GwaB
JF-Expert Member
- Mar 19, 2014
- 3,593
- 4,657
Kwa jinsi hali ilivyo hivi sasa pale Dodoma na mchakato mzima ulivyoanza tangu mwanzo ni wazi kabisa bila mashaka matarajio ya katiba bora ni kidogo sana.Hatua ya prof.Lipumba kujitoa nampongeza sana kwa kuweka maslahi ya nchi mbele.kuburuzwa kwa namna yoyote ile ya baadhi ya wajumbe kwa kisingizio cha wingi wa CCM ni kigezo tosha cha kukosea tangu mwanzo kama waasisi walivyokosea kwa kujifungia vyumbani na kusaini muungano wa nchi kubwa kama Tanganyika na nchi inayolingana na baadhi ya mikoa ya Tanganyika,hii haikuwa sawa tangu mwanzo na nategemea wale wajumbe 200 wakuteuliwa wafanye kitu kimoja muhimu,kuirudisha Tanganyika au wajitoe kwenye hiyo shughuli ya CCM ili tuanze upya.Gharama siyo hoja kwa jambo muhimu kama hili.:A S 13: