mcubic
JF-Expert Member
- Mar 3, 2011
- 10,310
- 6,546
Mtanange wa kukata na mundu unataraji kupigwa kwenye theatre of dream baina ya United na Liverpool, mnamo mida ya saa kumi na nusu za alaasiri. United wana nafasi kubwa ya kushinda game hiyo kwa kuwa ipo nyumbani na pia ina mshambulizi hatari (RVP) anayeoongoza kuzifumania nyavu. Tayari kibabu Fergie ameanza vita ya maneno kwa kumuambia refarii Howad Webb amchunge kwa makini Mshambulizi wa Liverpool Luis Suarez kwa tabia yake ya kushika shika kwa mikono mpira na kujiangusha. Pia Fergie amesema haelewi Liverpool wapo nafasi ya ngapi kwenye msimamo wa ligi. Maneno haya yanawaathiri kisaikolojia liverpool hivyo kuwafanya wawe na papara wakati wa mchezo, hali itakayowafanya wapate kadi na kufungwa kirahisi. Ni mtizamo tu......karibuni