Lowassa asisubiriwe anogewe na midundo, arejeshwe alipotoka!

Lowassa asisubiriwe anogewe na midundo, arejeshwe alipotoka!

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,138
Siku kadhaa zilizopita, niliandika humu JF hivi:Rais wetu tumeshamjua, twende na midundo yake!. Waliokurupuka katika kuelewa walivyotaka wakaniponda sana. Lakini, niliyaona yaliyokuwa yakitaka kutokea na yameshatokea.Leo sishauri, ila naomba. Nilishashauri:Ushauri wa mwisho kwa CHADEMA: Mfukuzeni Lowassa, Sumaye na wafuasi wao. Itumieni nafasi ya kurudi kwenye mstari wenu!

Kimsingi, Mhe. Edward Ngoyai Lowassa, Waziri Mkuu wa zamani wa Tanzania ameamua kujitokeza hadharani na kucheza midundo ya Rais Dr. John Pombe Magufuli. He appreciated and congratulated the national and fruitful deeds of our President. In fact, our President likes to be appreciated. He was sincerely moved.

Katika kumsaidia Lowassa kusema na kutenda kwa uhuru na amani, CHADEMA 'imrejeshe' CCM ili akaungane na 'wenzake' wanaoyaona mema ya Rais Magufuli.Apewe uhuru wake haraka iwezekanavyo kwakuwa alipo si mahala sahihi. Aende akashauri, akasifu na kutoa suluhisho kwa mambo mbalimbali. Asisubiriwe anogewe na midundo akiwa CHADEMA!
 
Hyo ndio kiki yakurudia ccm bado kingunge na sumaye wakirudi 2020 hakuna kupiga kampen tena
 
Unashaurije na pesa alizowamwagia 2015 hadi labda juzi.. au akiamua kuwaumbua kakaa unataka iweje?
Unajua CDM ipo ndani ya futi sita.. kweli unaona itatoka.

Ila jana ukimya wako.. aisee ulikuwaje na mshituko.. eeeeh

Itabidi wakipe cheo sasa na hivi jina lako wanalifahamu.

Anaongea na mapaparazi saa ngapi leo?
 
Unashaurije na pesa alizowamwagia 2015 hadi labda juzi.. au akiamua kuwaumbua kakaa unataka iweje?
Unajua CDM ipo ndani ya futi sita.. kweli unaona itatoka.

Ila jana ukimya wako.. aisee ulikuwaje na mshituko.. eeeeh

Itabidi wakipe cheo sasa na hivi jina lako wanalifahamu.

Anaongea na mapaparazi saa ngapi leo?
Nani anipe cheo Mkuu? CCM au CHADEMA?
 
Lowassa ni dosari kubwa ndani ya Chadema anapaswa kurudi ccm kwani ndio sehemu inayomfaa. Kitendo alichokifanya ni fursa nzuri kwa chadema kumtimua.

Chadema hawatapata sababu nyingine ya kumtimua bali wanapaswa kutumia mwanya huu. Atarudi hukohuko alikotoka na uzuri wa ccm wataanza kumsafisha
 
Lowassa ni dosari kubwa ndani ya Chadema anapaswa kurudi ccm kwani ndio sehemu inayomfaa. Kitendo alichokifanya ni fursa nzuri kwa chadema kumtimua.

Chadema hawatapata sababu nyingine ya kumtimua bali wanapaswa kutumia mwanya huu. Atarudi hukohuko alikotoka na uzuri wa ccm wataanza kumsafisha
Alisha safishwa na CHAGDEMA
 
Mzee aliutaka Urais sasa nafikiri ameona ndoto yake imeshazima kabisa - kwa sasa ameona muda wa kupumzika umeshafika; jua linachea - na kupumzika kwa amani ameona ni kheri arejee alikokulia.

Huwezi kukulia Masaki kisha eti uzeeke Tandare!! maisha ya Tandale tunayajua sisi wana -Tandare.

So the move was purely for Presidential status nothing else!!
 
Waliokuwa wanadeki barabara waje watoe ufafanuzi, na kama akihama je, watahama nae?
Kila MTU ubeba msalaba wake kwa kuangalia maslai yake kwa wakati husika yawe ya binafsi au ya kiumoja
 
Lowassa pekee hatoshi, Mbowe inabidi ajitathmini yeye kama mwenyekiti na katibu wake Mashinji. Haiwezekani eti chama kikuu cha upinzani kinapoteza wabunge na madiwani eti kwa kununuliwa na CCM, inamaana hata tukiwapa nchi mawaziri wao wanaweza kununuliwa. Inamaana wao hawana namna ya kupambana na hizo rushwa za CCM ?

Mnasusia uchaguzi, halafu baada ya hapo nini kinafuata ?
Toka jamaa alisema hajaribiwi mmeufyata kabisa, kutoa matamko na kurudi pangoni hakuonyeshi ukubwa wa tatizo mnalotaka kutuaminisha lipo kutoka utawala huu.
Kama uhuru na demokrasia ni muhimu ni lazima ipiganiwe, nyie ndio viongozi sasa tupeni hamasa ya kupigania huo Uhuru.

Kupambana na CCM ya sasa kunahitaji mtu mwenye uthubutu, labda Mbowe aliweza kupambana na awamu ya Maisha Bora Kwa Kila Mtanzania, ila hii ya kazi tu ni mchezo mwingine kabisa !
 
Back
Top Bottom