Lowassa mbona amehamia Zanzibar?

Lowassa mbona amehamia Zanzibar?

GHIBUU

JF-Expert Member
Joined
Jan 13, 2011
Posts
4,432
Reaction score
3,016
Wakati lowasa akiwa waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania sijui kama alifika zanzibar na kama alifika kwa sherehe za mapinduzi ya zanzibar.

Hivi karibuni nimekuwa nikiona habari akitembelea zanzibar sehemu mbalimbali, wazee wa zanzibar akiwatembelea mawaziri wastaafu pamoja na maraisi na miradi ya zanzibar.

Jee huyu lowasa amefikwa na nini? :what:
 
Edward Lowassa alipo mtembelea Ali Amer
 

Attachments

  • 1420227629544.jpg
    1420227629544.jpg
    91.7 KB · Views: 465
Anataka support ya uraisi kupitia kwa wazanzibar,amechelewa sana,hela watu watakula na 2015 ni mamlaka kamili kwa wazanzibar.
 
GHIBUU,

..kura za Znz ni muhimu ktk kinyang'anyiro cha kumpata mgombea Uraisi kupitia CCM.

..umesahau mwaka 95 jinsi wa-Znz walivyopiga kura kama kundi kumpitisha Mkapa dhidi ya Kikwete?
 
Last edited by a moderator:
Lowassa anahangaika sana uraisi ataishia kuusikiliza kwenye radio tuuu.
 
GHIBUU,

..kura za Znz ni muhimu ktk kinyang'anyiro cha kumpata mgombea Uraisi kupitia CCM.

..umesahau mwaka 95 jinsi wa-Znz walivyopiga kura kama kundi kumpitisha Mkapa dhidi ya Kikwete?

Wakipa urais halafu ndio wa kwanza kuikandamiza zanzibar na watu wake, kuwatisha vile vile, wamesahau bunge la Katiba walivyo watisha wazanzibari waka ufyata
 
Last edited by a moderator:
Wakipa urais halafu ndio wa kwanza kuikandamiza zanzibar na watu wake, kuwatisha vile vile, wamesahau bunge la Katiba walivyo watisha wazanzibari waka ufyata

..inategemea unazungumzia wa-Znz wapi.

..hivi ulitegemea Mkapa amtupe Dr.Salmini ktk wizi wake wa kura za uchaguzi wa 95?

..mpango wenyewe uko hivi: Mznz anamsaidia Mtanganyika kupita kinyanganyiro cha CCM, halafu Mtanganyika anamsaidia Mznz kuiba kura za uraisi na uchaguzi mkuu wa Znz.

..usifikiri kwamba wa-Znz wanakandamizwa tu na wa-Tgk bila ya kuwepo wa-Znz wanaoshiriki na wanaofaidika na ukandamizwaji huo.

cc Barubaru, Gs-300
 
Last edited by a moderator:
Shida nini mbona Kariakoo yote wamejaa wapemba
 
Huyu Mzee wa kutetemeka angetulia tu, hatakaa awe rais wa Tanzania
 
Aliyekuambia waziri mkuu ni cheo cha Muungano nani? mpaka aje Zenzi kipindi hicho,
 
pigeni vijembee wee,mwisho mtamwona ikulu.
team lowassa
 
Back
Top Bottom