Lowassa sema ukweli

Omuchimati

JF-Expert Member
Aug 23, 2014
427
202
Lowassa sema ukweli,ukweli utakuweka huru,ila usiposema kweli na kutenda kweli utashindwa kuwa huru mzee,waambie ndugu zangu wa Chadema kwamba hukwenda kwa ajili ya chama chao,ulienda kutafuta kichaka cha kujificha ukitegemea swala apite kando yake umle(URAIS) na ndio hoja umesimama nayo mpaka leo,wameshindwa kukuelewa, wengine wanakuona kama msukule uliovamia nyumba ya walio hai, wanajuta kwanini viongozi wao waandamizi walikukaribisha ndani ya chama,kwa kawaida majuto huwa mjukuu.

Kweli nyingine ni kuwa wewe ni mwana ccm kidakidaki, ukitaka upumzike kwa amani mzee wangu rudi ndani ya chama utubu, uzuri wana ccm hawamkatai mtu wewe ndie unajikataa mwenyewe,naomba unielewe kama yule mfalme alieambiwa akaoge mara saba ndani ya mto Yordani, nawe kafanye hivyo mzee wangu LOWASSA, uko ulipo unawatesa wana Chadema na kujitesa mwenyewe pia.........MKIIJUA KWELI NA KUITENDA MTAKUWA HURU KWELI KWELI.
 
Lowassa anawaumiza sana wanaccm ndo maana kila siku lazima wamtaje, ccm huwezi kuelekeza jambo jema la kuimalisha upinzani bali haya ni machozi ya mamba, Lowassa kaza Uzi
 
Lowassa sema ukweli,ukweli utakuweka huru,ila usiposema kweli na kutenda kweli utashindwa kuwa huru mzee,waambie ndugu zangu wa Chadema kwamba hukwenda kwa ajili ya chama chao,ulienda kutafuta kichaka cha kujificha ukitegemea swala apite kando yake umle(URAIS) na ndio hoja umesimama nayo mpaka leo,wameshindwa kukuelewa, wengine wanakuona kama msukule uliovamia nyumba ya walio hai, wanajuta kwanini viongozi wao waandamizi walikukaribisha ndani ya chama,kwa kawaida majuto huwa mjukuu.

Kweli nyingine ni kuwa wewe ni mwana ccm kidakidaki, ukitaka upumzike kwa amani mzee wangu rudi ndani ya chama utubu, uzuri wana ccm hawamkatai mtu wewe ndie unajikataa mwenyewe,naomba unielewe kama yule mfalme alieambiwa akaoge mara saba ndani ya mto Yordani, nawe kafanye hivyo mzee wangu LOWASSA, uko ulipo unawatesa wana Chadema na kujitesa mwenyewe pia.........MKIIJUA KWELI NA KUITENDA MTAKUWA HURU KWELI KWELI.
Kilicho nishangaza nipale Lowassa alipochukua fom kugombea urais ccm wana ukawa pamoja na viongozi wao walishangaa sana mmoja wapo ni mbowe alisema "yaani ccm wamempa huyu fisadi fom agombee urais" na tundu lissu alisema "kweli nchi imfika pabaya yaani lowassa anagombea urais" sasa alipokatwa akaenda kwao wakamsafisha wakamuita nabii sasa wanashangaa tena eti kwanini wananchi wameancha kumpa kura mtu anayetaka kulitetea taifa, hivi huoni hii ni njia yakuonyesha kua upinzani hawana sera bali wao wanachotaka nikuharibu wananchi ki fikra
 
Lowassa anawaumiza sana wanaccm ndo maana kila siku lazima wamtaje, ccm huwezi kuelekeza jambo jema la kuimalisha upinzani bali haya ni machozi ya mamba, Lowassa kaza Uzi
Hivi Lowassa unayemzungumzia niyule chadema walikua wanamuita fisadi au kuna mwingine?
 
Tangu lini umekua na huruma dhid ya cdm? Muache lowasa aimalize cdm ili iwe furaha kwa ccm. Watz kwa umbeya hamjambo
 
Ujio wa Lowassa CHADEMA umeua rasmi vita dhidi ya ufisadi.
Matokeo ya kupoteza agenda na kujiongelea vitu visivyoeleweka tumeyaona kwenye uchaguzi mdogo.
 
Pamoja na mapungufu yaliyofanyika wakati wa kumteua kugombea urais kwa tiket ya chadema, bado taifa linamhitaji mtu kama yy kuwa nje ya chama tawala kutoa changamoto kwa serikali
 
Back
Top Bottom