Mkuu, unamaanisha kwamba jamaa ni fisadi lakini anawajali wananchi kuliko kina Pinda anayejiita mtoto wa mkulima lakini hana jipya? Kama kweli fisadi Lowasa leo hii kaonekana malaika, pamoja na fedha chafu anazomwaga kwa wananchi na ambazo hazijulikana kazipataje, hiki ni kiashiria tosha kwamba kweli CCM wameishiwa viongozi....kuna ombwe kubwa sana la viongozi ndani ya CCM!!!!
Nilikuwa nahesabu kura kwa sample ya watanzania waliochangia uzi huu tu,naona jamaa amepita! Lakini bado najiuliza endapo jamaa alikuwa ameonewa kuhusu dili la kifisadi la Richmond ambalo bila shaka limeigharimu sana serikali yetu na lilisababisha kibarua cha jamaa(uwaziri mkuu) kiote nyasi.Unaposema Watanzania wengi wanamkubali, una ushahidi?? Maana hata hapa JF tukipiga kura sidhani kama tunaweza kupata hayo matokeo unayoyakadiria!! Hizo pesa za marafiki zake anazozigawa hovyo hovyo ndizo zitampeleka choonini 2015!!
ni kwamba,wewe unaweza usimpe,lakini waendesha boda boda na marafiki zake,jamaa ndugu na majirani watafanya hivyo,unaweza usiamini kitakachotokea,lakini ndio siasa ilivyo kwani vyama vyote duniani malengo yake ni kushika dola na si kupaka wanja na kikawaida huwezi kusimamisha jiwe kama unahitaji kushika dola,ni lazima umsimamishe mtu mwenye uwezo na mvuto kwa jamii,ndani ya ccm E.L anao uwezo huo,akifuatiwa na Dr. magufuli,Dr.makyembe,lakini kama tutahitaji rais mwanamke basi mama Dr.migiro anaweza kusimamishwa
Anaupenda kichizi
Kuna jamaa yangu aliwai nimbia msemo huu.."kila kiongozi umuonae madarakani anareflect akili za jamii husika "
Ukiona jamii inamuita mtu mwizi at the same time wanasema huyu ndio anafaa kutuongoza nafikiri hapo unapata picha akili za hiyo jamii zikoje.
Kashfa za ubadhirifu na matumizi mabaya ya ofisi yalipelekea EL ajiuzulu lakini leo hii anaitwa PM mstaafu ili kupunguza makali ya kashfa zake.
Sa hivi kajua akili za jamii anayotaka kuitawa ipoje anachofanya anamwaga tu hela afu anasikilizia pembeni...watu weeee raisi raisi raisi
Ni vizuri kwasababu siasa ni vita cha msigi mtu ashinde ila ni kweli kabisa watanzania tumekuwa wepesi kiasi hiki.
Kweli kweli huyu jamaa leo hii ndio anaonekana lulu..mwenye utajiri husiojulikana source mwenye kumwaga hela bila kujali atazirudisha vipi..duh
kama mwizi mbona hawampeleki mahakamani bana, huwezi mwita mtu mwizi tu from no where...na kwa sabb wameshindwa kumpeleka mahakamani hiyo inathibitisha kuwa lowasa sio mwizi..na ndio mana watu tuna imani naye..
ukiangalia kwa mapana yake kunzia serikali hadi wapinzani wote wezi tu!!!!!! kwani hujasikia huyo mbowe anakopesha chama chake hela na baadae anajilipa mamilioni zaidi? anaununua vifaa bya chama mwenyewe na chenji anawekandani..anafanya hayo kwa kushirikiana na watu wake wachache ndani ya cdm..hapo hajapewa wizara au uraisi itakuwaje?
kwa kifupi watanzania wengi hawajui tu kwamba siasa ni ajira na kwamba wanasiasa hawako kwa ajili ya wananchi bali kwa maslahi yao..mpka uelewe haya ndio utaelewa kuwa hakuna mwanasiasa msafi kizazi hiki