Lionel Messi apigwa faini

Lionel Messi apigwa faini

Miss Halima

Senior Member
Joined
Aug 4, 2026
Posts
132
Reaction score
317
Lionel Messi wa Inter Miami amepigwa faini kwa kumpiga kofi Quinn Sullivan mchezaji wa klabu ya Philadelphia Union wakati wa mchezo ulioisha kwa sare ya 2-2 katika Mechi ya Ligi Kuu ya Soka (MLS) Jumatano mnamo Agosti 19.

Messi mwenye umri wa miaka 39, alimpiga Sullivan kofi kichwani kuelekea mwisho wa mchezo huku akilalamika kwamba mchezaji wa Union alikuwa amempiga kiwiko baada ya kuucheza mpira.
Sullivan alijibu kwa hasira kofi hilo, lakini mwamuzi aliingilia kati haraka.

MLS imethibitisha Messi amepigwa faini, lakini haijafichua kiasi hicho.

Messi alifunga bao la pili la Miami katika Uwanja wa Subaru Park, akifunga bao la kwanza tangu baba yake afariki.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Argentina hakuwa pekee aliyepambana na Sullivan, kwani Ian Fray wa Miami pia almepigwa faini na MLS.

Fray alimshika shingo Sullivan baada ya wachezaji wote wawili kugongana Sullivan alipopoteza nafasi yake kwenye eneo la hatari.

Mechi ya hasira iliisha kwa kadi mbili nyekundu huku Yannick Bright wa Miami na kaka yake Sullivan Cavan wote wakitolewa nje kwa kadi nyekundu katika dakika za mwisho.

Hata hivyo, adhabu ya Cavan ya mchezo mmoja imefutwa baada ya mapitio na ya Yannick imeendelea kubaki kama adhabu.

1787397468496.png
 
Hivi ndivyo Ronaldo na Messi wamekuwa wakiwa treat wapinzani wao
1787398047489.png


Kwa miaka tumekuwa tukiambiwa kuwa Ronaldo ni mchezaji mwenye nidhamu mbaya, huku Messi akiwa portrayed kama mr nice guy au the humble guy.

But when you put the narratives aside and judge them by their actions, it tells a very different story.

Messi is every bad thing the media told you Cristiano Ronaldo was.
1787398279087.png


Da'Vinci
Greatest Of All Time
herman joshua

1787397917865.png
 
Interpreted by AI assistance. Ulishindwa kuiandika kwa kiswahili cha kawaida ambacho tumekizoea mkuu?
 
Basi hata hii issue tu, nayo itakua ni faraja kwa wale mashabiki wa yule Mbuzi wa ureno,

Wao hata Messi akijikwaa tu njiani hua wanafanya sherehe.

Leo MESSI The GOAT.
Hao mashabiki watakuwa ni wajinga sana na ni wa kuwapuuza Mkuu.

Messi kafanya kila kitu kwenye mpira na hatumdai. Hata hii ballon d'Or anastahili kabisa.

FB_IMG_1787404061999.jpg
 
Back
Top Bottom