Lini Frederick Sumaye amejiunga na CHADEMA?

Lini Frederick Sumaye amejiunga na CHADEMA?

Huyo mwanajeshi ni muhimu sana atujuze namna ya kuikabili green coler
 
View attachment 347319 View attachment 347319

Aliwahi kusema Mwalimu Nyerere kuwa ili maendeleo ya kweli yawezefikiwa moja ya vigezo vya kuzingatowa ni Siasa Safi na Uongozi bora.

Siasa safi niliyoielewa mimi ni pale panapokuwa na uhuru wa kufanya shughuli za kisiasa kwa maana ya kuwa wananchi wana uhuru wa kushiriki siasa kupitia vyama vyao na kwamba viongozi wa vyama hivyo wanasimamia maslahi mapana ya nchi ya vyama vyao na siasa kwa ujumla.

Hivi karibuni kuna vituko vimetokea na hivi ni vya kujiuliza wapi tunaelekea. Mwenyekiti wa CHADEMA alimpendekeza Aliyekuwa Fredrick Sumaye kuwa Mjumbe wa CC ya Chadema. Sio jambo baya lakini kwa sisi wana duru la siasa linatuachia Maswali mengi sana. Moja kubwa ni hili LINI SUMAYE AMEJIUNGA NA CHADEMA?

Katika mahojiano na Vyombo vya Habari mwezi wa 12 , 2015 Bwana Sumaye alikiri mwenyewe kuwa hajajiunga na Chama chochote cha siasa baada ya kutoka CCM. Isipokuwa moyoni mwake alieleza nia yake ya dhati ya kuona kuwa Ccm inasambaratika kwa kuwa sasa muda umefika.

Kwa fikira ndogo za mtu kama mimi nilidhani Chama kingejiridhisha kwamba juu ya Utayari wa mtu kama. Sumaye ambaye uenda anakwenda Chamani kutafuta ajira tu na sio kukisaidia chama. Ikumbukwe pia katika vikao vya uteuzi wa katibu mkuu wa Chama, mwenyekiti Mbowe aliwahi kutaka Sumaye awe katibu mkuu kabla jaribio lake hilo kushindikana na kuwa na jina la mtu ambaye hakuwa ameandaliwa na leo hii tunashuhudia chama kurudi ofisini tofauti na kilivyokuwa siku za nyuma.

Je hatujajifunza ya Mwalimu Juma Duni? Chadema kiliwahi kufanya jaribio katika kile kilitafsiriwa na wengi sisi kuwa jaribio la kuchukua nchi kwa hila. Walimchukia Lowasa toka CCM NA Duni toka CUF . Kilichoendelea kitoshe kuwa sehemu ya vituko. Babu Duni leo yuko CUF Karudi Chama chake na Lowasa anashinda barabarani tu akinunua mahindi na kuchekesha kuwa anakubalika wakati JPM anachanja mbuga na wananchi wanasoma Namba.

Turudi kwa Sumaye, Lini umejiunga na Chadema? Maana kwa umaarufu na umuhimu wako nilitaraji kusikia siku maalumu ya kupewa kadi ya Uanachama. Kwa maneno yako ulitwambia kuwa wewe hautojiunga na chama chochote. Au mwenyekiti Mbowe unaendelea na cinema zako zile.naomba kuwasilisha.
Wewe unaishi dunia gani? Mbona alishapewa kadi kwenye mkutano Wa hadhara Arusha? Fanya research kabla ya kutokwa mapovu hapa
 
Badala ya kutumia nguvu kuuliza swali juu ya swali, wana CHADEMA tungekuwa waumgwana tu kueleza ukweli. Wana CDM tunajua kuwa Sumaye si member wa chama chetu. Tunajua kuwa Sumaye ndiye anayeandaliwa kuwa mrithi wa Lowasa 2020. Tunajua kuwa hapa ni biashara tu inayofanyika na hakuna siasa safi. Mbowe kwa hii kashfa hastahili kuwa Mwenyekiti
ondoa neno chetu wewe ni wa lumumba,
 
Hoja yako ni nzuri maana yawezekana hukuwahi kusikia kuwa sumaye amejiunga na chama cha siasa baada ya kutoka ccm ila ulichokosea kabisa umeambatanisha na Mipasho kwenye hoja au swali lako hili...ila nashukuru watu wamekujibu lini sumaye amekabidhiwa kadi ya chadema...
 
Pamoja na uandishi wake kutatiza, ila swali alilouliza ni la msingi. Hivi mtafanyaje maamuzi ya kumteua mtu kuwa mjumbe wa CC ilhali si mwanachama wa chama hicho? Hii ni mara ya pili CHADEMA mnafanya kosa hili. Kwa mara ya kwanza mlimyeua mtu ambaye si mwana CHADEMA kuwa mgombea Mwenza na sasa mnamteua Sumaye kuwa Mjumbe wa CC ili mwaka 2020 awe mgombea Urais wenu
aziri mkuu wa awamu ya tatu Mh.Fredirick
Sumaye amtangaza rasmi kujiunga na chama
cha Demokrasia na maendeleo Chadema na
amekabidhiwa kadi na Mwenyekiti wa chama
hicho Mh.Freeman Mbowe.
Sumaye ambaye wakati wa uchaguzi alitangaza
kujiondoa CCM na kudai kuwa anaunga mkono
mageuzi yanayofanywa na vyama vinavyounda
katiba ya wananchi (UKAWA) bila kuweka
wazi kuwa yuko kwenye chama kipi kati ya
hivyo amesema asa ameamua kujiunga na
CHADEMA.
Akizungumza katika mkutano wa kufunga
kampeni za ubunge wa jimbo la Arusha kwa
chama cha CHADEMA uliofanyika kata ya baraa
Sumaye amesema anataka kuungana na
wanamageuzi wenzake katika kuendeleza
harakati za mabadiliko hapa nchini ambazo bado
zinaendelea.
Akizungumza baada ya kumkabidhi kadi
Mwenyekiti wa chama hicho Mh.Freeman
Mbowe amesema chadema na vyama washirika
wa UKAWA bado viko imara na vimeendelea
kuimarika na kwamba licha ya kudhulumiwa
ushindi azma yaoya kuleta ukombozi nchini iko
pale pale.
Awali aliyekluwa mgombea uras wa CHADEMA
akiwakilisha vyama vya umoja wa katiba ya
wananchi ukawa Mh.Edward Lowassa
ameendelea kuwataka watanzania wanaounga
mkono mabadiliko kuwa watulivu na kwamba kwa
vile wana dhamira ya dhati ya kuyaona
mabadiliko hakuna kukata tamaa kwani bado
kuna fursa yakufikiwa kwa malengo yao .
� Sumaye atangaza rasmi kuwa
mwanachama wa Chadema.
4
 
View attachment 347319 View attachment 347319

Aliwahi kusema Mwalimu Nyerere kuwa ili maendeleo ya kweli yawezefikiwa moja ya vigezo vya kuzingatowa ni Siasa Safi na Uongozi bora.

Siasa safi niliyoielewa mimi ni pale panapokuwa na uhuru wa kufanya shughuli za kisiasa kwa maana ya kuwa wananchi wana uhuru wa kushiriki siasa kupitia vyama vyao na kwamba viongozi wa vyama hivyo wanasimamia maslahi mapana ya nchi ya vyama vyao na siasa kwa ujumla.

Hivi karibuni kuna vituko vimetokea na hivi ni vya kujiuliza wapi tunaelekea. Mwenyekiti wa CHADEMA alimpendekeza Aliyekuwa Fredrick Sumaye kuwa Mjumbe wa CC ya Chadema. Sio jambo baya lakini kwa sisi wana duru la siasa linatuachia Maswali mengi sana. Moja kubwa ni hili LINI SUMAYE AMEJIUNGA NA CHADEMA?

Katika mahojiano na Vyombo vya Habari mwezi wa 12 , 2015 Bwana Sumaye alikiri mwenyewe kuwa hajajiunga na Chama chochote cha siasa baada ya kutoka CCM. Isipokuwa moyoni mwake alieleza nia yake ya dhati ya kuona kuwa Ccm inasambaratika kwa kuwa sasa muda umefika.

Kwa fikira ndogo za mtu kama mimi nilidhani Chama kingejiridhisha kwamba juu ya Utayari wa mtu kama. Sumaye ambaye uenda anakwenda Chamani kutafuta ajira tu na sio kukisaidia chama. Ikumbukwe pia katika vikao vya uteuzi wa katibu mkuu wa Chama, mwenyekiti Mbowe aliwahi kutaka Sumaye awe katibu mkuu kabla jaribio lake hilo kushindikana na kuwa na jina la mtu ambaye hakuwa ameandaliwa na leo hii tunashuhudia chama kurudi ofisini tofauti na kilivyokuwa siku za nyuma.

Je hatujajifunza ya Mwalimu Juma Duni? Chadema kiliwahi kufanya jaribio katika kile kilitafsiriwa na wengi sisi kuwa jaribio la kuchukua nchi kwa hila. Walimchukia Lowasa toka CCM NA Duni toka CUF . Kilichoendelea kitoshe kuwa sehemu ya vituko. Babu Duni leo yuko CUF Karudi Chama chake na Lowasa anashinda barabarani tu akinunua mahindi na kuchekesha kuwa anakubalika wakati JPM anachanja mbuga na wananchi wanasoma Namba.

Turudi kwa Sumaye, Lini umejiunga na Chadema? Maana kwa umaarufu na umuhimu wako nilitaraji kusikia siku maalumu ya kupewa kadi ya Uanachama. Kwa maneno yako ulitwambia kuwa wewe hautojiunga na chama chochote. Au mwenyekiti Mbowe unaendelea na cinema zako zile.naomba kuwasilisha.
Ulikuwa unaelekea kuwa na swali zuri japo swali lenyewe umeleta kwa sababu tu hufuatilii vyombo vya habari. Sumaye ni mwanachama wa Chadema. Umeharibu ulipoanza kuingiza mambo ya akina Haji Duni. Kama hadi leo hujui hata utaratibu uliotumika kwa Babu Duni kujiunga Chadema sidhani hata kama una deserve kuwa kwenye jukwaa hili!
 
Sumaye hivi sasa ameshakuwa mzoefu huko CDM, kadi alichukua muda mrefu tu baada ya uchaguzi mkuu.
 
Kwanza mlitupumbaza, kutulisha na kutukaririsha maneno wakati wa uchaguzi mwaka jana.watu tukahadaika mara tukakubali kubadili gia angani(zidumu fikra za mwenyekiti),mara mkatulisha maneno wamba dr slaa kahongwa an ccm,mara kaponzwa na mshumbushi n.k.na sasa mmemteua sumaye kuwa mjumbe wa halmshauri kuu.sasa nauliza hivi,ni kigezo gani kimetumika kumpa huo ujumbe??maana sumaye hana kadi ya chama chochote cha upinzani zaidi tu alisema amekuja kuongeza nguvu kwa lowasa,acheni kutufanya sisi mazezeta kiasi hicho,hizo habari za zidumu fikra za mwenyekiti na ufia chama inabidi zife
 
Kwanza mlitupumbaza, kutulisha na kutukaririsha maneno wakati wa uchaguzi mwaka jana watu tukahadaika mara tukakubali kubadili gia angani (zidumu fikra za mwenyekiti),mara mkatulisha maneno wamba Dr Slaa kahongwa na CCM,mara kaponzwa na mshumbushi n.k.na sasa mmemteua Sumaye kuwa mjumbe wa halmshauri kuu.

Sasa nauliza hivi, ni kigezo gani kimetumika kumpa huo ujumbe?Maana Sumaye hana kadi ya chama chochote cha upinzani zaidi tu alisema amekuja kuongeza nguvu kwa Lowassa, acheni kutufanya sisi mazezeta kiasi hicho,hizo habari za zidumu fikra za mwenyekiti na ufia chama inabidi zife.
 
Umedumaa akili hadi umesahau kuwa sumaye ni mwanachama wa CHADEMA, siyo (chadema)
 
Back
Top Bottom