Lowassa ana nini cha zaidi?

Lowassa ana nini cha zaidi?

mchambuzixx

JF-Expert Member
Joined
Nov 11, 2011
Posts
1,292
Reaction score
946
hivi huyu mtu ana kipi hasa...naona kuna nguvu kubwa sana inatumika dhidi yake ..tumeambiwa ni fisadi lakini fisadi huyo huyo anapendwa na wananchi ....nguvu ya kununua viongozi wa upinzani nayo haiko nyuma....lakini kila linalofanyika kwake ni kama linampaisha badala ya kumshusha..ninachokiona ccm ishachokwa hata kifanyike kitu gani huyu mtu hazuiliki
 
hivi huyu mtu ana kipi hasa...naona kuna nguvu kubwa sana inatumika dhidi yake ..tumeambiwa ni fisadi lakini fisadi huyo huyo anapendwa na wananchi ....nguvu ya kununua viongozi wa upinzani nayo haiko nyuma....lakini kila linalofanyika kwake ni kama linampaisha badala ya kumshusha..ninachokiona ccm ishachokwa hata kifanyike kitu gani huyu mtu hazuiliki
Kitu pekee cha ziada alichonacho ni Kuwa anayajua majizi yote huko ccm na ana uwezo wa kuwasweka ndani.
 
Lowasa anayomengi tu mfano ufisadi,rushwa,mpiga dili na muigizaji wa siasa.
umesahau kitu kimoja.Lowasa ana Nguvu kuliko serikali yoyote iliyowahi kuundwa na ccm
 
Lowassa ni level nyingine; tofauti kabisa na wanasiasa wengi hapa nchini. Huwezi kumsikia akijibu hoja za kipuuzi au kushiriki siasa za maji taka.
 
hivi huyu mtu ana kipi hasa...naona kuna nguvu kubwa sana inatumika dhidi yake ..tumeambiwa ni fisadi lakini fisadi huyo huyo anapendwa na wananchi ....nguvu ya kununua viongozi wa upinzani nayo haiko nyuma....lakini kila linalofanyika kwake ni kama linampaisha badala ya kumshusha..ninachokiona ccm ishachokwa hata kifanyike kitu gani huyu mtu hazuiliki

Unaweza kuwadanganya watu "WOTE" kwa muda unaotaka..... lakini huwezi kuwadanganya watu "WOTE" kwa muda WOTE amini Mkuu.
 
dada yake kasema hii nguvu mnaona ako nayo haijaanzia Jangwani juzi alivofunga Morogoro Road isipitike, alikuwa nayo tangu kuzaliwa; the guys ako na Nyota ya Kifalme yaani lazima umpende tu hata uwe na chuki vipi.
 
dada yake kasema hii nguvu mnaona ako nayo haijaanzia Jangwani juzi alivofunga Morogoro Road isipitike, alikuwa nayo tangu kuzaliwa; the guys ako na Nyota ya Kifalme yaani lazima umpende tu hata uwe na chuki vipi.
Pamoja na misifa yote hii uliyommiminia, imagine sasa angekuwa na charisma japo kidogo kama Obama. Haki ya nani uchaguzi ungefutwa tu akatangazwa moja kwa moja kuwa prezida. Sasa hivi yupo yupo tu kama zombie lakini bado anapendwa.

He is a good strategist na kila kitu alichofanya for the past 30 years ni kujiandaa na kujitandaza kuwa rais wa nchi hii. Sijui mpaka sasa ameshatumia pesa kiasi gani katika hii project yake. This is his last chance. Ngoja tuone!
 
Back
Top Bottom