Lowassa: Sikuhitajika na Wakubwa!

Lowassa: Sikuhitajika na Wakubwa!

Ozzie

JF-Expert Member
Joined
Oct 9, 2007
Posts
3,217
Reaction score
1,266
Wanabodi!

Kuna email ya shukrani imetumwa na Lowassa kwa baadhi ya wafuasi. Si mbaya, lakini haitoi hatima yake kwa sasa, na bado anahitaji maombi yenu.

Tumuombee.

Dear xxxx xxxx

Ninapenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru marafiki zangu wote mnaoniunga mkono na kuniombea. Pia ni masikitiko yangu kwamba sikuhitajika na wakubwa zangu katika kugombea nafasi ya urais.

Naamini Mungu anajua sababu zilizopelekea kuzima ndoto zangu lakini namshukuru kwakuwa amenitia nguvu sana kwani haikuwa rais sana kukutana na maamuzi hayo na kejeli za wazi. Naomba usiache kuniombea ili niyafanye yanayompendeza Mungu katika kipindi hiki kigumu.

Mungu ibariki Tanzania na watu wake

Hon. Edward N. Lowassa

Regards: Edward Lowassa Official Online Office.
 
Aulizwe kama atamuunga mkono na kumpigia kampeni Magufuli. Ashukuru kikombe kimemuepuka

Mzee Tupatupa
 
Na wale wengine 38 VP? Kwani hakujua n mmoja tu atakayepita? Nchi haiongozwi kwa ndoto
 
Tuko nae till the end...Mungu anakusudi na huyu mzee.Saa ya ukombozi imewadia.Misukosuko aliopitia huyu mzee ina hatima njema.Mungu sio dharimu na wala hadhihakiwi.
 
Waliokuwa wanamsifia lowassa na kujitapa kuwa "hakatwi mtu hapa" mbona siwaoni tena?
 
Tatizo huyo mzee wao hakusoma alama za nyakati. Angejua mapema angeishia kulee!! Arumeru kwa mkwelima wake.
 
Haikuandikwa sehemu kuwa atakuwa Rais wa Tanzania, wala hatuhitaji Rais wa ndoto
 
Ozzie

Kama ni mm presha ingeniua
 
Last edited by a moderator:
Kuna watu humu jf walimshauri vizuri sana hakutaka kuwasikia, na bado wanaendelea kumshauri na ushauri wenyewe ni huo wa kumtaka apumzike, afanye mambo yake tofauti na siasa lkn naona bado mzee wa Monduli kashupaza shingo, mwisho itavunjika......nimegundua washauri wake wanashinikizwa na hela ila hapa JF wanaangalia uhalisia.
 
Tuko nae till the end...Mungu anakusudi na huyu mzee.Saa ya ukombozi imewadia.Misukosuko aliopitia huyu mzee ina hatima njema.Mungu sio dharimu na wala hadhihakiwi.

Mungu hana kusudi naye ndio maana kawatia nguvu kamati ya maadili kumuondoa mapema....
Kama bado unampenda mfanye kuwa raisi wa ukoo wako....
 
.... "haikuwa rais sana kukutana na maamuzi hayo".......???
 
ww sifongo mbona hujapumzika humu JF!? Acha kebehi! Hii nnchi siyo yenu pekeyenu na wala ww hunamamlaka na maamuzi ya mtu mwingine!
 
Back
Top Bottom