Sauti ya Rondo
Senior Member
- Aug 1, 2009
- 127
- 226
Aliyekuwa waziri mkuu wa kwanza wa serikali ya awamu ya nne Edward Ngoyai Lowassa aendeleza vita ya kisiasa dhidi ya anaowaona mahasimu wake kisiasa kuelekea 2015.Akejeli safari ya rais wa Tanzania Mh.Kikwete ughaibuni kutibiwa akidai amekimbia sakata la Escrow na sio kama kweli anaumwa.Lowassa alienda mbali zaidi kwa kuwaeleza wapambe wake kwamba yeye akiwa rais hawezi kukimbia matatizo bali angeyakabili.Ajabu ni kwamba Lowassa naye anayaongea hayo akiwa nchini India kimatibabu katika hospitali ya Apollo na sio bungeni kama wafanyavyo wengine.
Pia Lowassa kuonesha anaumizwa na namna Pm Pinda anavyokabili mashambulizi yake na ya watu wake ameanzisha propaganda katika mitandao na magazeti ya nchini Tanzania na nje ya nchi akishirikiana na Rostam Aziz kushinikiza Pinda ajiuzulu kama alivyofanya yeye 2008.Lowassa anamshawishi Pinda ajiuzulu ili 2015 wafe wote wakiondolewa kugombea urais kwa tiketi ya Ccm.Ujio wa Pinda umezidi kumuumiza kisiasa.
Lakini bado Lowassa ana uadui mkubwa na waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Mh.Bernard Kamillius Membe!Hii inajidhirisha katika yale anayoandika au kuandikiwa na vijana wake iwe ni kwa kubuni au kuwatuma katika mitandao kuandika kuwa Membe alishiriki kuiangusha serikali 2008.
Lowassa hajui propaganda.Kila anachomfitini Membe kinakosa nguvu na kumjenga Membe.
Pia Lowassa kuonesha anaumizwa na namna Pm Pinda anavyokabili mashambulizi yake na ya watu wake ameanzisha propaganda katika mitandao na magazeti ya nchini Tanzania na nje ya nchi akishirikiana na Rostam Aziz kushinikiza Pinda ajiuzulu kama alivyofanya yeye 2008.Lowassa anamshawishi Pinda ajiuzulu ili 2015 wafe wote wakiondolewa kugombea urais kwa tiketi ya Ccm.Ujio wa Pinda umezidi kumuumiza kisiasa.
Lakini bado Lowassa ana uadui mkubwa na waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Mh.Bernard Kamillius Membe!Hii inajidhirisha katika yale anayoandika au kuandikiwa na vijana wake iwe ni kwa kubuni au kuwatuma katika mitandao kuandika kuwa Membe alishiriki kuiangusha serikali 2008.
Lowassa hajui propaganda.Kila anachomfitini Membe kinakosa nguvu na kumjenga Membe.