujibu hoja za Mpina zaidi ya kumshambulia binafsi, niko pamoja nae, naamini kile alichosema, na nimekiweka kwenye Hansard yangu.
 
Aisee inauma sana kupitisha bajet ambayo watu watagawana aitafanya shughuli za maendeleo ni vema sasa naonelea tusiwe na bajet kwanza kwa mdah huu wa miaka miwili mbaka tufanye uchaguzi tumpate raisi anayejitambua wa kuchaguliwa tuachane na hii mifumo ya kimalikia mtu kurithi uongozi baada ya baba kufariki anakua ana vision ajui afanye nn yupo yupo tu kusonya, na kuwaambia wezi wampishe
 

Moderators at JamiiForums!.
Hii ni post yangu ya nne kwa siku ya leo,na mnaziondoa kinyemela!
Sijui kama na nyinyi mmeanza kuingia kwenye list au?
Tafadhali sana muwe mnaheshimu mawazo ya wenzenu!
Otherwise bora mtumie Ban ili tuwaelewe rasmi kwamba hili sio jukwaa huru tena!
Badala ya kutupotezea muda tunaandika na ku-post halafu nyinyi mnachezea mouse kwa kuondoa threads as if mko na project maalumu ya kuwalinda wahusika?
Kwa nini hii inatokea tena bila notice?
Wakati mnao uwezo wa kuwasiliana nasi kwa urahisi kabisa!

Niliwahi kumueleza hili jambo Live,Maxence Melo!
Siku moja tulipokutana live kule Kubukubu Tented .....
Na aliahidi kulifanyia kazi.
Ila naona kuna baadhi yenu mko ofisini ki-vyenu vyenu zaidi.
Mark my words!
 
Taifa linalo kusanya trilioni 2 Kwa mwezi ...mtu anakuja kusema zimeibiwa trilioni 30?
Yaani pesa yote na ya mikopo na misaada??hata ya mishahara ya mwaka mzima pia imeibiwa??

Na kuna watu wanamshangilia??

Hata kama kuzidisha chumvi ...only wapumbavu ndo wanaweza kukushabikia...
Watu wenye akili wanakuona huna akili kabisa....
 
Mheshimiwa Mpina amezungumzia ongezeka l gharama za ujenzi wa reli ya SGR toka Tabora kwenda Kigoma (ongezeko la 1.7 trillion) baada ya Serikali kutoa zabuni kwa kampuni ya (China Constructon Company) mwenye gharama kubwa badala ya kampuni ya kituruki inayojenga kipande cha Dar es Salaam -Morogoro Mheshimiwa Mpina amependekeza Waziri wa Fedha na Mipango, Waziri wa ujenzi na uchukuzi,Mkurugenzi Mkuu wa TRC wajitafakari na kuachia ngazi kwa kuisababishia Serikali hasara na matumizi mabaya ya fedha za walipa kodi
 
Mheshimiwa Mpina amezungumzia ongezeka l gharama za ujenzi wa reli ya SGR toka Tabora kwenda Kigoma (ongezeko la 1.7 trillion) baada ya Serikali kutoa zabuni kwa kampuni ya (China Constructon Company) mwenye gharama kubwa badala ya kampuni ya kituruki inayojenga kipande cha Dar es Salaam -Morogoro Mheshimiwa Mpina amependekeza Waziri wa Fedha na Mipango, Waziri wa ujenzi na uchukuzi,Mkurugenzi Mkuu wa TRC wajitafakari na kuachia ngazi kwa kuisababishia Serikali hasara na matumizi mabaya ya fedha za walipa kodi
Hawatufai kabisa
 
Katika mjadala unaoendelea Bungeni kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 11, Kikao cha 4 jioni ya leo April 11, 2023 Mbunge wa Kisesa Luhaga Mpina amesema katika uchambuzi wa ripoti ya CAG anaoendelea kuufanya, amebaini kuwa zaidi ya Trilioni 30 zimepotea.

View attachment 2584490

Ameonesha masikitiko yake kuwa wabadhirifu hawa bado wapo serikalini na Mamlaka haziwachukulii hatua.

Amesema, “Mhe. Naibu spika, kwa summary tu hapa, ubadhirifu wote huu wa CAG ambao mimi nimeainisha na bado naendelea kuainisha ni zaidi ya trilioni 30, trilioni 30. Sasa mkishakuwa na ubadhirifu wa trilioni 30, unakaa kwenye bajeti kufanya nini, yaani unathibitisha pesa zote zikagawanwe?”

Amemalizia “Lazima tuchukue hatua kali Mhe. Naibu spika, kwa watu hawa wanaofanya haya mambo”

UPDATE:
Jenesta Mhagama ameomba mwongozo wa takwimu hizo ambazo kwa maelezo yake amedai zikiachwa kama zilivyo zinaweza kuleta sintofahamu kubwa kwa Taifa kuanzia leo.

Naibu spika Mussa Azzan Zungu amesema Serikali imepewa siku 21 kujibu hoja za CAG hivyo ametoa amri ya kuondoa kwenye Hansard za Bunge maneno ya Mbunge Luhaga Mpiga.
Kwa jinsi Bi Ruksa mwenyekiti wake asivyopenda shida, Bw. Luhaga aage kabisa bungeni.
 
Naibu Spika atuambie, vipi baada ya hizo siku 21 ikibainika ni kweli hiyo hasara imepatikana, bunge litarudisha hayo maneno kwenye Hansard? au litaendelea kuwa mtumwa wa serikali?

Very sad, bunge haliaminiki.

Lakini pia kwasababu hao jamaa hawajawahi kujibu hoja za Mpina zaidi ya kumshambulia binafsi, niko pamoja nae, naamini kile alichosema, na nimekiweka kwenye Hansard yangu.
Hakuna kitu kama hicho .....hoja zitajibiwa na tutajua hasara halisi sio kila hoja ni sahihi ....ndio maana zimerudishwa Kwa KM wizara wazijibu.....
 
Katika mjadala unaoendelea Bungeni kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 11, Kikao cha 4 jioni ya leo April 11, 2023 Mbunge wa Kisesa Luhaga Mpina amesema katika uchambuzi wa ripoti ya CAG anaoendelea kuufanya, amebaini kuwa zaidi ya Trilioni 30 zimepotea.

View attachment 2584490

Ameonesha masikitiko yake kuwa wabadhirifu hawa bado wapo serikalini na Mamlaka haziwachukulii hatua.

Amesema, “Mhe. Naibu spika, kwa summary tu hapa, ubadhirifu wote huu wa CAG ambao mimi nimeainisha na bado naendelea kuainisha ni zaidi ya trilioni 30, trilioni 30. Sasa mkishakuwa na ubadhirifu wa trilioni 30, unakaa kwenye bajeti kufanya nini, yaani unathibitisha pesa zote zikagawanwe?”

Amemalizia “Lazima tuchukue hatua kali Mhe. Naibu spika, kwa watu hawa wanaofanya haya mambo”

UPDATE:
Jenesta Mhagama ameomba mwongozo wa takwimu hizo ambazo kwa maelezo yake amedai zikiachwa kama zilivyo zinaweza kuleta sintofahamu kubwa kwa Taifa kuanzia leo.

Naibu spika Mussa Azzan Zungu amesema Serikali imepewa siku 21 kujibu hoja za CAG hivyo ametoa amri ya kuondoa kwenye Hansard za Bunge maneno ya Mbunge Luhaga Mpiga.
Zungu, Zungu unapopoma kuondoka hansadi Nini kazi ya Bunge?
Hizo siku 21 mtakuja na majawabu kweli au ndio kuzika hoja chini chini.
Hakuna wa kumfunga paka kengele hapo.
Jieleweni Kuna wengine hamkutakiwa hapo basi ni Kwa vile!

Sasa swala kama la BISWALO linaundiwaje Tume na kwanza hamkutakiwa kuwepo ofisini, TAKUKURU mpo wapi?
Yeye mwenyewe alitakiwa awe amepisha kazi.

Bunge ni like lile la kuficha maovu.
Na hizi sifa kwenye magazeti kila siku waandishi wa habari mnaumizaà Taifa.
 
Back
Top Bottom