Lori la Magufuli limekwama, Tulisukume

Lori la Magufuli limekwama, Tulisukume

OBO5

Member
Joined
Jan 31, 2013
Posts
54
Reaction score
35
Tangu kuapishwa novemba 5 2015 suala la viwanda limekuwa ndoto za mchana. Kujifariji ikatangazwa kila vyerehani vinne ni kiwanda kidogo.

Suala la kuhamia Dodoma nalo ni kigugumizi kila kukicha.

Uwazi katika manunuzi pia ni kitendawili, wananunua ndege bila kutuambia bei yake kana kwamba ni misaada.

Uongozi bora na utawala wa sheria ni mbingu na ardhi. Wanaamru mpaka SHILAWADU waonyeshe video gani.

Upigaji wa rambirambi za Kagera na zile za Gambo.

Hayo ni machache, kwa kuwa mkulu alisema yeye ni dereva wa lori ni wazi kuwa amelipitisha njia yenye tope. Lori hili limekwama tumsaidie kulisukuma.
 
Unatamani iwe hivyo..
Unaisoma namba hadi na uongo mwingi umekujaa. Subiri wenzako mshangiliane juu ya hili.
 
Nyie endeleeni kuchoma MB zenu tu,nchi inasonga kama kawa.JF ina ulimwengu wake tofauti na uhalisia,ukiwa humu waweza dhani una wafuasi kibao,kumbe mtaani picha tofauti.Watu wanaendelea na maisha kama kawaida,hawana time.Raisi ni huyu huyu mpaka 2025, nyingine ni porojo tu.Jifunzeni kuendana na mazingira yaliyopo tu, vinginevyo hameni nchi kwa muda.
 
Back
Top Bottom