Lizaboni
JF-Expert Member
- Feb 21, 2013
- 33,901
- 20,410
Kwa siku za karibuni, mwelekeo wa mwenyekiti wa CUF, Ibrahim Lipumba, unazua maswali mengi sana. hali hii inafanya baadhi ya watu waanze kutilia mashaka uzalendo wake hali inayomfanya aonekane kuondokana kabisa na zile siasa zake za kistaarabu. kwamba, wakati Maalim Seif akichochea vurugu kule zanzibar kabla ya yale maridhiano, mzee lipumba alikuwa na mwelekeo tofauti kwa kupinga siasa za vurugu. hali hiyo ilimfanya aheshimike sana kitaifa na kimataifa.
Mashaka yangu yameanza pale alipoanza kuzua kuwa Rais JAKAYA KIKWETE anandaa mazingira ili abaki madarakani hadi mwaka 2017. Kwamba kikwete anataka mchakato wa katiba mpya uchelewe ili aendelee kuongoza nchi mpaka muda huo. Kanusho la Ikulu kuhusiana na taarifa hiyo limemvunjia heshima mzee Lipumba na amejidhalilisha.
Hivi punde kuna taarifa zimeanza kuzagaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa kesho tarehe 17/5/2013, shughuli za kijamii zitasimama mjini mtwara ili wananchi wapate fursa ya kusikiliza hotuba ya waziri wa nishati na madini. Sijui taarifa hizo wamezipata wapi maana nijuavyo mie ni kuwa waziri wa nishati anawasilisha hotuba yake Jumatano ijayo na si kesho kama uzushi huo ulivyokuwa. Shauku yao ni kutaka kujua jinsi serikali ilivyoshughulikia madai yao ya kupinga usafirishwaji wa gesi ghafi.
Kilichonishangaza zaidi ni ushiriki wa mzee Lipumba kwenye sakata hilo. kuna baadhi ya wananchi ambao wanajua undani wa sakata hilo, wamedokeza kuwa IBRAHIM LIPUMBA, Mwenyekiti wa CUF amepewa fedha na makampuni ya mafuta na gesi yakiongozwa na kampuni ya AGGRECO, ili ahamasishe wananchi wa mtwara wagomee mpango wa serikali. Pia mzee Lipumba ameandaa watu wake ili hiyo kesho walete fujo na kupora mali za wananchi. inadaiwa kuwa makampuni hayo yanapinga mradi huo ili yaendelee kunufaika na biashara ya mafuta na gesi toka mataifa ya nje. Makampuni hayo ya mafuta inadaiwa kuwa yanatumia fedha nyingi kuwanunua watu wenye ushawishi kwenye jamii ya wana Mtwara ili kuchochea vurugu.
Kutokana na hali hiyo, nimeanza kupata mashaka na kuanza kujiuliza, upo wapi uzalendo wa mzee lipumba, uko wapi usomi wa mzee lipumba ambaye alikuwa anatumia elimu yake kuishauri serikali. kwa hili la kuhamasisha vurugu na uvunjaji wa amani ni wazi kuwa huyu mzee ameanza kufilisika kimawazo. Najua kuwa anatumika na makampuni hayo ya mafuta kama tulivodokezwa, ila cha kujiuliza ni kuwa anafanya hayo kwa faida ya nani? Ona sasa jeshi la polisi limepeleka askari wengi mtwara na silaha za kutosha kudhibiti vurugu hizo, je wananchi wakiuawa, yeye atapata faida gani. hilo likitokea najua kuna watu watageuka. Wale waliokuwa wanasema kuwa serikali ni dhaifu wataanza kusema kuwa serikali ni kandamizi.
Hayo ni maoni yangu tu.
SOURCE: mimi mwenyewe
Mashaka yangu yameanza pale alipoanza kuzua kuwa Rais JAKAYA KIKWETE anandaa mazingira ili abaki madarakani hadi mwaka 2017. Kwamba kikwete anataka mchakato wa katiba mpya uchelewe ili aendelee kuongoza nchi mpaka muda huo. Kanusho la Ikulu kuhusiana na taarifa hiyo limemvunjia heshima mzee Lipumba na amejidhalilisha.
Hivi punde kuna taarifa zimeanza kuzagaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa kesho tarehe 17/5/2013, shughuli za kijamii zitasimama mjini mtwara ili wananchi wapate fursa ya kusikiliza hotuba ya waziri wa nishati na madini. Sijui taarifa hizo wamezipata wapi maana nijuavyo mie ni kuwa waziri wa nishati anawasilisha hotuba yake Jumatano ijayo na si kesho kama uzushi huo ulivyokuwa. Shauku yao ni kutaka kujua jinsi serikali ilivyoshughulikia madai yao ya kupinga usafirishwaji wa gesi ghafi.
Kilichonishangaza zaidi ni ushiriki wa mzee Lipumba kwenye sakata hilo. kuna baadhi ya wananchi ambao wanajua undani wa sakata hilo, wamedokeza kuwa IBRAHIM LIPUMBA, Mwenyekiti wa CUF amepewa fedha na makampuni ya mafuta na gesi yakiongozwa na kampuni ya AGGRECO, ili ahamasishe wananchi wa mtwara wagomee mpango wa serikali. Pia mzee Lipumba ameandaa watu wake ili hiyo kesho walete fujo na kupora mali za wananchi. inadaiwa kuwa makampuni hayo yanapinga mradi huo ili yaendelee kunufaika na biashara ya mafuta na gesi toka mataifa ya nje. Makampuni hayo ya mafuta inadaiwa kuwa yanatumia fedha nyingi kuwanunua watu wenye ushawishi kwenye jamii ya wana Mtwara ili kuchochea vurugu.
Kutokana na hali hiyo, nimeanza kupata mashaka na kuanza kujiuliza, upo wapi uzalendo wa mzee lipumba, uko wapi usomi wa mzee lipumba ambaye alikuwa anatumia elimu yake kuishauri serikali. kwa hili la kuhamasisha vurugu na uvunjaji wa amani ni wazi kuwa huyu mzee ameanza kufilisika kimawazo. Najua kuwa anatumika na makampuni hayo ya mafuta kama tulivodokezwa, ila cha kujiuliza ni kuwa anafanya hayo kwa faida ya nani? Ona sasa jeshi la polisi limepeleka askari wengi mtwara na silaha za kutosha kudhibiti vurugu hizo, je wananchi wakiuawa, yeye atapata faida gani. hilo likitokea najua kuna watu watageuka. Wale waliokuwa wanasema kuwa serikali ni dhaifu wataanza kusema kuwa serikali ni kandamizi.
Hayo ni maoni yangu tu.
SOURCE: mimi mwenyewe