Tulimumu
JF-Expert Member
- Mar 11, 2013
- 14,395
- 13,266
Wakati huu mchakato wa wanachama wa CCM waliochukua fomu kuwania kuteuliwa kukiwakilisha chama katika kinyang'anyiro cha urais kwenye uchaguzi mkuu mwaka huu 2015 wakizunguka mikoa mbali mbali kutafuta wadhamini, waziri mkuu aliyejiuzulu ambaye naye anawania kuteuliwa anaonekana kupewa upendeleo wa wazi kwenye vyombo vya habari kama televisheni, redio na magazeti.
Mimi binafsi sijaelewa kama upendeleo huu ni kutokana na mhusika mwenyewe kuwagharimia waandishi wa habari au ni vyombo vyenyewe ndio vinaonesha upendeleo huo au kuna asali imepitishwa ili jamaa apewe promo kubwa. Ukweli ukifuatilia taarifa za mizunguko ya watia nia wakitafuta wadhamini, Lowassa anapambwa sana na vyombo vya habari hasa TV kuliko wenzake.
Yaani wengine hata hawasikiki utadhani wamechukua fomu na kwenda nazo nyumbani. Mimi nashauri vyombo vya habari kutupa habari kwa haki na usawa kwa watia nia wote hasa kama taarifa zao zinagharimiwa na vyombo husika.
Lakini Kama ni watia nia wenyewe ndio wanaogharimia waandishi hapo sina neno kwani jamaa yule mpunga kwake sio tatizo na kila mwandishi angependa kuambatana naye maana wahenga walisema "Fuata asali ule nyuki"
Mimi binafsi sijaelewa kama upendeleo huu ni kutokana na mhusika mwenyewe kuwagharimia waandishi wa habari au ni vyombo vyenyewe ndio vinaonesha upendeleo huo au kuna asali imepitishwa ili jamaa apewe promo kubwa. Ukweli ukifuatilia taarifa za mizunguko ya watia nia wakitafuta wadhamini, Lowassa anapambwa sana na vyombo vya habari hasa TV kuliko wenzake.
Yaani wengine hata hawasikiki utadhani wamechukua fomu na kwenda nazo nyumbani. Mimi nashauri vyombo vya habari kutupa habari kwa haki na usawa kwa watia nia wote hasa kama taarifa zao zinagharimiwa na vyombo husika.
Lakini Kama ni watia nia wenyewe ndio wanaogharimia waandishi hapo sina neno kwani jamaa yule mpunga kwake sio tatizo na kila mwandishi angependa kuambatana naye maana wahenga walisema "Fuata asali ule nyuki"