Kuna uvumi mkubwa unaotanda Mkoani Singida, kuwa Mbunge wa jimbo la singida Mashariki, Tundu Lissu huenda akavuliwa Ubunge kama alivyofanyiwa Lema. Japo bado kesi inaendelea, wananchi wameanza kukata tamaa kwa kuona vikao vingi vya Viongozi wote wa CCM, pamoja na waliosadikiwa ni Usalama wa Taifa toka Ikulu. vikao hivyo vilifanyika Jengo la CCM Mkoa jana. Mmojawapo ya vitu vinavyozidi kutoa shaka, ni kuwa Alhamisi walalamikaji ambao ni CCM walisema kuwa wangefunga ushahidi, baada ya shahidi wao wa mwisho kuja kuwaumbua mahakamani kwa kusema ukweli, pamoja na kuwa walimnunua kwa pesa inayosadikiwa kufika milioni 5, Jaji alikubaliana na maombi ya kuanza kuletwa mashahidi wengine wapya. HATUELEWI Jaji kwanini aliomba upande wa walalamikaji kuendelea kuleta mashahidi wakati walalamikaji walisema wanafunga ushahidi siku hiyo. Shahidi aliyemalizia anaitwa Hasani Musuna aliwaumbua vibaya sana CCM pamoja na kumhonga, mpaka ikabidi aombe ulinzi wa polisi, na siku hiyo alitolewa na gari ya RCO Kupelekwa kwao. kabla ya kuja Mahakamani, CCM walijihakikishia kuwa shahidi huyo angewaumbua sana CHADEMA kwa ushahidi wa kutunga, na CCM wakawasadikisha polisi kuwa Shahidi huyo alikuwa anaenda kutoa majibu yote na hivyo wafuasi wa CHADEMA wangeleta fujo mahakamani. Polisi walifika mahakamani siku hiyo wana mabomu ya machozi, Bunduki na Virungu na Risasi za moto. Ila baada ya huyo shahidi kumaliza, WOTE WALIONDOKA VICHWA CHINI. Kama kweli kuna njama kama hizo Basi Kikwete atakuwa ameamua kuipeleka nchi anakotaka yeye:Tusubiri hatima: