Falsafa ya kutawala na kutawaliwa:
Anayetawala anapomkosea mtawaliwa, mtawaliwa makini humpa mtawala muda wa kujirekebisha. Muda ukisonga na mtawala hajirekebishi mtawaliwa humwambia na kumkanya kuwa hapendezewi na anavyofanya. Ikitokea akaendelea na kukosea basi huwa huyu mtawala ni taabu kurekebika hivyo mtawaliwa huwa hana budi kumchukia. Wakati wa kumchukia kama mtawaliwa ana Uwezo wa kumuondoa humuondoa. Anapomuondoa sio lazima amuweke kama aliye mtoa. Anaweza akawa na Uwezo zaidi au pungufu ya huyu wa kwanza lakini kwa kiwango alichofikia huyu mtawala kumubadilisha huwa ni lazima. Huyu mtawala anapotolewa huendaa akakaa na kujivinjari kwa mini katolewa. Hapa ndipo hugundua kuwa alikuwa anamkosea mtawaliwa na hujuta kwa mini alikuwa hajirekebishi? Hujiapiza kurudia kutawala na kujisemea kimoyo moyo kuwa pindi akirudia kutawala tena atatawala kama mtawala anavyopenda. Na yule aliyewekwa hujiuliza sababu ya kutolewa mtawala wa kwanza na kuwekwa yeye. Naye hujiapiza kutofanya makosa ili asije akaja kuondolewa kama yule wa kwanza. Katika mazingira haya ya mabadiliko ya watawala mtawaliwa utengeneza ushindani ambao kwake huwa ni kutawaliwa vizuri.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.