chikanu chikali
JF-Expert Member
- Aug 29, 2017
- 1,141
- 1,826
Wanaochafua upinzani kama akina musiba wao wanafanyajwe? Hii ni nchi ya wote na si ccm pekeeWaziri wa Mambo ya Ndani aliagiza Jeshi la Polisi nchini Tanzania kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA) kuwasaka watu wanaotoa maneno ya uchochezi dhidi ya Rais John Magufuli na Serikali.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Februari 13, 2019 jijini Arusha Lugola amesema wanaotoa maneno ya uchochezi kupitia simu zao, Blogs na makundi ya WhatsApp watasakwa popote na kuchukuliwa hatua za kisheria.
“Watanzania tumieni vizuri mitandao ya kijamii, msitumie kuvuruga amani ya nchi, usijidanganye unaweza kufanya uchochezi na usikamatwe,” amesema akidai watu hao wanamchonganisha Rais Magufuli na wananchi.
“Kama unatoa kauli za kumtukana Rais na uchochezi ina maana kuna watu nyuma wanakutuma,” amesema Lugola.
Chanzo: Mwananchi