"list of shame" ya mwembe yanga.

Mpalakugenda

JF-Expert Member
Jun 2, 2015
2,043
1,287
Dr Slaa akiwa ktk ubora wake alitutajia orodha ya aibu.
1. Lowassa akiwa mmoja wa waliotajwa ametoka serikalini na amejivua gamba.
2. Jakaya naye hayupo tena madarakani,amepumzika anakula kiinua mgongo.

Hao hapo juu kuna aliye na kinga ya kutoshtakiwa kwa masuala aliyoyafanya akiwa rais..sijui kwa yale kabla ya kuwa rais. Mwingine tunasubiri mahakama ya mafisadi ianze maana ndipo pekee ushahidi utapatikana.

Je,waliobaki wapo wapi na wanafanya nini kwa sasa? Rais Magufuli anaweza kuwatumbua ili nao wasubiri mahakama ya mafisadi?
Ama naye hakubaliana na ile orodha yote maana ulikuwa ni uzushi wa kujipatia umaarufu na huruma toka kwa wananchi.
Namsubiri Dr Slaa akirudi toka uhamishoni nae aje atupe usahii wa ile orodha kama bado anaisimamia ama inamarekebisho.
 
ndo umeandika nini?! nimerudia mara5 sijaelewa! unaandika kama umekurupushwa toka lumumba!
 
nachojua list of shame ilidukuliwa na kutolewa kwenye mtandao wetu wa chadema bila maelezo yoyote. baada ya kuona hivyo wakubwa tukang'amua yanayoendelea. kwamba mzee ametua ndani na miguu yote. na hakuna kuuliza chochote. tuliambiwa "SHUT UP YOUR MOUTH". kamanda Mbowe akapigilia msumari wa mwisho akaizika ajenda ya ufisadi. usengerema gani huu! !
 
makamanda msitukumbushe machungu! ! mnataka tutoe machozi hafharani nini
 
Back
Top Bottom