Lini tutasema sasa Inatosha!

Lini tutasema sasa Inatosha!

Travelogue_tz

JF-Expert Member
Joined
Sep 28, 2010
Posts
855
Reaction score
1,224
Kwa zaidi ya miaka 15 nimekuwa nikifuatilia historia na matukio mengi yanayohusu harakati za kisiasa za Vyama vya Upinzani Tanzania.
Tumejionea mauaji, mateso, manyanyaso, ubaguzi ,chuki na machukizo ya kila aina dhidi ya Wapinzani wa Chama tawala -CCM.
Tumeshuhudia mauaji ya Alfonce Mawazo aliyepigwa risasi
Tumeshuhudia jaribio LA mauaji ya Tundu Antipas Lissu
Tumeonana wanachama lukuki wa opposition parties wakiuwawa au kujeruhiwa.
Tumeshuhudia ubaguzi wa kimaendeleo dhidi ya Upinzani.
Leo Tumeshuhudia mawakala wakitolewa nje kabisa ya polling stations, baadhi yao kutekwa, wengineo kukatwa mapanga.
Je, tunasubiri nini kitokee ili kuchukua hatua madhubuti? Hili ni swali gumu kwa opposition supporters ---
 
Kwa zaidi ya miaka 15 nimekuwa nikifuatilia historia na matukio mengi yanayohusu harakati za kisiasa za Vyama vya Upinzani Tanzania.
Tumejionea mauaji, mateso, manyanyaso, ubaguzi ,chuki na machukizo ya kila aina dhidi ya Wapinzani wa Chama tawala -CCM.
Tumeshuhudia mauaji ya Alfonce Mawazo aliyepigwa risasi
Tumeshuhudia jaribio LA mauaji ya Tundu Antipas Lissu
Tumeonana wanachama lukuki wa opposition parties wakiuwawa au kujeruhiwa.
Tumeshuhudia ubaguzi wa kimaendeleo dhidi ya Upinzani.
Leo Tumeshuhudia mawakala wakitolewa nje kabisa ya polling stations, baadhi yao kutekwa, wengineo kukatwa mapanga.
Je, tunasubiri nini kitokee ili kuchukua hatua madhubuti? Hili ni swali gumu kwa opposition supporters ---
Let nature take its own course!!! Hayatokei bure haya,kuna jambo.
CCM ina idadi kubwa ya wabunge na madiwani na pia inaongoza serikali kwa nini itumie nguvu kiasi hiki?
Huu ulikuwa uchaguzi wa kujipima na kujirekebisha lakini umetonesha vidonda na unaigawa nchi kwa kasi kubwa.
Binafsi si mshabiki wa vurugu na kuliko iendelee kumwagika damu ni afadhali CCM ichukue viti vyote na maisha yaendelee.
 
Dunia leo imejua kuwa CCM ni hatari sana, hata kama wapinzani watashindwa lakini ukweli umejulikana kuwa CCM inachukiwa kupita kiasi.
 
Kwa zaidi ya miaka 15 nimekuwa nikifuatilia historia na matukio mengi yanayohusu harakati za kisiasa za Vyama vya Upinzani Tanzania.
Tumejionea mauaji, mateso, manyanyaso, ubaguzi ,chuki na machukizo ya kila aina dhidi ya Wapinzani wa Chama tawala -CCM.
Tumeshuhudia mauaji ya Alfonce Mawazo aliyepigwa risasi
Tumeshuhudia jaribio LA mauaji ya Tundu Antipas Lissu
Tumeonana wanachama lukuki wa opposition parties wakiuwawa au kujeruhiwa.
Tumeshuhudia ubaguzi wa kimaendeleo dhidi ya Upinzani.
Leo Tumeshuhudia mawakala wakitolewa nje kabisa ya polling stations, baadhi yao kutekwa, wengineo kukatwa mapanga.
Je, tunasubiri nini kitokee ili kuchukua hatua madhubuti? Hili ni swali gumu kwa opposition supporters ---
Haya ni matatizo ya utawala yanayostahili kufanyiwa kazi. Ktk CCM naamini wanatakiwa kuwa wamekomaa kiasi kwamba waachane na siasa za kulaumiwa. Siasa siyo njama mbaya kiasi hiki. Kwa sasa mambo haya yanaonekana kuwasumbua opposition lakini itafikia wakati yatasambaa na kila mmoja ataona ndiyo mbinu ya kupambana na mpinzani wako.

Kwa upande wa opposition pia kuna kichefuchefu. Tunachoona siyo kuimarisha siasa, ni kutafuta umaarufu binafsi na kujitajilisha. Iweje miaka yote hii ya kuwepo kwa CUF, NCCR, CHADEMA, nk. hadi leo hakuna chama kilichojiweza hata kujiwekea mifumo ya kudumu. Leo hii CHADEMA ina wabunge wengi kiasi cha kujiimarisha hata kiuchumi lakini, wapi! Watu wanapiga tu ruzuku na misaada. Hata kujenga ofisi moja ili ionekane ndo makao yao makuu ktk nchi, hakuna!! NO! Tusilie lie wakati hatujiinui. Ofisi kuu ya CHADEMA, CUF, NCCR, nk. ktk nchi ni wapi? Hapo kwenye kupanga?
 
hakuna demokrasia utawala huu.demokrasia imebaki kwenye makaratasi yakuombea misaada.uimla umetamalaki.
 
Kila lililo na mwanzo huwa na mwisho wake,tuiombee nchi yetu mema
 
Very soon.... Mungu atatusikia
Mpwa kesha tusikia sana! Nadhani hata yeye anatushangaa kwa uzoba tulionao kusubiri atushushie malaika wenye silaha watulinde na uonevu huu.
Nchi zote zilizokuwa na uonevu walioonewa walichukua hatua thabiti na watawala manyangau walisalimu amri iwe sisi?
HAPANA, something should be done immediately
 
chadema wameaua red brigade.tayari uoga umewaingia zaidi ya kunguru. hata kupigwa lissu ulikuwa ni uzembe wa lissu na chadema yenyewe. walipaswa kumwekea cover fasta.
 
Kamanda wangu hakuna siku mtasikilizwa kama mlivyokuwa mnasikilizwa. Sahizi mnafanya siasa za kujijenga badala ya kujenga siasa na vyama.

Sijaona hata siku moja mnasema juu ya msitakabali wa maendeleo ya nchi kwa kutumia sera zetu na falsafa za kwetu. Tumebaki watu wa kulaumu na kusema na si kuleta mbadala wa mawazo. Mnakosoa kwa kupiga kelele si kujenga.

Pia, angalia mnavyoamua vitu vyenu. Wengi mmetukatisha tamaa sana. Hatujui tuko wapi katika chama na tunaelekea wapi. Hii ni kwa mtu aliyeenda shule zaidi. hatuoni!!!

Tujitafakari na kurudi tulipoanguka, tuendelee. Si ngonjera hizi za FB na JF.

Rudisha chama cha 2005-2015.

Usajili wa dirisha dogo 2015 na kuwahakikishia kila kitu ndani ya chama, imetuangusha sana. Ingawa si wengi wanataka sikia haya. Hata wewe hutaki sikia.

Mwaka 2020 ni zamu zenu. Naamini mtapigwa hata mtashindwa kuomba maji.
 
Back
Top Bottom