Miss Halima
Senior Member
- Aug 4, 2026
- 132
- 317
Lionel Messi wa Inter Miami amepigwa faini kwa kumpiga kofi Quinn Sullivan mchezaji wa klabu ya Philadelphia Union wakati wa mchezo ulioisha kwa sare ya 2-2 katika Mechi ya Ligi Kuu ya Soka (MLS) Jumatano mnamo Agosti 19.
Messi mwenye umri wa miaka 39, alimpiga Sullivan kofi kichwani kuelekea mwisho wa mchezo huku akilalamika kwamba mchezaji wa Union alikuwa amempiga kiwiko baada ya kuucheza mpira.
Sullivan alijibu kwa hasira kofi hilo, lakini mwamuzi aliingilia kati haraka.
MLS imethibitisha Messi amepigwa faini, lakini haijafichua kiasi hicho.
Messi alifunga bao la pili la Miami katika Uwanja wa Subaru Park, akifunga bao la kwanza tangu baba yake afariki.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Argentina hakuwa pekee aliyepambana na Sullivan, kwani Ian Fray wa Miami pia almepigwa faini na MLS.
Fray alimshika shingo Sullivan baada ya wachezaji wote wawili kugongana Sullivan alipopoteza nafasi yake kwenye eneo la hatari.
Mechi ya hasira iliisha kwa kadi mbili nyekundu huku Yannick Bright wa Miami na kaka yake Sullivan Cavan wote wakitolewa nje kwa kadi nyekundu katika dakika za mwisho.
Hata hivyo, adhabu ya Cavan ya mchezo mmoja imefutwa baada ya mapitio na ya Yannick imeendelea kubaki kama adhabu.
Messi mwenye umri wa miaka 39, alimpiga Sullivan kofi kichwani kuelekea mwisho wa mchezo huku akilalamika kwamba mchezaji wa Union alikuwa amempiga kiwiko baada ya kuucheza mpira.
Sullivan alijibu kwa hasira kofi hilo, lakini mwamuzi aliingilia kati haraka.
MLS imethibitisha Messi amepigwa faini, lakini haijafichua kiasi hicho.
Messi alifunga bao la pili la Miami katika Uwanja wa Subaru Park, akifunga bao la kwanza tangu baba yake afariki.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Argentina hakuwa pekee aliyepambana na Sullivan, kwani Ian Fray wa Miami pia almepigwa faini na MLS.
Fray alimshika shingo Sullivan baada ya wachezaji wote wawili kugongana Sullivan alipopoteza nafasi yake kwenye eneo la hatari.
Mechi ya hasira iliisha kwa kadi mbili nyekundu huku Yannick Bright wa Miami na kaka yake Sullivan Cavan wote wakitolewa nje kwa kadi nyekundu katika dakika za mwisho.
Hata hivyo, adhabu ya Cavan ya mchezo mmoja imefutwa baada ya mapitio na ya Yannick imeendelea kubaki kama adhabu.