Lowassa: TANESCO jiandaeni kuwajibika

Lowassa: TANESCO jiandaeni kuwajibika

Ocampo four

JF Senior Expert Member
Joined
Feb 28, 2014
Posts
5,789
Reaction score
2,159
Mzee wa maamuzi magumu na sahihi ambaye ni mgombea urais wa CHADEMA anayeungwa mkono na umoja wa Ukawa Ndg. Edward Lowassa kasema kuanzia tarehe 27 baada ya matokeo kutangazwa TANESCO waanze kuwajibika wenyewe kama hawatashughulikia hali ya umeme ipasavyo.

Lowassa kaonyeshwa kukerwa na mgao usiokoma kwa miaka zaidi ya 10, "kila siku ni mgao, mgao, huu mgao utaisha lini? TANESCO inalalamika, serikali yenyewe inalalamika. Sasa kama serikali na Tanesco wanalalamika na kukosa majibu mnategemea wananchi wakimbilie wapi?...alisema

Ni muda mrefu sasa nchi imekubwa na mgao wa umeme, na mbaya zaidi wananchi hawajui hali hii itakoma lini. Waathirika wakubwa wamekuwa wakina mama wajasiariamali, wafugaji wa kuku, vijana wanaojihangaisha kwa kupata ujira mdogo kama vinyozi wa saloon, vijana wenye ajira za kubangaiza viwandani, mama ntilie n.k

Ni jambo la kushangaza sana kuna mgombea ambaye ni waziri mwandamizi katika serikali hii lakini amekuwa akihaidi viwanda kila wilaya sasa sijui hivyo viwanda vitatumia power bank au?...

NB: Ninapoandika huu uzi tayari umeme ushakatwa..... Kwa hakika nchi inamuhitaji Lowassa kuondoa kero kama hizi....
 

Attachments

  • 1444195182176.jpg
    1444195182176.jpg
    45.9 KB · Views: 711
Tutawanyoosha tu. Na wale waliowapa wachina gas miaka 7 nao wajiandae. Lazima tuwanyonge
 
Hana lolote alishindwa kuwanyoosha akiwa waziri mkuu matokeo yake akaibuka na RICHMOND,Magufuli naamini atawanyoosha maana yeye hajawahi kushika hii wizara,walau naweza kusema alishindwa kuingilia wizara za wenzake.ILA LOWASA YEYE ALIKUWA MKUU WA WIZARA ZOTE
 
Hana lolote alishindwa kuwanyoosha akiwa waziri mkuu matokeo yake akaibuka na RICHMOND,Magufuli naamini atawanyoosha maana yeye hajawahi kushika hii wizara,walau naweza kusema alishindwa kuingilia wizara za wenzake.ILA LOWASA YEYE ALIKUWA MKUU WA WIZARA ZOTE

Alikaa muda gani kwenye nafasi ya waziri mkuu... Kwa muda wa miaka miwili alifanya jitihada kubwa sana, kwenye Richmond ambayo sasa ni Symbion na pia kuleta mvua ya Thailand...

Ufarasa hasa kaskazini mwa ufarasa wanatumia technologia ya Thailand... Sisi hapa kwa sababu CCM imetudumaza akili tunaona kama ni agano jipya... Poor CCM
 
hana lolote kazoea kupiga deal, safari hii kapigwa yeye na kina mbowe

Lazima patachimbika, pesa ya Mafia hailiwagi bure. Na nimjuavyo mchaga yule pesa akishaishika mkononi kuiachia ni ngumuu...
 
Alikaa muda gani kwenye nafasi ya waziri mkuu... Kwa muda wa miaka miwili alifanya jitihada kubwa sana, kwenye Richmond ambayo sasa ni Symbion na pia kuleta mvua ya Thailand...

Ufarasa hasa kaskazini mwa ufarasa wanatumia technologia ya Thailand... Sisi hapa kwa sababu CCM imetudumaza akili tunaona kama ni agano jipya... Poor CCM
Mvua ya Thailand ipo wapi,zaidi ya alipiga dili tu,hana lolote miaka miwili ni mingi sana kwa mtu kuonyesha impact zilizo positive kama kweli ana nia
 
Magufuli arudishe kwanza billion 262 alizoiba na CAG akathibisha.
 
Nampenda Lowasa maana ana maamuzi sahihi kabisa tena maamuzi yenye maana
 
Mgawo wa umeme umekuwapo nchini tangu mwaka 1992. Siwezi hapa kusisitiza adhari za kukosekana umeme wa uhakika kiuchumi na kijamii. Swali la kujiuliza ni je, hili tatizo litaendelea hadi lini? Jibu la swali hili lipo katika nukuu ya Mwanafizikia na Mwanafalsafa nguli wa karne ya 20 katika nukuu yake hii: "We can't solve problems by using the same kind of thinking we used when we created them". Tafsiri isiyo rasmi ni "Huwezi kutatua tatizo kwa kutumia akili hiyo hiyo iliyosababisha hilo tatizo liwepo". Maana yake ni kuwa chama hicho hicho kilichokuwa madarakani; mfumo huo huo; na sera hizo hizo vilivosababisha tatizo la mgawo wa umeme havitaweza kamwe kuliondoa.
 
Back
Top Bottom