Lowassa: Niko tayari kufa nikitetea Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya

mpk

JF-Expert Member
Sep 26, 2012
3,115
3,864
"NIKO TAYARI KUFA NIKITETEA TUME HURU YA UCHAGUZI NA KATIBA MPYA"

Kama kwaida ya CCM wao hushangilia kila kitu na kuwaaminisha viongozi wao kwamba wanafanya vizuri hata kama wanaelekea shimoni. Ndiyo! Kwani wanaomshangilia Magufuli si wale wale waliomshangilia Kikwete? Naamini hata kama Magufuli angewaudhi namna gani hili la kuzuia mikutano ya upinzani watamshangilia mpaka jino la mwisho litaonekana. Naambiwa pia Dkt Tulia alimwagiwa sifa kedekede jana kwenye kikao cha CC ya CCM.

Hata hivyo napenda kuwakumbusha viongozi wangu hawa kwamba wanaposhangiliwa leo na hawa wanaoshangilia kila kitu wajiandae kuzomewa au kukejeriwa na hao hao wanaowashangilia. Kama hawaamini maneno yangu wamuulize mzee Kikwete. Lakini pia wakumbuke kwamba kuua upinzani si kazi rahisi, kama hawaamini wamuulize mzee Mkapa na Dr Salimin. Walitumia nguvu zao zote kuua upinzani ukashindikana.

Natabiri kipindi cha cha Magufuli kuibuka kina Dr Besigye wa Tanzania. Dr Besigye alivunja rekodi ya dunia kwenye kampeini za Uganda alipokamatwa na kushitakiwa mara 7 kwenye mwezi mmoja na leo tunavyoongea yuko ndani kwa tuhuma za uaini. Jana nilimuona Lowassa akisema yuko tayari kufa kutetea katiba mpya na kudai tume huru ya uchaguzi!

Kuna aliyetegemea kauli nzito namna hiyo toka kwa mwanasiasa mstaarabu na mpole kama Lowassa?
 
lowassa hana jipya!! BAVICHA tulieni dawa iwaingie, nguvu ya dola itatumika!! unaposema mkapa alitumia nguvu hivyohvyo ili kuua upinzani waziri mkuu wake alikuwa sumaye
 
lowassa hana jipya!! bavicha tulieni dawa iwaingie, nguvu ya dola itatumika!! unaposema mkapa alitumia nguvu hivyohvyo ili kuua upinzani waziri mkuu wake alikuwa sumaye
Acha Sumaye hata angekuwa Mbowe. Je aliweza kuua upinzani?
 
Kuna kila dalili CHADEMA imebinafsishwa, sasa hivi ni mali ya mtu mmoja tu ambaye yuko tayari kuipasua nchi vipande vipande ili awe rais. Wale 'marafiki' waliokuwa wanachanga mamilioni ya harambee bado wapo?
 
Hahahahahaha
Huyu ashaahidigi mvua za kutengeneza bahati mbaya dili.lilibumbuluka na baadae akapigwa chini uPM kutokana na tuhuma za ufisadi kutoka kwa wabunge wa chadema miaka hiyo.

Jamaa ni bonge la msanii
 
Kauli nzito zaidi kuwahi kutolewa na huyu mzee wetu ni pale aliposema atamleta balali na kumtoa babu seya na kuwaachia huru mashekhe wa uamsho,katiba mpya na tume huru alizipinga wakati yupo ccm hakujua kama kesho kuna maisha mengine,anatung'ong'a rafiki yake hakukutana nae barabarani!
 
Ina uzito gani? Hayo maneno hujawahi yasikia? Mbona alishasema "Jk is a visionery" kisha akasema "rafiki yake JK is a monster"
"NIKO TAYARI KUFA NIKITETEA TUME HURU YA UCHAGUZI NA KATIBA MPYA"

Kama kwaida ya Ccm wao hushangilia kila kitu na kuwaaminisha viongozi wao kwamba wanafanya vizuri hata kama wanaelekea shimoni. Ndiyo! Kwani wanaomshangilia Magufuli si wale wale waliomshangilia Kikwete? Naamini hata kama Magufuli angewaudhi namna gani hili la kuzuia mikutano ya upinzani watamshangilia mpaka jino la mwisho litaonekana. Naambiwa pia Dkt Tulia alimwagiwa sifa kedekede jana kwenye kikao cha CC ya Ccm.

Hata hivyo napenda kuwakumbusha viongozi wangu hawa kwamba wanaposhangiliwa leo na hawa wanaoshangilia kila kitu wajiandae kuzomewa au kukejeriwa na hao hao wanaowashangilia. Kama hawaamini maneno yangu wamuulize mzee Kikwete. Lakini pia wakumbuke kwamba kuua upinzani si kazi rahisi, kama hawaamini wamuulize mzee Mkapa na Dr Salimin. Walitumia nguvu zao zote kuua upinzani ukashindikana.

Natabiri kipindi cha cha Magufuli kuibuka kina Dr Besigye wa Tanzania. Dr Besigye alivunja rekodi ya dunia kwenye kampeini za Uganda alipokamatwa na kushitakiwa mara 7 kwenye mwezi mmoja na leo tunavyoongea yuko ndani kwa tuhuma za uaini. Jana nilimuona Lowassa akisema yuko tayari kufa kutetea katiba mpya na kudai tume huru ya uchaguzi!

Kuna aliyetegemea kauli nzito namna hiyo toka kwa mwanasiasa mstaarabu na mpole kama Lowassa?
 
Kauli nzito zaidi kuwahi kutolewa na huyu mzee wetu ni pale aliposema atamleta balali na kumtoa babu seya na kuwaachia huru mashekhe wa uamsho,katiba mpya na tume huru alizipinga wakati yupo ccm hakujua kama kesho kuna maisha mengine,anatung'ong'a rafiki yake hakukutana nae barabarani!
Kwani angekuwa amiri jeshi mkuu asingeweaza? Tuambie, Magufuli hajui Balali alipo? CCM ni ile ile
 
Hana lolote huyo, ni mwana ccm aliyeasi kwa uchu wa madaraka, hana hadhi ya kuwa rais toka 1995 anasaka urais hajapata zaidi ya kukatwa tu. Ila nyumbu wanakwambia alipo wapo..
Leo mbona mnamshangilia Wassira na Makongoro waliowahi kuwa upinzani mpaka wakawa wabunge? Acha ubaguzi wa hovyo!
 
Back
Top Bottom