simaye
JF-Expert Member
- Nov 5, 2010
- 426
- 214
UKAWA wanafukuza upepo na kujitoa ufahamu
Nakumbuka zilipokua zinakaribia siku za uchaguzi ndani ya CCM wapo waliojipiza kama nyie wa leo juu ya Lowassa kwamba hakatwi mtu na alipokatwa walibaki vinywa wazi na vilio tele kwa sababu mirija ya ulaji ilikua imekatwa.
Na sasa mnajiapiza tena kwa kujitoa ufahamu kwenu eti hata iweje mtampa kura Lowassa hata awe mgonjwa vipi ahahahaa mpeni ila mjue atapigwa Chini tena kwa kura za wananchi safari hii baada ya 25 25th October. Mtulie kama mnanyolewa vile maana najua hamchelewi kutuletea fujo maana kwa maandamano tu hamjambo. ..
HAPA KAZI TU. .M4C. .MAGUFULI FOR CHANGE
Apigwe chini na watanzania wengi kwenye sanduku la kura na si watu wachache kujifungia kwenye kichumba na kuzuia ndoto ya mtu. Ndoto ya Lowassa ni kuwa siku moja awe Rais kwa ridhaa ya watanzania na alikuwa amejipanga hivyo.
Kujitoa ccm ambako ndoto hiyo ilitaka kuzuiwa ni ujasiri na fundisho kwa wanasiasa wachanga kuwa chama hakiwezi kuwa ndiyo msingi wa kuwa kiongozi wa watu.
CCM imezima ndoto nyingi sana za viongozi bora na badala yake wanatuletea watu ambao mwisho wa siku hawana kitu kichwana na kila wanapopewa madaraka hawawatumikii wananchi.
Lowassa ni jasiri na atabaki kuwa hivyo katika vitabu vya historia, na Mungu kama atamjalia kushinda itaandikwa historia mpya ya siasa za Tanzania na atastahili medali ya shujaa wa karne Tanzania aliyepitia magumu mengi ndani ya chama chake.
Lazima tukubali kuwa pamoja na wanachama wa ccm kutopendezwa na uamuzi wake lakini lolote linaweza kutokea ashinde au ashindwe anastahili kupongezwa na vijana kwa kuwa amekuwa mfano mzuri.
ccm si tiketi pekee ya kuwa kiongozi, vijana tafuteni uongozi kupitia vyama vingine kama CHADEMA, NCCR, CUF, ACT-Wazalendo na vingine badala ya kuwa wapiga debe wa ccm amabayo hata wakifanikiwa kushika madaraka mnasahaulika!