Lissu: Tuna vithibitisho na mashahidi wa utekaji toka serikalini, mawaziri mnaogopa nini?

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,885
Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, alikusudia kutoa Shilingi katika Bajeti ya Waziri Mkuu, akiitaka Serikali na Waziri Mkuu kutoa kauli ya Kuzuia Kikosi Maalumu cha Utesaji, utekaji udhalilishaji na mauaji kinachoratibiwa na Idara ya Usalama wa Taifa, kwa kuwa kikundi kazi hicho kinavunja katiba na sheria za nchi.



Ushahidi wa Utekaji,udhalilishaji , Utesaji na mauaji yanayofanywa na kikundi hicho ulitolewa na Tundu Lissu ambapo alisisima bungeni kuelezea kuwa wapo watu 18 anaowatetea Mahakamani ambao wapo tayari kutoa ushahidi huo, dhidi ya kikundi hicho kinachotumia nyumba iliyopo Mikocheni na Oysterbay ambapo watu mbalimbali wamekuwa wakisafirishwa kutoka mikoani mpaka kwenye nyumba hizo kuteswa kinyama bila jamii kujua.

Mbali na ushahidi wa wazi wa Nape kutishiwa bastola hadharani, Bashe kutishiwa maisha na usalama wa Taifa kuwa yupo kwenye orodha ya wabunge 11 wanaotakiwa kufanyiwa mabaya, Godbless Lema na Lissu mwenyewe kukamatwa na polisi bila kibali cha ukamataji kuwekwa rumande na kunyimwa dhamana, Ben Saanane kupotea, Ney wa Mitego kukamatwa, Roma Mkatoliki kutekwa na kuteswa, Clouds Media Group kuvamiwa na mtu ambaye Watanzania wote wanamjua na nashangaa kwanini bado ni Kiongozi wa Serikali na serikali imekaa kimya? Je, kuna baraka za Ikulu?

Jambo hilo limepingwa sana na Mawaziri wa CCM, Jenister Mhagama na Angela Kairuki kwa kuwa wamesema hakuna habari zozote za namna hiyo, wakidai kuwa hakuna utekaji nyara hapa nchini kuwa ni maneno ya baadhi ya watu wa mitandaoni wanoataka kuichafua Serikali.

Walimuomba Waziri Mkuu asitoe kauli yoyote kwa kuwa jambo hilo ni uchochezi. Mawaziri hao wameona matukio yote hayo si kitu wala si chochote katika nchi kana kwamba walioteswa si watu wanaowahusu, wala hao hawastahili kulindwa utu wao na kana kwamba si Watanzania. Mawaziri hao wameitetea Serikali na kumwomba Spika kuwa Hoja hiyo isijadiliwe Bungeni.

Jambo hilo lilimpelekea Spika kutaka kura ipigwe na ndipo Wabunge walio wengi wakaomba kujadili kwa kina na serikali itoe kauli. Spika kwa mamlaka yake ameamua jambo hilo lisijadiliwe kabisa ndani Bunge.

My Take katika hili:

Kama Mawaziri na baadhi ya wabunge wa CCM wasiotaka jambo hilo lijadiliwe Bungeni kwa mustakabali wa amani ya Taifa letu, wanadhani kuwa wanaweza kumzuia Mungu asilete wokovu wa Taifa hili kwa njia ya Bunge basi wajue kuwa Mungu ataleta wokovu wa Taifa hili kwa njia nyingine.
 
Kama mnaweza bas "SAA YA MAPAMBANO IMEFIKA" tuache kulialia na baadhi ya viongozi wa serikali ya CCM na na CCM wanaojipendekeza kwa serikali yao na vibaraka kutoka sehemu tofauti km (mnyamwezi wa cuf) kwa kuvunja katiba.

Ni lazima tuoneshe kuilinda katiba kwa vitendo ili tulitoe PANGONI hili GENGE la mateso na mauaji. The time for fierce confrontation is now...let NOT tomorrow...!
 
Mna vithibitisho vya mabomu soweto, vithibitisho vya ufisadi wa lowasa, vithibitisho chungu nzima hamjavitoa.
Tutawaamini aje.
 
Back
Top Bottom