1. Huyu fisadi papa akienda ikulu nyerere anafufuka
2. Akienda ikulu huyu popobawa babomu mengine yatalipuka
3. Akigombea na watanzania wakaamuunga mkono basi watanzania ni mijusi si watu
4. Akithubutu kuchukua fomu na wakati anafahamu kuwa watanzania wanamfahamu kama fisadi= basi kwenye kundi la mamba na kenge wapo
5. Kadiri anavyotuzugazuga bila sisi kufahamu ifike mahali wote tuchapwe viboko 70 kila mmoja wetu
6. Kweli si si em haina watu ina maboga!
1. Kwa definition ya fisadi nchini, kiongozi gani siyo fisad? Wanapishana udagaa, upapa na unyangumi. Nyerere ndiyo alim-groom Lowassa kwenye siasa, tafuta confidants wa Nyerere wakuambie, na aliamini kwenye uwezo wake.
2. Mabomu yamelipuka Mbagala akiwa hata siyo Waziri Mkuu na sasa yamelipuka tena, tuache utani huo.
3. Mijusi watu kwasababu wanamuamini? wewe ambaye siyo mjusi mtu unayo haki ya kumpigia wa kwako unayemtaka.
4. Namuombea Mungu afya njema na athubutu kuchukua fomu 2015 na mimi naamini wewe utakuwa wa kwanza kumsaidia.
5.Tuchapwe kwa kutaka maendeleo??
6. CCM ni madhubuti kabisa.
Tumpeni mtu haki yake, na yeye anayo haki ya kikatiba kama wewe, na ameifanyia mengi nchi hii ya kimaendeleo kuliko hata wewe na mimi, labda... Mambo ya Urais ni mipango ya mungu - nani alijua Mkapa angekuwa Rais 2005?? Hata 2015, Rais aaweza kuwa Zitto Kabwe, lakini kila mtu anayo haki yake kama Mtanzania.