Foleni ni kubwa na amesema anasubiriwa Lowassa atakuja kupiga kura kituoni hapo.
Yupo live muda huu.
Updates 1..
Tayari Lowassa ameshapiga kura akiambatana na mama Regina na amehojiwa na vituo mbali mbali vya habari ikiwemo mwandishi wa Al Jazeera International ambapo Lowasaa ameyajibu maswali yote kwa kiingereza safi kabisa kwa hali ya juu kabisa
Updates 2..
Lowasa akihojiwa ameulizwa yupo tayari kukubali matokeo? Amejibu kuwa kama uchaguzi utakuwa huru na wa haki atakubali matokeo na kama hautakuwa huru na wa haki basi hatakubali matokeo kamwe.
Updates 3..
Mama Lowassa anasema kuwa ana uhakika kabisa mume wake ataibuka mshindi. Ameyasema hayo akihojiwa live na Spencer Lameck wa ITV
Yaani hata Aljazeera wanafatilia zaidi habari za Lowassa! Yaani leo asubuhi wameonyesha kidogo Magufuli akiwa barabarani lakini wakabakia kwenye nyomi ya jangwani jana! Intrest ya internation inaonekana Lowassa
Kama inavyosisitizwa na watu mbalimbali kuchagua mgombea mcha MUNGU. Leo Lowassa kaanza kwanza kwenda kusali kanisani na sasa yuko kituoni na mkewe kwa ajili ya kupiga kura