Lowassa ni Superpower, amemzidi maarifa Shetani

Lowassa ni Superpower, amemzidi maarifa Shetani

Hussein Massanza

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2012
Posts
1,016
Reaction score
2,195
Mchambuzi George Hope wa Uingereza, aliuchambua Uchaguzi Mkuu wa nchi hiyo, uliofanyika Mei, 7, mwaka huu kuwa ulikuwa mkubwa kuliko siasa za vyama, andiko lake lilibeba kichwa; This Election is far bigger than Party Politics.

Vilevile mchambuzi Chris Trueman wa Marekani, aliwahi kueleza kuwa siasa za vyama zinapotea na badala yake nguvu ya ushawishi wa mtu mmoja inakuwa mtaji mkubwa. Kwa maana mwanachama wa Republican siku hizi humpigia kura mgombea wa Democrat kutokana na mvuto wake.

Kwamba, Barack Obama wa Democrat aliweza kumshawishi Colin Powell wa Democrat na kutangaza hadharani kwamba anamuunga mkono, akaahidi kumpigia kura na kushawishi wana Republican wengine kumchagua Obama. Powell alikuwa alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje katika muhula wa kwanza wa Rais George Bush.

Powell alisema alishawishika kumuunga mkono Obama kwa sababu hotuba zake zilimpambanua kama mtu mwenye maono ya kiwango cha juu katika kuistawisha Marekani.

Binafsi naunga mkono maneno hayo kwa kuchukua hoja hizo za Hope na Trueman kisha kuzioanisha na hali halisi nchini. Bila shaka, nguvu kubwa ya mgombea wa Chadema na Ukawa, Edward Ngoyai Lowassa, imekuwa na mapinduzi makubwa.
Kwanza tuseme kweli kuwa matokeo ya sasa yanadhihirisha kwamba Lowassa ni zaidi ya Chadema, na msuli wake ni mkubwa kuliko wa Ukawa. Tunaweza kukubaliana kwamba safari ya Lowassa Chadema imechagizwa na udhaifu wa sheria za nchi.

Laiti sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zingekuwa zinaruhusu uwepo wa Mgombea Binafsi, Lowassa asingeingia Chadema wala asingefunga ndoa na Ukawa. Angesimama peke yake na mshikemshike huu unaonekana sasa, ungekuwepo bila punguzo.

Lowassa hakuhitaji kuingia Chadema kwenda kumpa unyonge Dk. Willibroad Slaa aliyeamua kujiweka kando na chama chake, wala hakuwa na kusudio la kwenda kumkimbiza Profesa Ibrahim Lipumba Cuf na Ukawa. Lowassa hakuwa na namna.

Anaufikiria Urais, na kwa njia anazopita, inamtaka awe mcheza mpira mgumu (a hardball performer) ili kufanikisha malengo. Hata kama anajua anaumiza wengine, hana namna ya kuwatuliza. Kokoro au mkwabo kwa lugha ya Kigoma, hukusanya na visivyohusika.

Jinsi Lowassa anavyouelekea Urais, ni sawa na askari anayetumia kombora la kivita kumuua mtu mmoja, linapolipuka huua na kujeruhi walio karibu na mlengwa. Pale alipo Lowassa anamhurumia Slaa, anamsikitikia Lipumba lakini hana njia nyingine za kuwafurahisha. Mgombea binafsi angekuwa anaruhusiwa, pengine asingewajeruhi.

Kufikia hapo hatutapingana kuwa Lowassa amebadili siasa za nchi. Amekuwa ni kiungo kitamu katika uchaguzi wa mwaka huu. Amesababisha mvumo mkali ambao umewazindua hata wanaopenda kuilalia siasa, nao wameshtuka na kuifuatilia.
Amekuwa sababu ya walevi wa michezo na burudani, waliokuwa wakiita siasa uzushi, nao sasa ni washereheshaji wazuri wa mada za kisiasa vijiweni, ndani ya familia na zaidi kwenye mitandao ya kijamii.

Lowassa ni kiungo kinachoweza kumpa hamu ya chakula asiyejisikia au aliyekinahi. Ndiyo maana waliokuwa wakiisema vibaya Chadema kuwa chama cha hovyo, siku hizi ndiyo kimbilio lao. Rejea matamko ya nyuma ya Dk. Milton Makongoro Mahanga, Goodluck ole Medeye na wengineo waliomfuata Lowassa Chadema.


John Guninita aliwahi kujiondoa CCM miaka ya 1990 kisha akawa mpaka Naibu Katibu Mkuu wa Chadema. Aliporejea CCM alisema maneno mengi ya hovyo kuhusu vyama vya upinzani na Chadema. Leo amerejea Chadema kwa sababu ya Lowassa. Unaweza kurejea misimamo ya Khamis Mgeja, halafu fikiria tu kuwa sasa ni mwanachama wa Chadema.


Lowassa ni superpower! CCM yenyewe imesinyaa, hayo matokeo ya Slaa na Lipumba ni rashasharasha tu. Mgeuko wa akina Mgana Msindai kukimbilia Chadema ni kijiupepo tu! Kimbunga chenyewe ni jinsi ambavyo CCM imekuwa kimya, Lowassa anatamba.


Tusipime msafara mdogo wa Dk. John Magufuli kwenda kuchukua fomu kwa ule wa Lowassa. Ambako tunatakiwa kuuona ukubwa wa Lowassa ni namna ambavyo vyombo vya habari vinavyosema naye katika sura chanya kuliko mgombea wa CCM.


Ipo hoja kuwa Lowassa amenunua vyombo vya habari, swali ni je, Lowassa ana pesa kuliko CCM? Tunaambiwa kuwa hata Chadema na Ukawa amewanunua, tujiulize, kama kweli hilo limewezekana, hatuoni kama huyo mtu ana uwezo mkubwa kuliko sayari hii?


Magazeti yaliyokuwa yanamuandama kwa kashfa za ufisadi, leo hii yanampamba vizuri. Waandishi waliowahi kutunukiwa tuzo kwa eti ni hodari wa kuchimbua madudu ya Lowassa, kwa sasa ndiyo watengeneza mapambio ya Lowassa. Ukiona hili ni la kawaida shauri yako!

Ni Lowassa peke yake ameweza kumzidi maarifa Shetani. Inajulikana binadamu ni watenda dhambi sana. Na kwa mujibu wa maandiko maratakatifu ya vitabu vyote, Torati, Zaburi, Injili na Kuran, anayeanguka dhambini anakuwa amepita njia ya Shetani.


Pamoja na binadamu kushawishiwa na Shetani kisha kutenda dhambi, haijawahi kutokea binadamu kumsema vizuri Shetani. Mtu anaweza kukutwa kitandani na mume au mke wa mtu lakini katika kujitetea, atamsema Shetani kuwa chanzo cha dhambi alizotenda.


Binadamu anaweza kucheza kamari kisha akamuomba Mungu amsaidie apate ushindi. Akishindwa na kuliwa fedha, papo hapo kibao kinageuka, anamlaani Shetani kwamba ndiye aliyemshawishi kucheza kamari ambayo ni haramu mbele ya Mungu.


Haijawahi kutokea binadamu kumsema vizuri Shetani na haitakuja kutokea. Binadamu akizaliwa, majina ya mwanzomwanzo kuyakamata mojawapo ni la Shetani, kwamba ni jitu baya. Tunaambiwa Shetani alikuwa malaika, tena ni ana sura nzuri (handsome) lakini michoro kuhusu Shetani ni ya kutisha.


Haitakuja kutokea binadamu amchore Shetani kwa sura na umbile zuri. Jambazi anavamia, anaua na kupora pesa lakini baada ya wizi hapigi goti na kumshukuru Shetani kwa kumpa maarifa ya ujambazi. Mbakaji anapokamilisha ushetani wake, hatamshukuru Shetani, badala yake atamlaani.

Lowassa ameweza kuwageuza waliomwita Shetani, sasa ndiyo wanaompamba kwamba ni malaika. Shetani anahitaji kukutana na Lowassa ili ampe maarifa. Kama imewezekana kwa Freema Mbowe na Tundu Lissu, watu wenye misimamo mikali. Kuna kitu cha kujifunza hapa!


Hapa inabidi Shetani mwenyewe aache ubishi, kila siku yupo kwenye maisha ya kawaida ya binadamu, anashirikiana nao kutenda dhambi lakini baada ya matukio na matokeo, huwa hawawi pamoja. Inawezekana Lowassa akamsaidia Shetani maarifa, jinsi ya kumgeuza anayekusema vibaya leo, kesho akuseme vizuri na kukushabikia.


Ninapowaza jinsi Lowassa alivyomzidi maarifa Shetani, nakosa namna ya kumlinganisha na CCM. Sishangai kuona siku Magufuli alipokwenda Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), kwenye vyombo vya habari halikuwa jambo la kushtua. Lowassa zamu yake ilipowadia, ikawa mtikisiko wa Jiji la Dar es Salaam.


Labda swali la kujiuliza ni hili; Lowassa amepata wapi maarifa ya wageuza waliomwita Shetani, leo wamnadi kuwa ni malaika? Nguvu za kuishinda CCM kushawishi vyombo vya habari kumuandika vizuri kila siku anazipata wapi?

Nguvu za kuwafanya akina Mbowe kumuona Slaa siyo lolote wala chochote siyo ndogo. Zinahitaji kuhojiwa! Zinapatikana wapi? Ni Lowassa mwenyewe peke yake? Msuli gani umetumika kuwafanya Cuf wamuone Lipumba si mali kitu tena, wakati walipata kumtukuza kama ‘Mungu-Mtu' wao?


Hiki kimbunga chake kinachotawala vyombo vya habari, vikiwemo vile ambavyo viliwahi kuwa adui yake namba moja, kina msaada wa nani? Waandishi waliotangaza kuwa wanawindwa wauawe na Lowassa, leo hii ndiyo maswahiba wake. Haya maarifa ya Lowassa siyo tu yanapaswa kuigwa na Shetani, hata Marekani.


Pengine siku zijazo Marekani wakishafanya mazungumzo na Lowassa, wataweza kuwafanya Wairan wawapende. Labda Marekani itawafanya Wapalestina, Walebanon, Waafghanistan, Wairaq na wengineo kuacha ugaidi na kuanza kuwa watetezi wa taifa hilo kubwa duniani.


Wanaompinga, wakati wanatoa hoja hasi dhidi ya Lowassa, lazima wawe wanakiri kuwa huyu mtu ni superpower, ana uwezo mkubwa wa kuyafanya yasiyowezekana yawezekane kirahisi kabisa. Kwa nini Magufuli siyo kipaumbele cha vyombo vya habari kwa sasa? Je, CCM haina uwezo wa kushawishi? Ameizidi maarifa CCM.


Wanaomshabikia, siyo kushangilia tu, ni vizuri kujiuliza nguvu alizonazo zinatoka wapi? Tusipuuze hoja kuwa amewekeana ahadi na watu kuhusu rasilimali za nchi yetu. Tuwaze mmojammoja, ni biashara gani inapigiwa chapuo baada ya Lowassa kuingia Ikulu?


Binafsi nawaza huu mkumbo (bandwagon) unachagizwa na nini? Sasa imekuwa fasheni kumshabikia Lowassa. Wale ambao siyo timu Lowassa wanaonekana hawaendi na wakati. Mwaka 1997, Charles Taylor ndiye alikuwa bandwagon wa Liberia. Watu hawakuambiwa kitu!


Taylor alimwaga fedha kwa vijana katika Uchaguzi Mkuu wa Liberia 1997. Pamoja na makatazo mbalimbali, watu hawakuambiwa kitu. Mwisho, Taylor alishinda kwa kishindo. Baada ya ushindi, Waliberia wanajuta mpaka leo. Tuwe makini tunapoutazama Uchaguzi Mkuu 2015.


by Luqman Maloto

 
Shule hazina walimu wa. Mashairi ingefaa kama ungewasaidia.
 
Afadhali kuwa Liberia kuliko kuendelea kuwa chini ya utawala wa CCM......

Kwanza CCM iondoke, mengine yatafuata baadaye. Nchi hii si MALI YA CCM na familia zao.

Mtabana weee na vitisho vyenu ila mwisho GOLI mtapigwa na TBC zenu.

 
Last edited by a moderator:
Mkuu umeandika vizuri kwa hoja lakini ndo hivyo tena kila shetani na mbuyu wake. You can feel some people....
 
Huyo mzee wako ni supa kwenye ufisadi tu wala siyo kuwatumikia watanzania.
 
Sure Lowassa ni super power na kamzidi shetani ujanja,mimi mwenyewe sijui kanishawishi vipi,maana alipokua ccm nilisema na niliandika humu kwamba ikiwa atapiyishwa kua mgombea uraisi basi mimi ntahamia sudani kusini au yemeni au somalia,nikasema bora kuishi huko kuliko kuishi na Lowassa akiwa rais.

Lakini sasa ni mshabiki wake huniambii kitu kuhusu Lowassa,Lowassa ndie tumaini langu jipya,lowassa ndie mkombozi wa watanzania. Lowassa sijui kafanyaje kunishawishi lakini yote tisa kumi lowassa ndie chaguo langu na chaguo la watanzania.

Nguvu ya lowassa ni kubwa kuliko ccm na vyama vingine vyote vya siasa. Kwenye fair competition ground ccm hawawezi kusimama dhidi ya Lowassa,Lowassa ni heavy weight na ccm ni light weight au feather weight,he will know them out very early in the morning on 25 october 2015.

Back to topic. Umetoa mifano mizuri ya obama na taylor lakini umehitimisha kwa mabaya ya taylor, fine, mbona hujasemea mazuri ya obama baada ya kuungwa mkono hata na wapinzani wake ambacho ndicho kitu kinafanyika sasa kwa Lowassa. Lowassa ni sawa na Obama.
 
Angegombea kupitia CCM usingeandika hivi CCM bora watoke tuanze upya hatuna Namna nyingine
 
Huyu anaweza kuwa zitto japokuwa anaweza asiwe yeye pia ila hiyo hoja ya kujiuliza nguvu za Lowassa zinapotoka asisahau kujiuliza ccm wanashindaje miaka yote 50 ya shida. Na maendeleo ya kusuasua utadhani nchi hii ni ya vita kumbe tuna amani tele ila maendeleo haba hapa jibu lako ni moja tuu watu wamechoka wanataka maendeleo hata kama hayapatikani ccm basi yanatafutwa ukawa sasa tusaidiane kufanya ukawa walete maendeleo tarajiwa kwa wote na sio kugombea fito wakati tunataka kujenga nyumba moja ya mabadiliko usipoelewa mabadiliko hayakusubiri wewe yatakusomba na mafuriko utajikuta uko kwenye njia ya mabadiliko tukutane oct na Nov serikali mpya kazini.
 
Mtoa mada kaandika maneno mengi ambayo nahisi hayajui!!lowassa anashabikiwa sana kwa sababu ndiye mtu pekee aliyeweza "kuimegua ccm"vipande viwili.kuishinda ccm iliyo "wamoja"ni ngumu,sharti lazima imeguke.kilikuwa ni kikundi "ovu"chenye "mrengo mbaya" wa wizi,ukatili na kuogofya!kwa namna kundi hili la "ujambazi" lilivyokuwa limejipanga kulikuwa hakuna hamna ya "kuliondoa".

Hivyo kuchaguliwa kwa lowassa kuna maana tatu kubwa 1.watanzania kwa sasa wako "radhi"kuhakikisha wanaitoa ccm kwa "njia"yoyote ile.narudia "njia yoyote ile".

2.mungu ndiye "muweza ya yote",na humpa amtakaye yule awaye yote.kwa akili ya kibinadamu,haikuwa rahisi kuamini kuwa kamati kuu ya chadema ingemkaribisha lowassa kama mwanachama achilia mbali kumpitisha kama mgombea kupitia chadema.mungu akiamua hakuna mwenye uwezo wa kuzuia.

3.binadamu hubadilika kimtazamo.fikra zetu hubadilika kadri mazingira yanavyotubadilisha.biblia inatuambia hata "mungu" hubadili "mawazo,soma wakati wa nuhu baada ya gharika lile,mungu aliona "huruma" na kuahidi "kutoua"tena kwa "maji".soma pia story ya "rutu"sodoma na gomora.ambapo mungu pia aliona "huruma"na kuahidi kutoua tena kwa "moto".

Kwa namna mambo yanavyokwenda hakuna namna ambayo ccm inaweza kushinda uchaguzi huu.hakuna!!!!nakuhakikishia kila mbinu "itafunuliwa". Sababu ni moja tu "mungu kaamua,basi".kama huamini,tunza uzi huu mpaka tarehe 25 october 2015 utakuja kukiambia.
 
Lowassa hazuiliki hata kidogo.... CCM sasa imefikia wakati kibadili jina na kuitwa chama cha WAMA.....
 
Ipo hoja kuwa Lowassa amenunua vyombo vya habari, swali ni je, Lowassa ana pesa kuliko CCM?
 
Sure Lowassa ni super power na kamzidi shetani ujanja,mimi mwenyewe sijui kanishawishi vipi,maana alipokua ccm nilisema na niliandika humu kwamba ikiwa atapiyishwa kua mgombea uraisi basi mimi ntahamia sudani kusini au yemeni au somalia,nikasema bora kuishi huko kuliko kuishi na Lowassa akiwa rais.

Lakini sasa ni mshabiki wake huniambii kitu kuhusu Lowassa,Lowassa ndie tumaini langu jipya,lowassa ndie mkombozi wa watanzania. Lowassa sijui kafanyaje kunishawishi lakini yote tisa kumi lowassa ndie chaguo langu na chaguo la watanzania.

Nguvu ya lowassa ni kubwa kuliko ccm na vyama vingine vyote vya siasa. Kwenye fair competition ground ccm hawawezi kusimama dhidi ya Lowassa,Lowassa ni heavy weight na ccm ni light weight au feather weight,he will know them out very early in the morning on 25 october 2015.

Back to topic. Umetoa mifano mizuri ya obama na taylor lakini umehitimisha kwa mabaya ya taylor, fine, mbona hujasemea mazuri ya obama baada ya kuungwa mkono hata na wapinzani wake ambacho ndicho kitu kinafanyika sasa kwa Lowassa. Lowassa ni sawa na Obama.

Hakika Mwandishi umejitahidiila katika hitimisho, lengo lako si zuri.Lowasa wa sasa na ajayenamfananisha na SAULI katika maandiko ya Mungu.

Sauli alitesa sana watumishiwa Mungu na yeyote aliye taja jina la Bwana. Sauli alikuwa jeuri kuliko kawaidalakini alikuja kubarikiwa na kuwa mcha mungu kuliko mitume wengine tena waliofanya kazi ya Mungu kwa muda mrefu!Mungu hutenda miujiza, iwejeleo mimi nimsifie Lowasa!?

Ujio wa Lowasa katika UKAWAni fulsa kwa Watanzania kuimarisha Demokrasia na kuleta historia ya kuwa na Uchaguzi Tanzania wenye mvuto na ushindani sawia wa hali ya juu dhidi ya Chama Tawala CCM chenye Serikali na kila kitu.

Kama alivyosema Prof Baregukatika Mdahalo katika ukumbi wa Blue Peal Jijijini Dar Es Salaam trh16.08.2015, wakati wakijadili Haki, Amani na Maadili kuelekea Uchaguzi Mkuu Oct2015, kuhusu Richmond, kwamba hana taarifa nyingine zaidi zinazo mhusu Lowasa juu ya uhusika wake / madhambi yake isipokuwa Report ya Kamati ya Bungechini ya Dr Mwakyembe. Vivyo hivyo hata mimi pengine hata mleta uzi huuhana taarifa nyingine zaidi ya hilo kuhusu uhusika wa E. Lowasa na Richmond.


Sauli huyu wa UKAWA anaweza kufanya maajabu kama alivyo fanya Sauli wa Yesu / Mungu. Iliwachukua mudawafuasi wa Yesu kumwelewa Sauli na kuamini kama kweli ameachana na madhambi yake. Tofauti na Sauli ambaye matendo yake yalikuwa bayana, madhambi ya Lowasa hayana uhakika bila kuacha shaka mbele yamacho ya kisheria.
Mwizi, mbakaji, au vyovyote vile utakavyo penda kumwita mbaya wako kwa kitendo alicho kufanyia, kama huwezi kuthibitisha kisheria kwamba kweli kakutendea hivyo ataendelea kuwa rafiki yako.

Nukuu isiyo rasmi ya Prof Baregu,

“Kama majambazi yapomafichoni na yanapanga kugawana walicho kuibia, mojawapo akatoka akaja kukupataarifa za wabaya wako walipo, utamdhuru au utampenda?”


Nakutakia tafakuri njema na mpya juu ya Lowasa!
 
Back
Top Bottom