Lowassa, Dk. Slaa, tusipotoshe ukweli

Lowassa, Dk. Slaa, tusipotoshe ukweli

ebu acheni lowasa lowasa hamna jingine?ongeeni sera ndan ya ccm walituhumiwa wengi km ni wakwel tuleteeni na wengiine kwa nn mmoja tuu mmmmmmmmmmmh jaman kuwen fair km ndo mnajiita wazalendo kweli ama uzalendo mpk uende jkt?
 
Sisi Watanzania MALOFA tunataka kuing'oa CCM kwa Gharama yoyote ile... UJINGA, UMASIKINI, MARADHI, UFISADI, UJANGILI, MIKATABA MIBOVU mwisho October 25...

Wanasiasa wanatutumia, wanaongea hivyo wakiwa wanamaanisha kwamba CCM itoke watawale wao, wale wao.

Ufisadi, ujangili, wizi wa mali za uma na mikataba inayowaneemesha wao sio agenda ya upinzani kwa sasa kwa sababu mgombea Urais ni fisadi na hataki ufisadi ujadiriwe kwenye mikutano! Nini kinakupa imani kwamba atafuta ufisadi?

Upande mwingine eti CCM itaanzisha mahakama ya ufisadi, kweli? Imshitaki nani sasa, maana chama chote full mafisadi!

Kwa kifupi siasa za mwaka huu ni za kijinga na tumeshikwa pabaya.
 
kwa kwa kwi kaondolewa kajiondoa sio yeye alieyeenda kumtafuta Lowassa kimempata kipi mnafiki mkubwa yule sasa uzandiki wake umejulikana mchana peupe tulimpenda lakini Delilla kampenda zaidi

Aliyetwist watanzania ni Dr Slaa mwenyewe kuwafundisha watu kusimama katika kweli what goes around comes around yamemfika unaiki akepwa, yeye afanye dili la kumleta Lowassa halafu baada ya vipande vya thumuni aruke kimanga nani atamthamini kajidharilisha mwenyewe kwa kuendekeza ya dunia delila kamkamata yote mema aliyofanyia nchi hii kavisafisha kwa vipande vya fedha

Usipotoshe ukweli, Slaa hakumtafuta Lowasa. Yeye alitapewa Taarifa za ujio wa Lowasa ndo akaanza kuhoji anakuja kama asset au liability? Chadema ilimpuuza, na kumdhihaki kuwa yet ni abiria wa treni, si dreva wala mmilki wa train. Kwamba mmilki wa train yupo, dreva yupo, wanahiari kumpakia abiria yeyote. Kama cdm wakweli wakanushe ada ya uanachama kiasi billion 10, walicholipwa!
 
Maskini mtanzania huyu kauli hizi za kishujaa anazitoa wapi, hivi unajua gharama yeyote manake nini? We mtoto si unaweza jikuta unapika na kupakua kwa njemba mwenzio Ili kuitoa CCM? Ebu jikazeni japo kidogo sio mnajiachia kiasi hiki.

Sisi Watanzania MALOFA tunataka kuing'oa CCM kwa Gharama yoyote ile... UJINGA, UMASIKINI, MARADHI, UFISADI, UJANGILI, MIKATABA MIBOVU mwisho October 25...
 
kwa kwa kwi kaondolewa kajiondoa sio yeye alieyeenda kumtafuta Lowassa kimempata kipi mnafiki mkubwa yule sasa uzandiki wake umejulikana mchana peupe tulimpenda lakini Delilla kampenda zaidi

Wanasiasa wanatutumia, wanaongea hivyo wakiwa wanamaanisha kwamba CCM itoke watawale wao, wale wao.

Ufisadi, ujangili, wizi wa mali za uma na mikataba inayowaneemesha wao sio agenda ya upinzani kwa sasa kwa sababu mgombea Urais ni fisadi na hataki ufisadi ujadiriwe kwenye mikutano! Nini kinakupa imani kwamba atafuta ufisadi?

Upande mwingine eti CCM itaanzisha mahakama ya ufisadi, kweli? Imshitaki nani sasa, maana chama chote full mafisadi!

Kwa kifupi siasa za mwaka huu ni za kijinga na tumeshikwa pabaya.

Kweli kabisa, binafsi nilimpenda Dr Slaa, 2010 alivyokuwa anachambua issues na jinsi ya kuzitatua. Maelezo yake yalikuwa yanajenga matumaini. Ila hawa tunaowaimbia sasa hivi yaani binafsi sioni kitu. Eti tukishafika ikulu ndo tutajua cha kufanya. Hapana tunapotoka!
 
"Ni jamii iliyochoka na kuchakaa; ni jamii iliyooza na kuchoma pua kwa harufu ya uvundo wa rushwa na kujaza nzi wakubwa wa rangi ya Kijani, Ni jamii yenye ufisadi na ukandamizaji; ni jamii isiyojua mbele wala nyuma, ni jamii iliyokosa dira". Bunge lipo kwa jina tu kwa sababu limewekwa kwapani na watawala; Madaraka ya Rais ni makubwa kwa kiwango cha kupora demokrasia: Utajiri wa nchi upo mikononi mwa kikundi kidogo cha "wateule" na watawala kilichowageuza wananchi wadunda kazi wasiofaidi jasho lao.

Na pale maandamano ya wanawake, wanaume na vijana wenye njaa yanapopita karibu na Makazi ya Wenye nacho,Malodilofa husimama ghorofani, wakawatazama na kuuliza, "kulikoni?". Na walipoambiwa kwamba yalikuwa ya "malofa" wenye njaa waliokosa mkate wa kila siku, wao walijibu: "Kama ni hivyo, kwa nini wasile nyasi na mihogo?

"Vijana wanaangamia kwa kukosa maarifa mashuleni na wanaishia kubwia "unga" ambao ni biashara pendwa ya Malodilofa,vijana wasanii wenye vipaji mbalimbali wanageuka ombaomba na wakati wa Kampeni wanakuwa "lulu" kwa kutumika kujaza "nyomi" katika mikutano,wakulima wanazeeka kwa kazi ngumu mashambani na kukosa pembejeo za kisasa na mazao yao yanaishia kukopwa kwa bei ndogo ajabu,wavuvi wanachomewa nyavu zao walizonunua kwa wafanyabiashara wajanja wenye meno,wawindaji wa vitoweo wanaambiwa ni majangili huku tembo wakiuwawa kwa tama ya meno yao na twiga wakipandishwa ndege kwenda ulaya na Asia..

Dah! wagonjwa wanakufa huku wamelala mzungu wanne sakafuni mahospitalini kwa kukosa madawa,wakina mama wanajifungulia vichochoroni kwa ubovu wa barabara, Na wanapoona malofa wanawapigia kelele kwa madai yao sahihi wanaamuru majeshi ya ndugu zao wanyonge wawapige mabomu ya machozi na kuwaua na kuwasababishia vilema vya maisha na kuwatesa waandishi wa habari zao za kilofa.Watawala wetu hivi leo wanatuhumiwa kumiliki mabilioni ya fedha wanayomiliki huku wakiyaita ni "vijisenti", au "fedha ya mboga", wakati kipato cha Watanzania walio wengi ni chini ya shilingi mia nane kwa siku.

Wananchi wanapopiga kelele kugugumia bei kubwa ya kivuko wanaambiwa "Wapige mbizi" na pale ndege ya Rais na rada chakavu inaponunuliwa kwa pesa nyingi zenye asilimia kumi za wajanja wanaambiwa "Ni heri wale nyasi"…Pamoja na mikakati mikubwa na yakutumia fedha na rasilimali nyingi za walala hoi kwa ajili ya kuvuruga "Mabadiliko" kwa kuwanunua wanasiasa uchwara na kuwakashfu kuwa ni "wapumbavu,malofa na mbumbumbu".

Wakati umefika,chama kilichokuwa na dhamana ya haya yote kipumzishwe,ili kijitafakari,kitakapokuja kwa mara nyingine (MUNGU akikijaalia) kije kikiwa kamili....Kwa wakati huu,nathubutu kusema,Naichagua UKAWA,...sio kwa sababu za uimara wa CDM,CUF,NLD,NCCR MAGEUZI ama Uimara wa UKAWA la hasha!!Ila ni kwa sababu ya udhaifu wa CCM na ahadi ilizoshindwa kuzitekeleza kwa miaka 54 mfululizo.

"ALUTA Continua, Victoria Ascerta".... "The Struggle Continues, Victory is Certain"; ...Mapambano yanaendelea, Ushindi unakuja!! ≠HapaNimakwenziTu!!
 
mkulimawakiteto

tutampeleka Ikulu ili tujue anachotafuta hasa huko Ikulu ni kitu gani,as longer as we have nothing to loss acha tumpe tu,tumevumilia 54 years why not 5 years na yeye akate kiu yake
 
Last edited by a moderator:
Inapozungumzia mtu binafsi ni sawa na kumuosha mbwa makalio. Hapo hata wewe huenei kwenye mizani ya uchambuzi usioelemea masilahi fulani.

Ila piga pesa ya watawala. Mimi lazima niwatose kwa sababu kwa miaka yote waliokaa madarakani sijauona mstakabali wa maisha yangu wala ya wajukuu wangu.

NI GIZA
 
ebu acheni lowasa lowasa hamna jingine?ongeeni sera ndan ya ccm walituhumiwa wengi km ni wakwel tuleteeni na wengiine kwa nn mmoja tuu mmmmmmmmmmmh jaman kuwen fair km ndo mnajiita wazalendo kweli ama uzalendo mpk uende jkt?
Kabla ya Singhasingha na james, atuhumiwa wakuu wa ufisadi Tanzania ni Rostam,Chenge na Lowasa. Mengi kwenye orodha yake ya mafisadi papa alimtaja rostam pia. Mengi alituambia kuwa bila kushughulikia rostam na wenzake tutafukuza makatibu wakuu na mawaziri kila Siku.
Miongoni mwa wagombea lowasa ni mtuhumiwa, alituhumiwa na Nyerere, katuhumiwa na mwinyi. Mkapa na JK wakajifanya vichwa ngumu wakampa nafasi, lowasa bila kufanya ajizi akawaliza. Isitoshe pesa ya rostam ndo inafanya kampeni za lowasa. Chenge ansjulikana ni teamlowasa. Kifupi, lowasa kaondoka na watu wake. Ndo maana neno ufisadi halisikiki tena cdm.
 
Watu wameshakuwa misukule wa CCM mpaka wanashindwa kuuona ukweli na kuusema ukweli kuwa wanaoutaka urais kwa gharama zozote ni CCM waliosema waziwazi kuwa watahakikisha CCM inashinda kwa gharama zozote hata kwa goli la mkono,CCM haohao ndio waliomwaga damu Pemba kwa kuwaua wananchi kwa mabomu ili wahakikishe wanaendelea kuwepo madarakani.

CCM haohao wanaomtumia Dr Slaa kuhujumu upinzani ndio waliotaka kumuua Dr Slaa kwa sumu kwa kumtumia mulinzi wake walipoona kuwa Dr Slaa ndiye mtu peke aliyeonekana kuhatarisha utawala wao kwa wakati ule.
 
Ndugu yangu Karugendo ....Taifa limepigwa ganzi ....Leo kuna watu wanataka hata kumpiga mawe Dr Slaa ....huu usaliti tuliomfanyia baada ya kuweka roho yake rehani kwa muda mrefu kujenga Chama na kutetea wanyonge unasikitisha sana ..... Kwa tabia hii itazaa watu waoga kutetea taifa wakijua ni rahisi Kuwa twist Watanzania .....Leo hakuna hata anayetaka kufikiri ...

Dr silaa simkubali kwa sababu za kimsingi.
1. Kama adui wake mkuu ni lowassa basi angetumia busara kuwanadi wabunge na madiwani wa cdm kwani hawakuchukua nafasi yake ya urais
2. Euro 1.5million alizopokea hakujitokeza hadharani kukanusha?
3. kama mwanandishi wa makala haya I can judge you straight foward kama kada wa ccm aliyetumwa, evidence ipo. Tutakuamini kuwa wewe siyo mwendawazimu ukiweza tu kuzungumzia ufisadi wa :
3.1 vichwa vya treni,
3.2 nyumba za serikali zilizouzwa na Dr. Magufuli kwa bei ya kutupa,
3.3 escrow,
3.4 epa
 
Sisi Watanzania MALOFA tunataka kuing'oa CCM kwa Gharama yoyote ile... UJINGA, UMASIKINI, MARADHI, UFISADI, UJANGILI, MIKATABA MIBOVU mwisho October 25...

Unazungumzia mafisadi wapi? Unataka kuondoa mafisadi wapi wakati unao nyumbani kwako mwenyewe? Hii inaonyesha taifa halina watu wenye kufikiri kiundani bali ni ushabiki uliokithiri. Hakuna mabadiliko kwa kutumia watu wale wale wenye tabia zile zile. Soma vyema thwread ya kalugendo itakusaidia kufikiri upya. Vinginevyo uwe kati ya wale wanaolipwa kushinda humu.
 
Sisi Watanzania MALOFA tunataka kuing'oa CCM kwa Gharama yoyote ile... UJINGA, UMASIKINI, MARADHI, UFISADI, UJANGILI, MIKATABA MIBOVU mwisho October 25...
Mtu yeyote anayepinga hoja za dr slaa atakuwa na tatizo la upeo kabisa.
 
Wewe ufisadi hauwezi kuwa mwisho wakati mtarajiwa wenu ndo fisadi nyangumi, na kukishakuwa na ufisadi UJINGA,UMASIKINI,MARADHI,UJANGILI, NA MIKATABA MIBOVU lazima viongezeke kwa kasi ya ajabu kisemo chake.

Kama mnajua hilo, kwa nini hamkumpeleka mahakamani ili haki itendeke? Kulala mika hapa mitandaoni na kwa wananchi ndiyo kuondoa ufisadi?

Mnasemaje juu ya ufisadi wa magufuli na mafisadi lukuki yaliyobaki ccm?

Masharti ya Slaa ilikuwa lowasa ajitakase. Ameshasema mwenye mradi wa richmond ni Kikwete, angesema kwa lugha ipi ili mmuelewe? Mbona hamwendelei hapo alipoishia kumhoji kikwete?

Huwezi kuunganisha dots kwamba kwa ufisadi wa kikwete ndiyo maana hana moral authority ya kumfikisha lowasa mahakamani?


Acheni ujinga. Dr. Slaa tumeshaambiwa hakuondoka kwa ajili ya Lowasa bali kwa karipio la mke wake na mashahidi wamesema kwamba Slaa na mchumba wake wote pamoja kwa nyakati tofauti wamekiri kuwa mgogoro wa slaa kujiondoa CHADEMA ni shinikizo la mke wake kutaka awe first lady.

Hajakanusha wala uwezo huo hana.

Wewe ni nani unayetaka tukubalie maruweruwe yako yasiyokuwa hata na chembe ya mchaganuo?

Hizo fisadi zilizojaa hadi darini mwa serikali kiasi serikali inapumlia juu juu, zimeletwa na Lowasa?

Kwa nini utulazimishe tuendeee kuwa chini ya mafirauni waiozalsha na kukomaza ufisadi na bila haya mnamlazimisha Lowasa ajitetee hata baada ya kujitetea hamjui nini cha kufanya. Kwa nini msiyalazimishe hayo mafirauni yenu yanayowadanganya na kuunda maakama ya ufisadi YATOE MAELEZO TOSHELEVU JUU YA MAFISADI LUNDO YALIYOKO CCM YENYE MEREMETA, EPA, RADA, NDEGE YA RAISI, KAGODA, ESCROW, REA, UJENZI WA BOMBA LA GAS, UJENZI WA MABARABARA YA MAGUFULI N.K?

Huoni kwa ccm kukataa kuongelea ufirauni hii, na kufanay cheap politics za kuzomea ukawa ni mafisadi wakati wakijua ccm imejaa ufisadi kuwa ni hila na kukosa dhamira ya kweli ya kupambana na hali hii?

Tafadhali fungeni virago mtuachie nchi yetu. Kwanza msiendelee kutuchafulia hali ya hewa hapa kwa kuleta mada za kipumbavu.
 
Hoja siku hizi imekuwa kwanini amkumpeleka mahakamani hawa majamaa ata kesho wanaweza kuibuka na kutuambia Rostam Aziz amekuwa anasingiziwa tu kwa muda mrefu, wakati ni wao wenyewe ndio waliotumia nguvu nyingi kutuaminisha huyo mtu afai kama walivyofanya kwa Lowassa wanaemtetea leo.

It begs ze kwesheni kama kweli ni waumini wa kile wanachosema kama wanaweza jikana wao wenyewe pia hadharani. Maswali ni mengi kuliko majibu kwa wale wanaoamini uongozi wa CDM chini ya Mbowe niwakutukuka.
 
Karugendo ana hoja... MTAZAMO ana hoja....mwanakijiji ana hoja.......wafuasi wa Lowasa wana viroja...hawajibu hoja......hatuwezi kuwa nao pamoja.

Wewe kaendelee kumnadi zzk huko mwandiga,habari za kitaifa tuwachie sisi
 
Last edited by a moderator:
Aliyetwist watanzania ni Dr Slaa mwenyewe kuwafundisha watu kusimama katika kweli what goes around comes around yamemfika unaiki akepwa, yeye afanye dili la kumleta Lowassa halafu baada ya vipande vya thumuni aruke kimanga nani atamthamini kajidharilisha mwenyewe kwa kuendekeza ya dunia delila kamkamata yote mema aliyofanyia nchi hii kavisafisha kwa vipande vya fedha

Slaa jamani yu taabani
 
Kwa hiyo unatushauri vipi tuwape CCM tena? Na hapo ndio kwenye,tatizo kwa wapiga kura wengi. Yote uliyo tasema kweli lakini CCM miaka 5 mingine haoana. Na hata huyo Magufuli si mwadirifu pia. Kama angekuwa, angesha tika kama Dr Slaa alivyofanya.

Sisiem no no no no kabisa
 
Kwa hiyo unatushauri vipi tuwape CCM tena? Na hapo ndio kwenye,tatizo kwa wapiga kura wengi. Yote uliyo tasema kweli lakini CCM miaka 5 mingine haoana. Na hata huyo Magufuli si mwadirifu pia. Kama angekuwa, angesha tika kama Dr Slaa alivyofanya.

Lowasa ndiye chaguo la watanzania
 
Back
Top Bottom