Suala la washabiki wa Simba kushangilia timu ngeni hawajaanza wao, wanachofanya sahivi ni kulipiza kisasi tu lakini suala hili kwa hivi karibuni limeanzishwa na washabiki wa Yanga waliponunua jezi za TP Mazembe na kuishangilia sana, wale wa Simba nao wakaja kulipiza kwa Zamalek baada ya hapo imekuwa ni mwendelezo.
Na washabiki wa Yanga wengi wao ndo wa ovyo kabisa maana hata timu ya Taifa ikiwa na wachezaji wengi toka Simba wao wataizomea si kwa sababu ni ya hovyo bali sababu yake ni kwamba klabu yao haijatoa wachezaji katika timu ya Taifa.