Lowassa hakudhuria Msiba wa Mwalimu Nyerere

Lowassa hakudhuria Msiba wa Mwalimu Nyerere

KALASHNIKOV

Member
Joined
Feb 11, 2015
Posts
49
Reaction score
29
Lowassa anahukumiwa na Historia ya kutokuwa na Mahusiano mazuri na Familia ya Mwalimu Nyerere. Lowassa hajawahi kufika Butiama Tangu Mwalimu afariki.

Lowassa hakuhudhuria Msiba wa Baba wa Taifa. Ni Mgombea pekee wa Urais ambaye hajui kaburi la Baba wa Taifa liko wapi.

Inasemekana alishangilia na kufanya tafrija fupi Monduli wakati Watanzania wanaomboleza Mwezi Mzima Butiama.

Huyu hakuwa na Mahusiano mazuri na Mwalimu aliyependa viongozi waadilifu. Lowassa kakwepa mara nyingi kwenda Butiama kwasababu ya kuogopa Mzimu wa Nyerere. Nafsi inamsuta kwasababu hakudhuria Mazishi ya Mwalimu, Doa na kumbukumbu hii haiwezi kufutika hata awe nani leo mpaka kesho.

Leo anagombea Urais, umepatikana msiba wa kijana wa Mwalimu, Marehemu John Nyerere inasemwa Lowassa atakwenda Butiama, Lahaula! Kwasababu gani?

Au kwakuwa Msiba umevuta hisia za wengi? Au kwasababu Msiba umetokea kipindi muhimu kuelekea uchaguzi? Kwasababu msiba utakusanya walio wengi wa Muhimu? Au kwakuwa kwasasa itakuwa rahisi kujulikana kuwa hukuhudhuria?

Mbona sijakuona Msasani Dar es Salaam?? Maana unavyopenda picha zingekuwa Magazetini.

Acha unafiki kama hufika Msiba wa Baba wa Mtoto wake unakusibu nini? Sikatalii msiba la hasha! Ni mshangao kama Lowassa amesahau kuwa Mzimu wa Nyerere bado upo na unaishi, utamzukia Butiama na kumuangusha?
Maana haujapata kumuona tangu Mwalimu amefukiwa Mwitongo.

Leo Familia itashangaa, Wazee wa Zanaki watashangaa, Wanaojua siri hii watakushangaa.

Nenda lakini Mzimu wa Mwalimu unakusuta! Ulikuwa wapi siku zote?
 
Siamini kama hii hadithi ni kweli, bora asiende tu atapatwa na Majanga.
 
  • Thanks
Reactions: DSN
Siamini kama hii hadithi ni kweli, bora asiende tu atapatwa na Majanga.

Kama hakwenda kwa wa kwake anafuata nini kwa wa Mwanae mtu...yeye hayati Baba wa Taifa na marehemu mwanae nani bora kwake ..Mtoto au Baba...yani uliojna wapi maji yakafuata moto.Na ni vyema asitie mguu na mambo ya chiefdom hayachelewi kuaibisha mtu mbele ya za watu ...mara puuuu...jasho jingi watu eeeheee nini jamani kuna mtu kaibiwa...jamani....
 
Lowasa anahukumiwa na Historia ya kutokuwa na Mahusiano mazuri na Familia ya Mwalimu Nyerere. Lowasa hajawahi kufika Butiama Tangu Mwalimu afariki.
Lowasa hakuhudhuria Msiba wa Baba wa Taifa. Ni Mgombea pekee wa Urais ambaye hajui kaburi la Baba wa Taifa liko wapi.

Inasemekana alishangilia na kufanya tafrija fupi Monduli wakati Watanzania wanaomboleza Mwezi Mzima Butiama.

Huyu hakuwa na Mahusiano mazuri na Mwalimu aliyependa viongozi waadilifu. Lowasa kakwepa mara nyingi kwenda Butiama kwasababu ya kuogopa Mzimu wa Nyerere. Nafsi inamsuta kwasababu hakudhuria Mazishi ya Mwalimu, Doa na kumbukumbu hii haiwezi kufutika hata awe nani leo mpaka kesho.

Leo anagombea Urais, umepatikana msiba wa kijana wa Mwalimu, Marehemu John Nyerere inasemwa Lowasa atakwenda Butiama, Lahaula! Kwasababu gani???
Au kwakuwa Msiba umevuta hisia za wengi? Au kwasababu Msiba umetokea kipindi muhimu kuelekea uchaguzi? Kwasababu msiba utakusanya walio wengi wa Muhimu? Au kwakuwa kwasasa itakuwa rahisi kujulikana kuwa hukuhudhuria?

Mbona sijakuona Msasani Dar es Salaam?? Maana unavyopenda picha zingekuwa Magazetini.

Acha unafiki kama hufika Msiba wa Baba wa Mtoto wake unakusibu nini? Sikatalii msiba la hasha! Ni mshangao kama Lowasa amesahau kuwa Mzimu wa Nyerere bado upo na unaishi, utamzukia Butiama na kumuangusha?
Maana haujapata kumuona tangu Mwalimu amefukiwa Mwitongo.

Leo Familia itashangaa, Wazee wa Zanaki watashangaa, Wanaojua siri hii watakushangaa.

Nenda lakini Mzimu wa Mwalimu unakusuta! Ulikuwa wapi siku zote?

unataka kila issue umuone. mualike kwenye ndoa yako na mumeo uone kama hatakuja alafu ndo uandike humu ''hakuhudhuria kwenye ndoa yangu'' TUTAKUSOMA
 
Hata kama si mshabiki wa Lowasa lakini sioni kama kuna ulazima
wa kuelewana na kila mtu, Nyerere ni binadamu wa kawaida tu
hakuwa nabii hivyo kutofautiana na kutoelewana kwake na Lowasa
sio sababu ya kumnyima Fursa ya kuwania uraisi, labda kama kuna
mambo mengine lakini si hilo.
 
Peleka jukwaa la porojo

Kama mnazania ni Porojo wamwambie aende...jua Mwalimu anatoka ukoo wa Kichifu na koo yoyote ya kichifu ina mambo yake...i hope alishaambiwa na watu wazima kwa hiyo msimpump asahau mambo watu wazima waliokwisha mwambia siku hizo yakamfanya ASIKANYAGE BUTIAMA kwa FAIDA YAKE.
 
Kuna jamaa kaniambia kuwa tangu Mwaka 1990 Lowasa hajawahi kwenda Butiama hata wakati Mwalimu yupo.

Mwalimu alipatwa Msiba wa kaka yake Kiboko Nyerere Lowasa hakuhudhuria.

Mwalimu alifiwa na Mama yake Mzazi Bibi Mogaya Nyerere watu wote walifika kuhani msiba isipokuwa Lowasa.

Nyerere ameugua mpaka anakufa Lowasa hapata kumwona wala kufika kutoa pole.

Msiba umefanyika Butiama, Nchi nzima ilizizima, Watu wengi walifika Lakini Lowasa hakufika.

Huyu mtu wenu ana walakini. Kazi ipo.
 
Haya ni ya kweli jamani au mnatania tu ! duh kazi ipo!
Ukizaliwa koo ya kichifu hayo ni yakawaida kwa wanaukoo...unaweza ukashangaa mtu anaphd kaludi kwenda kukaa kijijini basi tu yupo ....wazee wameamua akae...na siku wakisema atoke mnaweza kusema alikuwa nanyi miaka yote.Ndio maana katoto kadogo ka miaka 13 kanapewa mamlaka ya kukaa na RAIS wanapiga STORY HUKU MAELFU WAKO MITA MIA.

Tukielimishwa vizuri mambo hayo katika misingi ya kawaida tu ni UTAMADUNI wetu wa Mwafrika, na mkataa kwao ni mtumwa.
 
Hivi usipoenda kwenye msiba wa Nyerere basi huna sifa ya kuongoza?
Kwanini Nyerere tunamfanya Mungu kiasi hiki? Jamani hivi na hii nayo hoja ya kumfanya mtu asichaguliwe? Mi nadhani tusifike hatua ya kuangalia mgogoro wa mtu binafsi na mwenzake, kwani wewe mleta mada kama uliwahi kukosana baba riz ukiomba uongozi tusikuchague kisa una bifu na baba riz?

EL ahukumiwe na mchango wake duni wakati wa uongozi wake kama upo, ahukumiwe na matendo yake yasiyofaa kama kuhusika na rushwa, ahukumiwe tabia yake chafu ya kuhonga watu fedha etc.
Hili la msiba halina mashiko sana.
Ni mtazamo wangu tu.
 
Hata kama si mshabiki wa Lowasa lakini sioni kama kuna ulazima
wa kuelewana na kila mtu, Nyerere ni binadamu wa kawaida tu
hakuwa nabii hivyo kutofautiana na kutoelewana kwake na Lowasa
sio sababu ya kumnyima Fursa ya kuwania uraisi, labda kama kuna
mambo mengine lakini si hilo.
Gazeti kaka yako au dada yako wa kwanza nyumbani kwenu ana umuhimu gani kwenye maisha ya familia yemu?
 
Gazeti kaka yako au dada yako wa kwanza
nyumbani kwenu ana umuhimu gani kwenye maisha ya familia yemu?

Kwa umuhimu wowote atakaokuwa nao bado si sababu ya kumtenga mwanafamilia
mmoja eti kwa kuwa aligombana na marehemu kaka au dada, Kimsingi ubinadamu
unapitia changamoto zote hizo HAKUNA MKAMILIFU.
 
Kuna jamaa kaniambia kuwa tangu Mwaka 1990 Lowasa hajawahi kwenda Butiama hata wakati Mwalimu yupo.

Mwalimu alipatwa Msiba wa kaka yake Kiboko Nyerere Lowasa hakuhudhuria.

Mwalimu alifiwa na Mama yake Mzazi Bibi Mogaya Nyerere watu wote walifika kuhani msiba isipokuwa Lowasa.

Nyerere ameugua mpaka anakufa Lowasa hapata kumwona wala kufika kutoa pole.

Msiba umefanyika Butiama, Nchi nzima ilizizima, Watu wengi walifika Lakini Lowasa hakufika.

Huyu mtu wenu ana walakini. Kazi ipo.

Subiri watakuja na "Photoshop" muda si mrefu kukuthibitishia alikuwepo mcban...
 
Hivi usipoenda kwenye msiba wa Nyerere basi huna sifa ya kuongoza?
Kwanini Nyerere tunamfanya Mungu kiasi hiki? Jamani hivi na hii nayo hoja ya kumfanya mtu asichaguliwe? Mi nadhani tusifike hatua ya kuangalia mgogoro wa mtu binafsi na mwenzake, kwani wewe mleta mada kama uliwahi kukosana baba riz ukiomba uongozi tusikuchague kisa una bifu na baba riz?

EL ahukumiwe na mchango wake duni wakati wa uongozi wake kama upo, ahukumiwe na matendo yake yasiyofaa kama kuhusika na rushwa, ahukumiwe tabia yake chafu ya kuhonga watu fedha etc.
Hili la msiba halina mashiko sana.
Ni mtazamo wangu tu.
Waulize viongozi wenzie walikuwa wanafuata nini BUTIAMA kabla na baada ya kuwa Viongozi wa Kitaifa.Hivi mandera ana umuhimu gani mpaka kusimamisha DUNIA siku ya MSIBA wake JIULIZE [Mtoto wa Kichifu=Nyerere].Mwalimu Nyerere ndiye aliyemjenga Mandera.Siku Mwalimu anatangazwa na Rais Benjamini William mkapa kuwa amefariki TANZANIA ilizizima kama ilivyozizima msiba wa marehemu Sokoine.Sasa kama TAIFa linazizima leo hii mtu aliyepata kuwa WAZIRI MKUU asisimukwe na tukio linalo muhusu Mzee yule basi HATAREEEE.
 
Back
Top Bottom