Wakudadavuwa
JF-Expert Member
- Feb 17, 2016
- 17,505
- 16,006
Nyota njema huonekana asubuhi, ndivyo unavyoweza kusema katika kipindi cha mwaka mmoja tangu kupigwa chini na watanzania,Aliyekuwa Mgombea uraisi wa Chadema ndg.Lowassa anaitia katika wakati mgumu. Ni kama gundu la ufunguzi wa mwaka 2016 pale rafiki yake mkubwa Gwajima alipotangazia waumini wake na Dunia kuwa hakuwahi kumuunga mkono Lowassa. Kisaikolojia tulijua kitumbua kimeingia mchanga.
Muda haukupita wapiga domo wake wakuu tokea CCM, wakiongozwa na Mwapachu,Msindai na makundi mengine mamilioni yakimtosa kimya kimya yakimuacha bila kumuaga.
Makada Chadema nao wamemtosa bila kumtaarifu, hawamtembelei wala kumzungumzia kama ilivyokuwa baada ya uchaguzi. Hawataki kuhusishwa naye kwa Lolote, wamemwachia Mbowe 'zigo' la msumari.
kitu pekee kinachomliwaza ni wanahabari, angalau kwa vijisenti wanalazimika kumuandika. Vijana wa chadema Mtandaoni, wakiongozwa na Kijana Yericko Nyerere aliyewahi kujitambulisha kama Mwenyekiti wa chadema mitandaoni wamefunga midomo na vidole vyao haviandiki hekaya zozote za kumsifu kamanda Lowassa.
Ni dhahiri, pamoja na mafuriko Lowassa amechuja mapema sana kwenye vinywa vya makamanda ukilinganisha na Dr.Slaa ambaye alidumu kwenye vinywa vya makamanda miaka takribani mitano hadi pale Mbowe aliporubuniwa.
Ukweli mwingine ni kuwa atabaki hapo chadema kwani ana hati miliki lakini wale makamanda halisi wanashirikiana naye kwa kujificha ficha, hawataki jamii iwahusishe naye. Ukiacha Mbowe na Mashinji ni ngumu kukuta vijana wengine wakiwa karibu naye ili kulinda kumbukumbu zao siku za mbeleni.
Nawasilisha.
Muda haukupita wapiga domo wake wakuu tokea CCM, wakiongozwa na Mwapachu,Msindai na makundi mengine mamilioni yakimtosa kimya kimya yakimuacha bila kumuaga.
Makada Chadema nao wamemtosa bila kumtaarifu, hawamtembelei wala kumzungumzia kama ilivyokuwa baada ya uchaguzi. Hawataki kuhusishwa naye kwa Lolote, wamemwachia Mbowe 'zigo' la msumari.
kitu pekee kinachomliwaza ni wanahabari, angalau kwa vijisenti wanalazimika kumuandika. Vijana wa chadema Mtandaoni, wakiongozwa na Kijana Yericko Nyerere aliyewahi kujitambulisha kama Mwenyekiti wa chadema mitandaoni wamefunga midomo na vidole vyao haviandiki hekaya zozote za kumsifu kamanda Lowassa.
Ni dhahiri, pamoja na mafuriko Lowassa amechuja mapema sana kwenye vinywa vya makamanda ukilinganisha na Dr.Slaa ambaye alidumu kwenye vinywa vya makamanda miaka takribani mitano hadi pale Mbowe aliporubuniwa.
Ukweli mwingine ni kuwa atabaki hapo chadema kwani ana hati miliki lakini wale makamanda halisi wanashirikiana naye kwa kujificha ficha, hawataki jamii iwahusishe naye. Ukiacha Mbowe na Mashinji ni ngumu kukuta vijana wengine wakiwa karibu naye ili kulinda kumbukumbu zao siku za mbeleni.
Nawasilisha.