figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,492
- 54,895
sasa hivi ndo rais anaingia na msafara wa magari 12.polisi ni wengi, wametanda kuanzia high way hadi baharini. Tutaenda kujuzana kadli mda unavyo kwenda. mia
=====================UPDATE=======================
=====================UPDATE=======================
anayetangaza ni Mecky Sadick. anasema daraja hili litaunganisha mji wa dar esalaam na mji mpya wa kigamboni. anasema daraja litapunguza foleni ya kivuko cha magogoni. Ukamilishaji wa mji mpya wa kigamboni unategemea ushiriki wa wakazi wa kigamboni. mradi huu una manufaa makubwa kwa wakazi wa dar. Huu ni utekelezaji wa irani ya ccm. tunakupongeza sana kwa kutekeleza ahadi za ccm. napenda kuwahakikishia wananchi walio kuwa wanatumia vivuko vya waananchi kwamba tumeshapata sehemu mbadala anasema sadick. mia
wanatambulishwa watu muhimu;
Hosamu Muhalam(sina hakika na spelling) ni balozi wa Misri, mwingine ni katibu mkuu wa kazi Erick Shitumbi. John Ndunguru, Abubakari Rajabu wa NSSF, mkurugenzi mkuu Ramadhani Dau wa NSSF ambao wanachangia garama kubwa, Patrick Mfugale TANROAD, Mhandisi Mataka wa NSSF aliye simamia Chuo kikuu Dodoma, James Wanyancha na watendaji wakuu; Boniface Mhegi, Maselina Magesa, Mwakalinga. mia
mkurugenzi wa nssf anasema;
anaanza nakushukuru;
nssf kwa kushirikiana na serikali inajenga daraja lenye uurefu m680 na barabara 6. watembea kwa miguu ni m2 kila upande hawatatozwa ushuru.
nssf itagaramia asilimia 60 na serikali 40 na kulipa gharama za fidia. ujenzi utagharimu bil 214.6 na utachukua miaka 3. eneo la mladi limekabidhiwa 1.mwezi 2. mwaka huu. hili mnalo liona ni daraja la mda la kuwasaidia wajenzi. daraja litakuwa upande wa kulia wa hili. mia