Omuchimati
JF-Expert Member
- Aug 23, 2014
- 427
- 202
MHE LOWASSA,
Salamu sana MHE,ni siku nyingi sasa sijakuandikia barua binafsi,mimi ni mtanzania mpenda amani mpenda mabadiliko ndugu Mhe,kati ya watu wanaokupenda mimi ni mmoja wapo,nilikupenda toka umaanza kuwa Waziri ndani ya Jamhuri hii ya muungano licha ya kukutwa na kashfa za hapa na pale,kuanzia ndani ya chama chako kwa kuingia mkataba usiokuiwa na manufaa wa kukodisha jengo la umoja wa vijana UVCCM,ilo likapita yakaja mengi mengine ambayo nikiyaandika yote hapa nitakuwa kama mnafiki kwa kutoonyesha upendo wangu kwako.
Lengo mahsusi la waraka huu ni kutoa ushauri wangu kwako mzee wa PEOPLES(sauti ndogooo,Ndugu EDWARD NGOYAYI LOWASSA,umekuwa hodari ulikuwa na afya nzuri,lkn sasa uzee umekuingia,unaumwa mzee wangu,umechoka,unatetemeka pasipo hata kutetemeshwa,unapiga hatua ambazo ukilinganisha na ulivyokuwa zamani saa hivi unanyata,naamini nafsi yako inachukia kwa jinsi ulivyo, kumbuka MUNGU huwa ana mipango yake siku zote tofauti na alivyo binadamu,na ndio maana maandiko huwa yanatushauri kumshirikisha Mungu katika mipango yetu,wewe ulipanga mipango yako kama mwananandamu ,uliutamani URAIS,lakini MUNGU anajua kuwa huwezi kuwa RAIS kulingana na hali yako ilivyo,RAIS wa nchi yoyote ya watu wenye akili na ufahamu lazima awe na kumbukumbu nzuri na afya nzuri,Mzee afya yako imedorora huna kumbukumbu nzuri,uliyoyasema jana leo unayakataa,mengine unawaahidi watu yalishafanyika,mara nyingine huwa nahisi labda uko ndani ya ndoto unaota haujaamka siku ukiamka utawaambia Watanzania hii ilikuwa ni ndoto leo nimeamka,Watanzania naomba mnisamehe kwa kuwashirikisha ndoto hii amabyo imewapotezea mda na wakati wenu,Kama sio dhambi Mhe Lowassa unajiterngenezea dhambi ambayo watanzania hawaitasahau watu wenye mapenzi mema na vyama vya siasa hawatasahau kwa sababu utawaacha wakiwa wamebomoka hawawezi kusimama tena,hata hivyo wameshaanza kubomoka.
Najua unasoma maandiko matakatifu,kama husomi sasa naamini ulipokuwa chuo kikuuu ulipata kusoma soma ingawa saa hivi sitaki kuamini sana kama unayosoma,sababu tangu mwaka 2000,ulianaza kuwa muumini mzuri wa pombe na nyama choma (Mbuzi choma) ambao ulikuwa ukichinja kila mwisho wa wiki ,ukila na kunywa na rafiki zako ambao wanajiita Friends of Lowassa,wakikupa matumaini kuwa ipo siku utakuwa RAIS,lengo sio kuingia katika maisha yako binafsi nataka kukufahamisha tu kuhusu maandiko matakatifu,wakati mmoja mfalme EZEKIAH alitembelewa na nabii wa mwenyezi MUNGU wakati huo akiwa mfalme wa ISRAEL,na kumueleza kuwa amebakisha miaka chache aage dunia, ulikuwa ni ujumbe wa mwenyezi MUNGU,mfalme alishtuka, kumbuka huyu ni mflame huenda angemkamata huyu nabii na kukata kichwa chake,lkn maneno yale yalimchoma akamgeukia MUNGU wake na kumkumbusha MUNGU mema yote aliyoyatenda maishani mwake kwa uchungu akilia,ndipo MUNGU alimuongezea miaka zaidi ya kuishi.
Nakusihi mzee wangu siku zako zimehesabiwa, mngeukie MUNGU,hili naliongea kutoka kwa maono niliyoyapata,najua mtabeza lakini liwekekeni kama kumbukumbu wana JF,siku litakapotokea liwe fundisho kwenu ambao mnamwaacha MUNGU na kuanza kuabudu fedha na wnasiasa,nilitamani nikutane nawe ana kwa ana lakini kulingana na majukumu yangu MZEE EDWARD LOWASSA,hii barua nimependa niweeke ndani atakaeguswa nayo yeyote ambayo yupo karibu yako akupe ushauri umrudie MUNGU wako.
MUNGU AZIDI KUKUBARIKI KATIKA MAISHA YAKO.
Ndimi mtumishi wa MUNGU Josephat.
Salamu sana MHE,ni siku nyingi sasa sijakuandikia barua binafsi,mimi ni mtanzania mpenda amani mpenda mabadiliko ndugu Mhe,kati ya watu wanaokupenda mimi ni mmoja wapo,nilikupenda toka umaanza kuwa Waziri ndani ya Jamhuri hii ya muungano licha ya kukutwa na kashfa za hapa na pale,kuanzia ndani ya chama chako kwa kuingia mkataba usiokuiwa na manufaa wa kukodisha jengo la umoja wa vijana UVCCM,ilo likapita yakaja mengi mengine ambayo nikiyaandika yote hapa nitakuwa kama mnafiki kwa kutoonyesha upendo wangu kwako.
Lengo mahsusi la waraka huu ni kutoa ushauri wangu kwako mzee wa PEOPLES(sauti ndogooo,Ndugu EDWARD NGOYAYI LOWASSA,umekuwa hodari ulikuwa na afya nzuri,lkn sasa uzee umekuingia,unaumwa mzee wangu,umechoka,unatetemeka pasipo hata kutetemeshwa,unapiga hatua ambazo ukilinganisha na ulivyokuwa zamani saa hivi unanyata,naamini nafsi yako inachukia kwa jinsi ulivyo, kumbuka MUNGU huwa ana mipango yake siku zote tofauti na alivyo binadamu,na ndio maana maandiko huwa yanatushauri kumshirikisha Mungu katika mipango yetu,wewe ulipanga mipango yako kama mwananandamu ,uliutamani URAIS,lakini MUNGU anajua kuwa huwezi kuwa RAIS kulingana na hali yako ilivyo,RAIS wa nchi yoyote ya watu wenye akili na ufahamu lazima awe na kumbukumbu nzuri na afya nzuri,Mzee afya yako imedorora huna kumbukumbu nzuri,uliyoyasema jana leo unayakataa,mengine unawaahidi watu yalishafanyika,mara nyingine huwa nahisi labda uko ndani ya ndoto unaota haujaamka siku ukiamka utawaambia Watanzania hii ilikuwa ni ndoto leo nimeamka,Watanzania naomba mnisamehe kwa kuwashirikisha ndoto hii amabyo imewapotezea mda na wakati wenu,Kama sio dhambi Mhe Lowassa unajiterngenezea dhambi ambayo watanzania hawaitasahau watu wenye mapenzi mema na vyama vya siasa hawatasahau kwa sababu utawaacha wakiwa wamebomoka hawawezi kusimama tena,hata hivyo wameshaanza kubomoka.
Najua unasoma maandiko matakatifu,kama husomi sasa naamini ulipokuwa chuo kikuuu ulipata kusoma soma ingawa saa hivi sitaki kuamini sana kama unayosoma,sababu tangu mwaka 2000,ulianaza kuwa muumini mzuri wa pombe na nyama choma (Mbuzi choma) ambao ulikuwa ukichinja kila mwisho wa wiki ,ukila na kunywa na rafiki zako ambao wanajiita Friends of Lowassa,wakikupa matumaini kuwa ipo siku utakuwa RAIS,lengo sio kuingia katika maisha yako binafsi nataka kukufahamisha tu kuhusu maandiko matakatifu,wakati mmoja mfalme EZEKIAH alitembelewa na nabii wa mwenyezi MUNGU wakati huo akiwa mfalme wa ISRAEL,na kumueleza kuwa amebakisha miaka chache aage dunia, ulikuwa ni ujumbe wa mwenyezi MUNGU,mfalme alishtuka, kumbuka huyu ni mflame huenda angemkamata huyu nabii na kukata kichwa chake,lkn maneno yale yalimchoma akamgeukia MUNGU wake na kumkumbusha MUNGU mema yote aliyoyatenda maishani mwake kwa uchungu akilia,ndipo MUNGU alimuongezea miaka zaidi ya kuishi.
Nakusihi mzee wangu siku zako zimehesabiwa, mngeukie MUNGU,hili naliongea kutoka kwa maono niliyoyapata,najua mtabeza lakini liwekekeni kama kumbukumbu wana JF,siku litakapotokea liwe fundisho kwenu ambao mnamwaacha MUNGU na kuanza kuabudu fedha na wnasiasa,nilitamani nikutane nawe ana kwa ana lakini kulingana na majukumu yangu MZEE EDWARD LOWASSA,hii barua nimependa niweeke ndani atakaeguswa nayo yeyote ambayo yupo karibu yako akupe ushauri umrudie MUNGU wako.
MUNGU AZIDI KUKUBARIKI KATIKA MAISHA YAKO.
Ndimi mtumishi wa MUNGU Josephat.