Konda wa bodaboda
JF-Expert Member
- Jul 18, 2014
- 7,981
- 4,174
Serukamba ambaye kwa sasa anamaliza muhula wake kama Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini anatarajia kugombea tena ubunge katika jimbo la Kigoma Kaskazini.
Chanzo : Habari Leo
Nadhani hapa ni dili ya kumpenyesha Zitto!.WAZIRI Mkuu mstaafu Edward Lowassa amesema huenda akamzuia Mbunge wa Jimbo la Kigoma, Peter Serukamba kugombea ubunge katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu ili amsaidie jukumu muhimu kwenye safari yake ya matumaini.
Akizungumza wakati wa kuomba udhamini kutoka kwa wanachama wa CCM mkoa Kigoma katika ofisi kuu ya CCM mkoa, Lowassa alisema Serukamba ni mmoja wa wanakamati katika safari hiyo ya matumaini.
Lowassa, anayewania kuteuliwa kugombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya CCM alisema katika safari hiyo kama mwanakamati Serukambaanayo majukumu muhimu ambayo anapaswa ayatekeleze zaidi ya kugombea ubunge.Ndugu zangu wananchi wa Kigoma nimekumbuka jambo moja ninaye mwana kamati ambaye ni mtoto wenu hapa Kigoma, Mbunge wenu Serukamba, yeye ni mmoja wa wajumbe katika kamati yangu alikuwa na dhamira ya kugombea tena ubunge, lakini mnaweza msimuone maana atakuwa na majukumu makubwa ya kunisaidia kwenye kamati, alisema Lowassa.
Pamoja na kutogombea ubunge kiongozi huyo alisema Serukamba anayo dhamira ya dhati katika kuwatumikia wananchi wa mkoa Kigoma na ili kutimiza lengo hilo ameomba wasali na kumuombea sana ili aweze kupitishwa na chama chake kugombea Urais, lakini pia kushinda katika uchaguzi mkuu.
Serukamba ambaye kwa sasa anamaliza muhula wake kama Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini anatarajia kugombea tena ubunge katika jimbo la Kigoma Kaskazini.
Chanzo: Habari Leo
Huyu anamuharibia tu mwenzake. Maana ye atakosa na huyo mwenzake nae atamkosesha
Connect dots...Zito kugombea Kigoma mjini,..Lowasa kujiunga ACT..deal ya 700mil...Serukamba kupewa kazi maalum
Jamaa ameanza kushtuka kwa upinzani mkubwa atakaopata Serukamba kwa michezo watatu hao wanayocheza. ZZK, Serukamba na EL. Mtakuja kuyaona haya maana anaogopa tu kusema hata ZZK ni mwanakamati na walishakaa wakakubaliana na ZZK kuhusu mchezo huo mchafu. Hapa napata wasiwasi kuamini watu wa Kigoma zaidi kwa usaliti
ccm wakimpitisha lowasa kama ndio mgombea wao, mi ntasubiri majukwaani tu kwenye kampeni.
Watamnadi vipi?watamsafisha kwa njia ipi?, maana wenyewe ndio walisema yeye mchafu (fisadi). Sasa nasubiri kuona kama atapitishwa na ccm, njia ipi itatumiwa kuwaambia wananchi (kumsafisha) kuhusu yeye.
Na akipitishwa na ccm, basi hapana shaka ccm itakuwa imefanya dharau kubwa kwa wananchi wake.
Maana wenyewe walisema hafai, baadae wanakuja kuwaambia wananchi wao kuwa anafaa na kutaka kumpa nchi aongoze, bonge la dharau hilo. Na akipitishwa na ccm, halafu wananchi wakamchagua kushika madaraka, basi patakuwa hapana shaka yoyote tukiingizwa kwenye guiness book.
Maana kitachotokea tanzania, kwa nchi zilizo makini na wanachokifanya hakiwezi kutokea kamwe.
Naona ukuu wa Mkoa unamnyemelea kama jamaa kiwa Rais