Loliondo, OBC, Dowans: The disturbing connection and secrets

Kwani hii inatofauti gani na Darfur?

Kwanini mkulu mwenyewe, Jakaya Mrisho Kikwete, asifunguliwe kesi ICC, the Hague?

Maana kukaa kwake kimya ina maana haya yanatokea kwa baraka zake ...
 


Mkuu Madabwada hii kitu imenistua sana.Hii kitu ilianza kile kipindi cha cha Mzee ruksa kama sikosei kuna mwandishi mmoja wa habari wa gazeti la mfanyakazi somebody katabalo aliandika sana story za Loliondo nadhani alikumbwa na mauti katika mazingira ya ajabu ajabu.

Ni bahati mbaya watanzania tunakubali hawa wanasiasa uchwara kuuza nchi yetu huku sisi tunabaki tunawachekea.Mjumbe wa CC na NEC Bwana A Kinana alihusika na hili dili la kumleta huyu mwarabu wakati huo alikuwa waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga taifa.Bwana Kinana baada ya kujua wananchi wengi wamemstukia akaamua kuacha kugombea ubunge jimbo la Arusha na kujikita zaidi katika siasa za ndani ya chama cha mapinduzi.
 
Nampongeza Rais kikwete na serekali yake kwa kuborotesha nchi bila ya wawekezaji nchi itabakia nyuma ondowa wamasai kama ni kuleta maendeleo ya nchi .
Sijakuelewa unamaanisha nini Sonara
Kama unamaanisha kuwa Wamasaai waondolewe ili maendeleo yapatikane kwa kuwakumbatia wawekezaji basi una problem kidogo ambayo itachukua muda sana kuiondoa kwasababu ni in-built in your mind. Lakini kama unamaanisha vinginevyo basi angalau utakuwa unajua na kuthamini utu na hakia ya mtu mwingine bwana Sonara
 
Nampongeza Rais kikwete na serekali yake kwa kuborotesha nchi bila ya wawekezaji nchi itabakia nyuma ondowa wamasai kama ni kuleta maendeleo ya nchi .

Sonara!!!!Huyu atakua mwarabu tu huyu,....
Maendeleo gani wanaleta wale waarabu pale porini,kama sikunyofoa malia asili zetu tu?
Hapa hakuna muwekezaji bali kuna mijizi tu,ikisaidiana mitz kama wewe sonara na viongozi wetu wasoshiba walicho nacho.
 
Kimsingi hili la Loliondo ni aibu kwa serikali yetu toka awamu ya pili na inaonyesha ni jinsi gani ndani ya serikali kuna watu wanamuangusha Rais Jakaya Kikwete kwa kufanya mambo ya ajabu na ya kudhalilisha maisha ya Watanzania na kufanya hata ionekane kuwa Rais ameshindwa kutumia mamlaka yake ya 'milki ya hatima aliyopewa na sheria ya ardhi No. 4, 1999
 
Hivi mtu kama sonara anajidai kumpongeza Kikwete na Serekali yake kwa lipi hapa??
1. a) Uingiaji wa mikataba kati ya OBC na Serikali za Vijiji, mikataba ambao inaonyesha serikali imesaini mikataba na vijiji kwa niaba ya OBC iliyosaini kama shahidi katika mikataba hiyo.
b) Kutekwa kwa mawasiliano ya makampuni ya simu ya Tanzania katika maeneo yaliyo karibu na kitalu cha OBC ambacho hakina mipaka inayoonekana. Mfano, ukiwa eneo hilo unapata ujumbe mfupi was simu (sms) kutoka kampuni ya ETISALAT unaokukaribisha na kusema, “karibu katika Umoja wa Nchi za Falme za Kiarabu”.
c) Kujenga kiwanja cha ndege na kuwepo kwa mawasiliano ya Anga ya moja kwa moja kutoka eneo la kitalu kwenda nchi za nje. Kiwanja hicho hutua ndege kubwa zenye uwezo wa kubeba takribani watu mia nne na magari kadhaa.
d) Kutokueleweka utaratibu wa ukusanyaji wa kodi mbalimbali kwa sababu hakuna taarifa zinazoonyesha iwapo Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) yanakusanya mapato kutokana na magari yanayoingizwa na kutumika nchini yakiwa na namba za usajili wa Nchi za Falme za Kiarabu pamoja na rasilimali zinazochukuliwa moja kwa moja kupitia uwanja huo.
e) Kampuni ya OBC inapewa hadhi ya kidiplomasia na wakati ni kampuni iliyosajiliwa kama kampuni nyingine. Mfano, kambi ya kampuni hiyo inalindwa na FFU, jeshi la polisi na chombo cha dola! Aidha kuna vikundi-kazi vya serikali katika ngazi za wilaya hadi taifa vilivyoundwa kuratibu shughuli za kitalu hicho. Viongozi wa FemAct pamoja na Mitandao ya Wafugaji walikataliwa kuingia ndani ya kambi ya kampuni husika ila, badala yake, waliondoshwa kwa kusindikizwa na FFU na baadaye kusimamishwa na kuhojiwa na FFU walioagizwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha na Wilaya ya Ngorongoro.
Na kwa maendeleo gani imeleta katika eneo hili???

Tusiwe kama kasuku kila mara tunaimba vitu ambavyo hatuwezi kuvielezea maana yake na uhalisia wake.

Ukiona huna cha kuchangia,soma kisha kaa kimyaaaaa.
Arnghaaaaaaa,..ntakung'ata bure,..
 
Majanga yote yanayotokea sasa hivi loriondo, yanatokana na uzembe wa mtu mmoja:Jakaya Mrisho Kikwete.Kikwete ameshindwa kabisa kutetea haki za raia wake, women are being raped,houses burnt this is a scorched earth policy against us Tanzania.

Jamani tuangalie uwezekana wa kumfungulia huyu 'criminal' kikwete kama walivyomfanyia Bashir.

Hatuwezi kusubiri hali hii iendelee hivi.

angalia maafa hayo hapa:

Part 1
Part 2
 
Last edited by a moderator:
I support this!! THe president of Tanzania is for the Tanzanians not for the UAE; huyu Rais hafai hata kutetea na kuwalinda watu wake! Hivi huku Africa hawa MaRais wana kiburi gani? Charisma yao ipo wapi??
 
Ahhh....%^)&&**$#@@@ atasema nini wakati walishamkatia mafweza kibao, na pia kumpa dogodogo....!

Hoteli kubwa mpya, na hata hiyo proposed airport kule sio kwa maslahi ya nchi, ni kwa maslahi yao ili waendelee kuvuna wanavyotaka........! Halafu kudhiirisha upumbavu wao, leo unasikia eti hao Ortelo wanatoa magari, silaha na washawasha kwa ajili ya kusaidia serikali kupambana na ujangili...!! KN zao.....

Kule wanakula, Grumeti na ikorongo ndiyo kabisa......!! Hope wanavijiji sasa wataamka na kuwanyima kura hawa mabazazi....
 

Kwani hamuelewi maana ya miundo mbinu ?kuwepo kwa wamasai katika sehemu hiyo tija gani inapatikana kwa Taifa?
 
I support this!! THe president of Tanzania is for the Tanzanians not for the UAE; huyu Rais hafai hata kutetea na kuwalinda watu wake! Hivi huku Africa hawa MaRais wana kiburi gani? Charisma yao ipo wapi??

wacha wewe huyu Rais amechaguliwa na wananchi tena kwa asilimia kubwa ambayo hakuna Rais hata mmoja wa Tanzania aliyefikia wingi wa kura alizozipata, na hivi sasa ndio anakamilisha zile sera ambazo alizimwaga kwa wananchi na kufikia kumchaguwa miongoni mwake ni kuborotesha uchumi wa nchi na ndio anatekeleza hivi sasa kama ni kuondowa masai na kuimarisha uchumi wa nchi why not ? ondowa masai lete wawekezaji .
 
Unajua iko hivi: Kipindi cha Mwinyi nchi ilifulia vibaya kutokana na RUKSA ambayo ilifungua milango ya uchumi. Kama mtakumbuka ndio mwanzo wa kuona magari ya kijapani na ya kifahari, nyumba nzuri, fm academia schools zilifunguliwa, ili mradi ruksa ki kweli. ILISAIDIA SANA na pengine ndio mwanzo au mimba ya UFISADI tunaoona uliozaliwa sasa.

Baada ya nchi kufulia jamaa alienda UAE kuomba msaada kwa kuwa BOT haikuwa na mkwanja wa kufanya chochote. ILIFULIA. Akapewa msaada. Na kwa kuwa katika sheria ya uhifadhi wanyama pori na ardhi inamruhusu rais kutoa sehemu ya nchi kama zawadi kwa kikundi cha watu au mtu BILA maswali kwa kipindi atakachoamua. Jamaa alitumia hii fursa kwa fadhila.

Sasa tutafanyeje? Watu wakipewa nchi wanaiendesha kama familia zao. Anyhow, wanadai its unquestionable and I suspect it should be thinkable.
 
kaka,hili halina ubishi. kama watanzania tumeanza kuona ni sawa hao jamaa kuingia nchini na kujitangaza kwamba hako kaeneo ni kwao na ss tunaona ni sahihi, basi tunahtari kubwa.hata migodini kulipojaa ufisadi wa kutosha na kiburi wanachopewa na viongozi wetu hawajafikia hatua ya kufanya settings na namna hii kaka.

Kuna mkuu wa wilaya ambaye yeye familia ikiumwa, anaenda kutibiwa na dk wa mgodi kwaa gharama za mgodi. familia ikitakakwenda dar wanaenda kupanda ndege ya barrick.juzijuzi kapewa matofari kwenye eneo lililobomolewa akajenge kwake. kisha mtu huyuhuyu apelekewe malalamiko ya watanzania dhidi ya barrick, kweli atasaidia kitu huyu? mi hapa naona kuna tatizo serious.ingawa hiyo ya kujitangaza nchi ndani ya nchi ni zaidi ya hili.
 
Hakuna ubinafsishaji hapa Tanzania bali tunagawa;na viongozi wetu ndiyo wameridhia hivyo na ndiyo maana wakatengeneza sheria inayoielekea/kukaribia suala zima la ubinafsishaji.Inamaana bado hatuna sheria halisi ya ubinafsishaji wa mali za Taifa,labda hapo baadaye tunaweza kuwa nayo.Siku zote sisi tunakuwa nyuma,hiki si ndo kichwa cha mwendawazimu au mmesahau?
 
Tanzania as a nation is depressing...,our presidents,leaders even more depressing..,
 
Watu kama sonara, wenye mawazo punguani kama hayo aliyoandika ndiyo wale enzi zetu zileee vichwa vyao vilikuwa halali.....
 


Rais Jakaya Kikwete unae muongelea kwamba anaangushwa huenda pia alishiriki kwenye kusaini mikataba ya Mfalme huyu kupewa ardhi.

Hakuna sababu ya kufikiri Tanzania tuna Rais hadi wakati huu..!!

Hii nchi kama ingekuwa na uwezo mkubwa tunge shukuru kama Rais atapinduliwa na Jeshi kushika hatamu kwa muda..!

Hizi ni aibu kubwa...Ni kashfa ngapi zipo ndani ya serikali yetu na hakuna anaye weza kuzishughulikia..!
 
Kuniradhi kama hii iliishawekwa humu, ila ni vielelezo kwa njia ya mtandao. Kwa kweli ni mambo yakusikitisha.

Part 1:

Part II:

Natumaini hii kitu itamfikia Muungwana!
 
Last edited by a moderator:

Sonara,

Umekatiwa kiasi gani ili uje hapa na kujaribu kuiyeyusha hii hoja? Inabidi uone aibu angalau kidogo kwani matamko yako yanatengeneza maswali mengi kuliko majibu. Kama wamasai wasingelinda hiyo mbuga huyo mwarabu angekuta nini miaka hii ya 2000?

Kura zilizopatikana kwa wizi na kutoa rushwa kwa kutumia pesa za EPA hazina nafasi ya kuzungumziwa hapa. Kama huna cha kuchangia kaa kimya kama mimi.

Tiba
 
It is in fact unbelievable to see these things happening in a Country like tanzania, tena Arusha, a place where the former and famous US President Bill Clinton refered as
"The Geneva of Africa" .

His Exc. Clinton was refering the fact that peace resolutions on based conflicts were re-negotiated and concluded in Arusha . I have few concerns which I have noticed from the video:
1. Goverment refusal to admit the fact that people have actually suffered during burning operation. The statements bythe Arusha Regional Commissioner Vs. Prime Minister as the MP for Ngorongoro testifies leaves yet another deep discussion as who should have actually known of this terrible operation, given the seriousness of the problem .

2. Again, I was expecting to hear a piece of responce or reaction from the owner OBC or manager for that matter, having journalists in the trip, I find no reasons why that has not taken into consideration,.... I am used to kind of a good flow such as ..... now having heard from the victims,,,,, the onwer when contacted had this to say........ or at least to find a sentence that .......the owner or manager was out of reach during the visit......

Supprisingly, I did read from the local news papers, OBC's manager throwing complains to the NGOS, and other stakeholders that the complains against them have been cooked in other words "Not True" as reported in the video above . Now, I was expecting the journalist to have interviewed this person so that the whole story becomes one in which then people will be able to judge . This is my opinion !

Generally, It is a shame to have this story as true story for Tanzanian future Image, from the Image which people in the outside world have always known ....friendly....... peaceful....

With sad remarks, I am truely moved and feel sympathetic to these poeple and urge that resettement measures be taken soon , even if it costs a country to lose investors as long as citizen's right and liberty is preserved !

I am convinced that this story is true as far as the video above .

I stand to be corrected !
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…