Miezi miwili na ushee iliyopita mgombea huyu aliulizwa na wahariri wa magazeti iwapo atahama CCM kama haitamchagua kugombea urais mwaka huu. Jibu lake lilikuwa kwamba hatahama CCM kamwe kwa sababu ilimlea, na kwamba huyo ambaye hamtaki ndani ya CCM ndiye ahame chama hicho!
Hata hivyo, kabla mwezi haujakatika mgombea huyu akakihama chama hicho na kujiunga na chama cha Upinzani, na chama hicho kikamteua kugombea urais, na sasa kuna -vijana wanamshabikia! Kimsingi aliongopa katika jibu lake lile na taswira aliyojijengea ni ya mtu asiyeaminika katika kile anachosema.
Ingekuwa ni Wazungu au sisi watu wenye kufikiri sawasawa, tusingemshabikia -katika mbio zake za urais kwa sababu ni mtu mwongo, kigeugeu na asiyeaminika, mtu asiyeweza kusimamia maneno yake mwenyewe.
Lakini kwa uwezo wetu mdogo wa kufikiri, baadhi yetu- tunamzawadia mgombea huyo kwa kumuunga mkono kwenye kampeni yake ya kuusaka urais kwa udi na uvumba!
Uongo na ukigeugeu kama huo pengine ungevumilika kama nafasi yenyewe anayowania si urais. Lakini urais ni kazi yenye heshima, utukufu, uadilifu nk. Ni kazi ambayo haimfai mtu mwongo na asiyesimamia maneno yake mwenyewe.
Vijana wetu hawajiulizi, kama huyu alidiriki kutudanganya jana, kwa nini asiendelee kutudanganya hata leo au hata baada ya kuingia Ikulu.
Tutamwamini vipi katika hayo anayodai kuwa atatutendea akiingia Ikulu kama huko nyuma aliwahi kutudanganya kwa kushindwa kusimamia maneno yake mwenyewe? TAFAKARI:
Lumumba mnakazi kwelikweli au ndo kitengo cha IT masaki?Hafai kabisa huyo mzee, urais sio mchezo wa maigizo.
Lumumba mnakazi kwelikweli au ndo kitengo cha IT masaki?
Siku ambapo lowasa atajiunga na chadema, nitajiunga rasmi ccm! Siwez kuwa chama kimoja na fisadi papa kamwe!
Hivi rais alisemaje kuhusu kura ya katiba mpya?
Lowassa akiamia Chadema mi naamia ccm siwez kaa na mwivi
CHADEMA hakina hadhi ya kuungwa mkono na watu makini kama Mh.Lowassa.
Unadhani LOWASSA ni mtu wa ovyo kama BABU?
Huyu hawezi kujiunga na genge la wahuni milele.
Tulia dawa iwazame sawa sawa! Lowassa ni mtu makini, na CHADEMA ni CHAMA makini, hukuisikia ile kauli ya "over my dead body?" MACCM mwaka huu hamna chenu, Lowassa ndiye Rais anayefuata!Haya maneno uliyatoa wewe au mwingine?
Tulia dawa iwazame sawa sawa! Lowassa ni mtu makini, na CHADEMA ni CHAMA makini, hukuisikia ile kauli ya "over my dead body?" MACCM mwaka huu hamna chenu, Lowassa ndiye Rais anayefuata!
Tulia dawa iwazame sawa sawa! Lowassa ni mtu makini, na CHADEMA ni CHAMA makini, hukuisikia ile kauli ya "over my dead body?" MACCM mwaka huu hamna chenu, Lowassa ndiye Rais anayefuata!
quote name="MUSSA ALLAN" post=10103442] "Unadhani LOWASSA ni mtu wa ovyo kama BABU?
Huyu hawezi kujiunga na genge la wahuni milele".
NA BADO. Leo unasema hili kesho hili, yangu macho.