“Yapo mambo mazuri anayofanya Rais Magufuli, aungwe mkono. Na kwa kiasi kikubwa anafanya mazuri, lakini haya hayajatoka mbinguni, bali ni wajibu wake,” alisema Lowassa.
“Isionekane kama ni salamu kutoka mbinguni, ni wajibu wake kama Rais. Kazi ya Serikali ni kutoa huduma, ni kujenga shule, ni kujenga hospitali. Ndiyo kazi ya Serikali, kwa hiyo watu wasihesabu kuwa ni hisani.
“Wamefanya kazi yao, kwa kweli nawapongeza, lakini wasionekane wamefanya hisani. Kazi za Serikali zote duniani ni kuleta maendeleo kwa watu au kuandaa mazingira ya kuleta maendeleo.”
Lumumba wote wanatakiwa walielewe hili swala...
Na wananchi wa kawaida pia.