List ya beach nzuri DSM

Kwa Mfano Ramada Mbezi beach kama umechukuwa room hakuna gharama ya ziada, ila kama unakwenda tu na kuondoka inatakiwa ulipie bufee sh 50,000/= kwa kichwa.
Starehe gharama, Ramada is the best place.
 

Ni kweli Kikulacho, last weekend nilimuona Kijana mmoja wa hayo Mapira ya kuogelea kama alikuwa analazimisha fursa, Bint alikuwa akiogopa lakini akawa kama anazidi kusogezwa mbele, sadly enough kila Bint alivyokuwa akipata shida ya maji aina ya uokozi wa jamaa ulikuwa zaidi kushika Hotel ya mtoto.

Mamlaka husika zieweka mingozo au Usajili wa hawa Beach Boys/ Swimming Trainers
1. Swimming Trainers wasajiliwe ili iwe rahisi kuwashika/kuwafuatlia pindi likitokea tatizo
2. Kabla ya kwenda ndani ya Bahari Mteja/Muogeleaji Mwanafunzi aambiwe haki zake ikiwemo kutoshikwa shikwa ovyo au kupelekwa kwenye kina kirefu.
3. Ile Mipira na nguo zinazo kodishwa kwa ajili ya kuogelea ziwe zinafanyiwa usafi (japo Beach zetu nazo ni full uozo)
4. Beach Boys/Swimming Trainers au wenye Hotel na Jiji wawajibike na usafi wa Beach zetu vinginevyo zawadi ya Bingwa wa Uchafu kutoka kwa Mheshimiwa Makonda wapewe wao.
5. Huduma za Kijamii kama vile Vyoo vya kujisaidia na vyakula(Mihogo etc) itolewe katika mazingira ya usafi.
 
sina swali nashukuru ila hujaniambia ni mida gani mizuri ya kuogelea maana nasikia bahari ina mashart yake
 
shukrani mkuu .ila mimi najua kuogelea siitaji trainer
 
sina swali nashukuru ila hujaniambia ni mida gani mizuri ya kuogelea maana nasikia bahari ina mashart yake
Muda wa beach ni wakati wa jua, kuanzia saa 8 mchana ni muda mzuri wa kuogelea hata bahari inakuwa imejaa yote.

Ila ni vizuri kama hujui kuogelea ukajifunza kwanza kwenye swimming pool badala ya kujifunzia baharini.
 
Muda wa beach ni wakati wa jua, kuanzia saa 8 mchana ni muda mzuri wa kuogelea hata bahari inakuwa imejaa yote.

Ila ni vizuri kama hujui kuogelea ukajifunza kwanza kwenye swimming pool badala ya kujifunzia baharini.
kuogelea najua sana nimeogelea sana ziwani kwani kuna tofauti?
 
bufee elf 50 si nitaishia hapo kwenye misosi? nitaogelea tena kweli?
Kwa kifupi hiyo 50,000/= ndio kiingilio chako, hakuna tena malipo ya ziada utakula mpaka uvimbiwe kwa pesa hiyohiyo.

Kama umepanga kulala hapo hapo hulazimiki kulipia hiyo 50 ni free for hotel guests.
 
sijaelewa unakula unakunywa na kulala kwa hyo 50 ?
Hata Hotel za kariakoo hakuna kitu kama hicho.

Labda ni hivi nikurahishie, hotel room si chini ya Tsh laki mbili mpaka mbili na nusu inategemea na season, na hii ni bei ya bed and breakfast.

Sasa ukishakuwa umechukuwa room facilities kama swimming pool ni free kwa guests.

Ili kuzuia vibaka na wahuni mtu ambaye anakuja na kuondoka wameweka utaratibu huo wa kulipa 50,000/= for bufee.
 
ok shukrani kwa ufafanuzi ngoja nidowload form ya sponsorship toka italy maana kibongobongo nitaishia tu kusoma hapa
 
Ina maana hao wenye hotel hawana taarifa za hao ma life guard wao kuhusu vitendo wanavyowafanyia wateja wao? mbona ni mambo ya ajabu sana? mimi nadhani hao wateja hasa mabinti inabidi inapotokea kufanyiwa vitendo kama hivyo wanapaswa kutoa taarifa kwa wenye hotel/kampuni husika kusudi hatua zichukuliwe dhidi ya muhusika wa vitendo hivyo,kwani huu si uungwana hata kidogo kama ni kweli hayo mambo yanafanyika.
 
Beach zipo nyingi unaweza kuanza na mbalamwezi pale mikocheni kwa warioba kwa mbele kiingilio 5000 huwa inabadilika,kuna bahari beach kule kunduchi getini unalipa elfu 10000 kuna hapa escape one pia kiingilio bure ukija kigamboni ndio za kumwaga kuna southbeach,barakuda beach,mikadi beach na nyinginezo to mention a few
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…