...Jana (09/11/2011) niliangaliza movie moja saa tatu ama nne hivi usiku...DSTV Swahili. Nilikuta wakiangalia nyumbani, nami nikaungana nao. English subtitles zilikuwa mbaya mbaya mbaya...halafu kuna kijini mtu hicho wakati wote kinavuja tomato sauce mdomoni (eti wao wanatuaminisha kuwa ni damu)
Ni kweli tuna tatizo la ajira, lakini yatupasa tuwe makini na kazi zetu. Tufanye vitu vinavyofanana na ukweli ingawa ni vya kuigiza. Mara nyingi ukiangalia movie, kama ni ya ukweli...mtu huwa unasafiri na hiyo movie...lakini jana nilibaki palepale kwenye kochi nikikodoa macho...
Ushauri wangu ni kwamba, movie isirushwe hewani kama ina makosa dhahiri ya subtitles na makosa ya uhalisia.
Safari ni ndefu, ila nina imani wakuu wote wanaohusika wakiamua kufanya kweli...kila kitu kitawezekana; penye nia pana njia.
Ni kweli tuna tatizo la ajira, lakini yatupasa tuwe makini na kazi zetu. Tufanye vitu vinavyofanana na ukweli ingawa ni vya kuigiza. Mara nyingi ukiangalia movie, kama ni ya ukweli...mtu huwa unasafiri na hiyo movie...lakini jana nilibaki palepale kwenye kochi nikikodoa macho...
Ushauri wangu ni kwamba, movie isirushwe hewani kama ina makosa dhahiri ya subtitles na makosa ya uhalisia.
Safari ni ndefu, ila nina imani wakuu wote wanaohusika wakiamua kufanya kweli...kila kitu kitawezekana; penye nia pana njia.