Lisemwalo lipo..: Arusha yathibitisha!

Lisemwalo lipo..: Arusha yathibitisha!

Lakini hajasema atakayekuja kumdhamini naye awekwe ndani.kutetea maana yake fasaha ni kumsaidia, kumficha, kuiingilia, mamlaka inayohusika kuishawishi ili isimtie hatiani,kuharibu ushahidi kwa lengo makusudi,mimi nilielewa hivyo.
Wewe ulielewa hivyo lakini yeye hakumaanisha hivyo ulivyoelewa!
 
Wewe ni hewa nafikiri.T.L hata kama akichaguliwa hawezi kuwa jaji mkuu wa TZ au mwanasheria mkuu wa serikali ebo!!!atabaki hivyo ila nahofia kufa kwa chama hicho cha TLS na CDM kwa pamoja.
Hivi umepiga Mswaki kabla ya kuandika
 
Hata kutaja majina ya watu kwenye vyombo vya habari bila kuwa na ushahidi nako ni kubambikia watu kesi. Tunayaona haya kila siku. Mahakama zipo, lakini watu wanaona fahari zaidi kuacha kuzitumia.
 
Avatar na unayoandika asubuhi hii inathibitisha WEWE ni either ni mbwia MADAWA YA KULEVYA au MNYWA VIROBA ASUBUI KUPATA MZUKA......
Kisukule mama ya Lumumba...bado hujapewa ile buku 7 ukanywe chai?
 
Mkuu,umeiona hoja yangu. Hongera!
Kuna sample za kesi nyingi na wewe bora umetoa moja hii inayoeleweka kwa wengi wetu.
Arusha itathibitisha mengi, mfano scenario ya Mh. si kama tu kabambikiwa na kulazimisha asitoke lumande! Wanaoangalia mbele wanajua kuwa adui yetu ni umasikini, ujinga na maradhi na kumweka mtu ndani kwa kumkomoa hakika hakutaondoa moja kati ya hawa maadui na wala hakutapelekea ujenzi hata wa msingi wa kiwanda.
 
Mm nashangaa sana kwa mkulu kusema mtu akikutwa na kitu haramu awekwe ndan hata kama mtetez wake nae awekwe hivi kwa stail hii ya kubambikiwa kesi siwataenda wasio na hatia?

Hata Mkulu anaweza kuongea "pointless". Haina maana ukiwa Mkulu kila unachoongea ni sahihi. Mkulu ni mwanadamu kama wewe, anakula, anakunywa na kisha.....
 
Imekuwa ikisemwa sana kuwa wapo askari polisi wasio waaminifu wanaowabambikia wananchi kesi kwa lengo la kuwaomba rushwa au kuwakandamiza. Ndiyo maana,sisi Mawakili hujitokeza kuwatetea watuhumiwa kwakuwa si wote waliotenda kweli

Huko mkoani Arusha,askari polisi mmoja amekamatwa kwa kuwabambikia wananchi madawa ya kulevya kama bangi kwa lengo la kuomba rushwa. Askari huyo aliyekamatwa,kwa mujibu wa ITV Habari,ni kielelezo na uthibitisho kuwa kubambika kesi kupo

Kimsingi,kutaja au kuhoji au hata kushtaki mwananchi kwa tuhuma fulani si mwisho wa mambo. Ni mwanzo tu unaoficha mambo mbalimbali yakiwemo ya watu kusingiziwa kesi au vizibiti. Ndiyo maana, ipo haja ya kuwa makini na kesi za wananchi na kuacha mapambano ya kimahakama yaseme na kutenda haki.
 
Lakini hajasema atakayekuja kumdhamini naye awekwe ndani.kutetea maana yake fasaha ni kumsaidia, kumficha, kuiingilia, mamlaka inayohusika kuishawishi ili isimtie hatiani,kuharibu ushahidi kwa lengo makusudi,mimi nilielewa hivyo.
Wewe ulivyomuelewa, na wengine walivyoelewa wote mko sawa mpaka hapo yeye atakapotoa ufafanuzi akitaka, huna uhalali wa kukataa uelewa wa yule.
 
Back
Top Bottom