Kurzweil
JF-Expert Member
- May 25, 2011
- 6,622
- 8,397
Waziri wa Mambo ya Ndani aliagiza Jeshi la Polisi nchini Tanzania kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA) kuwasaka watu wanaotoa maneno ya uchochezi dhidi ya Rais John Magufuli na Serikali.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Februari 13, 2019 jijini Arusha Lugola amesema wanaotoa maneno ya uchochezi kupitia simu zao, Blogs na makundi ya WhatsApp watasakwa popote na kuchukuliwa hatua za kisheria.
“Watanzania tumieni vizuri mitandao ya kijamii, msitumie kuvuruga amani ya nchi, usijidanganye unaweza kufanya uchochezi na usikamatwe,” amesema akidai watu hao wanamchonganisha Rais Magufuli na wananchi.
“Kama unatoa kauli za kumtukana Rais na uchochezi ina maana kuna watu nyuma wanakutuma,” amesema Lugola.
Chanzo: Mwananchi
Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Februari 13, 2019 jijini Arusha Lugola amesema wanaotoa maneno ya uchochezi kupitia simu zao, Blogs na makundi ya WhatsApp watasakwa popote na kuchukuliwa hatua za kisheria.
“Watanzania tumieni vizuri mitandao ya kijamii, msitumie kuvuruga amani ya nchi, usijidanganye unaweza kufanya uchochezi na usikamatwe,” amesema akidai watu hao wanamchonganisha Rais Magufuli na wananchi.
“Kama unatoa kauli za kumtukana Rais na uchochezi ina maana kuna watu nyuma wanakutuma,” amesema Lugola.
Chanzo: Mwananchi