Live update: Simba SC va Azam FC

Live update: Simba SC va Azam FC

brave one

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2013
Posts
4,879
Reaction score
7,393
Baada ya pilika pilika za uchaguzi sasa tunarudi uwanjani.
Vinara wa ligi kuu Tanzania bara wekundu wa msimbazi Simba wanashuka uwanja wa taifa kupambana na Azam Fc leo jumatatu saa kumi jioni, mechi inatarajiwa kuwa kali ya kusisimua kwani kila timu inawania nafasi ya kuongoza ligi pia timu zote mbili hazijapoteza mchezo wowote msimu huu wa ligi.
Kikosi cha Simba kinachoanza leo
1. Dhaira
2. Willium lucian
3. Idrissa rajabu baba ubaya
4. Gilbert kaze
5. Joseph Owino
6. Jonas Mkude
7. Ramadhan singano
8. Said ndelma
9. Amis tambwe
10. Betram mombeki
11. Zahoro pazi
mechi itakuwa live TBC1
Mechi nyingine za leo
Coastal Union vs Mtibwa Sugar
Orjoro JKT vs Ashanti Utd
Ruvu shooting vs Kagera Sugar
UPDATE:
kikosi cha Azam FC
1. Mwadini ally
2. Erasto nyoni
3. Salum waziri
4. Said morad
5. Agrey moris
6. Kipre balou
7. Humfrey mieno
8. Sure boy
9. John bocco
10. Kipre tchetche
11. Joseph kimwaga
UPDATE
Mpira umemalizika
Azam FC wakipata ushindi wa shida wa bao 2 kwa 1, magoli ya azam yote yakifungwa na kipre Tchetche uku bao la Simba likifungwa na ramadhani Singano
FT: Simba 1 Azam 2, uwanja wa taifa
 
Mkuu naombea mpate sare ili kesho yanga wamchape mtu waongoze ligi.
 
Akitoa droo mnyama lazima ashangilie mi naona leo ni kipigo tu kwa mnyama
 
Mkuu, kiukweli sare hakuna (kitambaa kidogo) lazima mnyama anye mavi ya kila rangi.

mkuu Azam itabaki kuwa bidhaa bora ya bakhressa lakini si timu bora mbele ya mnyama, leo ni kichapo tu
 
Mnyama leo lazima akatwe mkia, mtakao bahatika kuhudhuri TAIFA msisahau kuja na mifuko (ikibidi kiroba) ya kubebea nyama, maana leo vijana wa jiji, Kiboko ya vigogo, wazee wa kuwalambisha (Azam) wanataka wamgane mnyama hadharani.
 
Nitafurahi kama matokeo yatakuwa hivi
Azam 0-0 Simba
T Prison 2-1 Mbeya city.
mechi zingine hazina madhara kwa YANGA.
 
mkuu naona umetanguliza matamanio yako kuliko hali halisi

Dk.90 zikiisha utaelewa nilicho kuwa namaanisha nyie kushinda leo ni sawa na fenesi kudondoka kwenye mnazi.
 
Dk.90 zikiisha utaelewa nilicho kuwa namaanisha nyie kushinda leo ni sawa na fenesi kudondoka kwenye mnazi.

Azam kwa Simba bado sana subiri dk 90 unbeaten run inaendelea kwa mnyama
 
Nitafurahi kama matokeo yatakuwa hivi
Azam 0-0 Simba
T Prison 2-1 Mbeya city.
mechi zingine hazina madhara kwa YANGA.
Mkuu, leo Azam haitafanya makosa muliyoyafanya Yanga. Kosa kubwa alilofanya Yanga ni uoga. Baada ya kumpakata Simba (akafikiria kapata paka) alipo geuka nakugundua kumbe ni Simba, uoga ukawaingia na kumtupa huku mukitimua mbio, ndipo mnyama akaanza kujitetea nakudhuru baadhi ya wasakaji wa Yanga. Sasa leo Azam hatutarudia makosa hayo. Tuta hakikisha tukimpakata hatumuachii.
 
Amis Tambwa ameondolewa kwenye kikosi kinachoanza na nafasi yake amechukua amri kiemba
 
Back
Top Bottom