Zaidi ya nusu ya wabunge wa ccm hawakushinda kihalali .
Kwa nguvu ya nani? Acheni kujidaganya na kutaka kumpa fisadi Lowasa uwezo ambao hana, kama alikuwa uwezo wa kufanya hayo angeshayafanya zamani sana kwanza hata kabla ya kutoka CCM!
Fisadi Lowasa ana matatizo ya akili na CCM wanamjua vizuri sana na ndiyo maana walimkata hata akina Mbowe wameshamstukia na muda siyo mrefu wataachana naye na kuwekeza nguvu zao kwenye mambo mengine, huyu Mzee ni mzigo kwanza nafikiri hata mke wake anashukuru vile anavyojishughulisha na chadema ili amuondolee mzigo nyumbani kwa maana kushinda siku nzima na jitu libishi na lisilojifunza kama hili ni lazima uchanganyikiwe!
Zaidi ya nusu ya wabunge wa ccm hawakushinda kihalali .
Mtatoa matamko sana na ukweli mnaujua kuwa mmeshindwa tu. We una wabunge 35 kati ya 265 utapataje urais! ungeunda serikali ya mseto or? mambo mangine muwe na aibu kidogo mtu mzima akivuliwa nguo huchuchumaa, heri mjadili hali ya kisiasa ya Zanzibar kuliko kudanganya nyumbu wenu na kuwapa matumaini hewa.
Utakuja kuambiwa kikao kimehairishwa, si unamjua babu wetu bwana!!
Leo atasema maneno mazito sana,kwa dakika tano,,mh,kumbe bora hata slaa alikua anatetemesha,lowasa ni hopeless case
Elimu inahitajika sana tena sana maana kuna watu wanajua siasa ni sawa na club za yanga na simba.
Julius aliwamba siasa ni kilimo siasa ni maendeleo lakini watu kama wewe ni shida kwa maendeleo ya Taifa.
CCM walikuwa wanakusanya matokeo pale nyuma ya Shorpers Plaza na Mlimani City haujaona??
Kuhusu wabunge halina hata shaka kwamba mumepora majimbo mengi pamoja na hayo mbona Msigwa alichukua Iringa akiwa na Madiwa watatu tu hilo ulioni?
Mkutano saa ngapi mbona mpaka sasa kimya.
Mbona umeisha saa nyingi!!!! Msg toka Mwananchi imesema anaungana na CUF kudai haki yao Zenji
Asante kwa taarifa,
hizo ndizo habari nzito?au kuna mengine mkuu.
Ngoja tusubiri taarifa kamili.