Lindi yetu na Sri Lanka


kwa jinsi nilivyoona kiongozi kakataa utamaduni katumia mfumo.Ila huo mfumo ni wa siku nyingi sana na ni wa kitaifa ,kwa kihalisia ni utamaduni.Utamaduni si lazima uwe km DNA.kama anakubali ufisadi na wizi upo kila kijiji,na kila office na ni tabia iliyooota mizizi mikubwa there is no way mheshimiwa akataka usiitwe utamaduni.mwovu hafukuzwi na kushitakiwa bali huamishwa kituo.
 
Hiyo hapo chini ni quote kutoka kwenye ile thread ya "Maisha ya rais wa Iran",labda tu tuondoe hapo kwenye "shall remain poor",labda akimaanisha kumaliza uongozi ama utumishi wa umma bila kuitumia nafasi hiyo kujitayarisha.Hizo ni hatua za kiongozi makini,tena wa taifa lenye utajiri mkubwa wa mafuta na maendeleo wanayo.Lakini bado wanatambuwa umuhimu wa viongozi kutokujitajirisha kwa kutumia utumishi wa wa umma na kulifisadi taifa!Sasa hilo tu linaonyesha utofauti wa viongozi wetu.Tatizo la ufisadi inajulikana kila pahala kuwa ndo lenye kudumaza maendeleo.Lakini sisi wapi?
 

Siyo rahisi kuendelea katika mfumo huu tulio nao.ufisadi ni mkubwa kupindukia.TANZANIA ni nchi ya kwanza afrika kupata misaada lakini fedha hizo zimishia kujenga barabara mbovu na zisizo na kiwango.dawa ni kupiga chini ccm leta CHADEMA.
 
Mipango ya Maendeleo ya ujumla ni utopia zaidi inafaaa sana siasa za kutowajibika kama za Tanzania na ndio maana hatuwezi kuendelea hata kidogo.

Ili tuendelee lazima tutumie competitive advantage ya kila mkoa. Mtoa mada well done Challenge kwao watu wa Magogoni JK et al msiogope kudhutubutu kufanya vitu nje ya mazoe yenu.
 
kwa vile mke wa jk anatoka lindi basi kila kitu lindi..i miss nyerere,hakupendelea butiama kama bagamoyo inavyopendelewa sasa hivi..
 
Mfuate aliko,mtoa mada ametolea mfano mkoa Lindi na jinsi unavyoweza kundokana na umaskini sasa mke wa rais anakuja vipi hapa?
 
Mdogo wangu Zitto Zuberi Kabwe, huwa ninapenda sana tafiti zako na the they way ambavyo huwa una apply kile ulicho tafiti, hakika wewe ni moja kati ya hazina kubwa katika nchi hii hasa katika eneo la uchumi, napataga sana shida ninapo mwona na kumsikiliza Mwigule Mchemba hasa siku ile mlipo kuwa na interview pamoja pale TBC, wewe ndo hakika Waziri wa Fedha wa nchi hii, pengine wengine wamesahau, wewe ndo mwasisi wa chanzo cha fedha za kuendesha hivi Vyuo vya VETA (rejea bajeti ya upinzani mwaka jana). Tunao watu ndani ya magamba wamesoma masomo ya uchumi kama wewe, tena wengine wanadai walifauru vizuri kulioko wewe, lakini ukweli hatuoni interpretation ya kile walicho jifunza katika utendaji wao, Aibu kubwa.

Mwaka jana uliwahi kuja na issue ya Mkonge Tanga, tena kupitia Channel 10 nilikusikia umeisha fanya utafiti hadi wa soko kwani ulijua kabisa matumizi mapya ya Mkonge duniani, ulipoliweka suala hilo Bungeni,Mmmm, hata Wabunge wa mkoa wa Tanga nao wakakuijia juu,AIBU kubwa, sitashangaa sana mwaka 2015 wakazi wa Tanga tena wakawarudisha Wabunge wale wale tena (shida ya dini nayo ni tatizo kubwa sana kwa wapiga kura wa mikoa ya Pwani, huu utafiti wangu binafsi, sio taasisis yeyote), umezungumza sana issue ya gas, nani akusikilize? Wenzio wameng'ang'ania eti we unatoka chama cha upinzani, tumekuwa tuna mjaji mtu na sio alicho kisema, AIBU kubwa mno katika nchi yetu.

Nini kaka cha kufanya, ukweli haya yote hata na hakika unayo mengine mengi mno ya maendeleo au solution za kuikomboa nvhi hi katika lindi kubwa la umasikini, ndani ya chama hiki kinachaofaidika na umasikini wa Watanzania yaani ccm, sioni kama itawezekana, umasikini wa Watanzania, ccm inafaika nao sana tu, nimeona ulicho kifanya kule kwenu Kalinzi, Mkabogo, Matizyazo, hakika dogo umeboresha sana maisha ya watu wa kule kwa kilimo cha Kahawa tu, baadhi ya vijana wenyeji wa huko sasa hivi wamerudi huko na kukomaa na kilimo cha Kahawa, sababu, kina lipa sasa hivi, utasikia magamba wako busy eti kukomboa jimbo hilo, wao muhimu kwao ni kutawala na sio kuondoa umasikini, AIBU kubwa, kumbe tukiwa na Viongozi wa type yako inawezekana kabisa kupingana na matusi tuliowahi kutukanwa na akina Peter Botha, mimi narudia, shida kubwa ya nchi hii if not nchi zetu hizi za Kiafrika, sio Elimu, tunao wasomi wengi mno wazuri tu, shida yetu kubwa ni kutafsiri kile mtu alicho soma shule katika vitendo tu basi, issue sio Elimu kabisa, nakataa, hiyo ilikuwa sababu kwa miaka ya 70 na 80 na kidogo mika ya 90 mwanzoni but sio karne hii ya 21. Hima Watanzania, tushirikiane kuitokomeza ccm, ndio chanzo cha umasikini wetu, hakuna kingine!
 
mheshimiwa si yupo aifanya hii thread more interactive kwa kujibu na kutoa maoni yake.
 
 
Nchi nyingi za Asia na Mashariki ya mbali wanatumia mfumo wa serikali za majimbo, mfumo huu unawapa wananchi kuwa karibu zaidi na viongozi wao katika kupanga na kusimamia rasilimali za jimbo husika. kwa utaratibu huo maendeleo ya jimbo moja huleta impact kwa taifa. Vilevile mfumo wa majimbo huleta ushindani maendeleo wa jimbo moja na jingine. Mfumo tulionao sio rahisi kuendelea kwa kuwa kila kitu kinaamuliwa na wakubwa walioko Dar. Chukua mfano kulikuwa na maana gani kuagiza kila halmashauri ya wilaya kununua power tiller, je serikali yetu inaama kila mtanzania ni mkulima ? na kila halmashauri inaradhi bora ya kilimo cha kununua power tiller ?
 
Nchi nyingi za Asia na Mashariki ya mbali zinatumia mfumo wa serikali za majimbo, iwapo Tanzania tunataka kusongo mbele hatuna budi kuliweka jambo hili katika katiba. Mfumo wa majimbo unaweka wananchi karibu na viongozi wao na hivyo kupanga na kusimamia maendeleo kwa ukaribu zaidi. sisi mipango yetu imekuwa ni ya kitaifa bila kuangalia priorities za mikao. matokeo yake ni kuwa maamuzi yote hutolewa na viongozi wakuu wa kitaifa huku wa ngazi ya chini wakiwa ni watekelezaji tu. Majimbo yataleta umoja wa kitaifa na pia ushindani wa maendeleo kulingana na rasilimali zinazopatikana katika maeneo husika. Jiulieze kulikuwa na maana gani kuagiza kila halmashauri ya wilaya kununua power tiller ?, je inamaana kila mtanzania ni mkulima na je kila halmashauri ina ardhi inayofaa kwa kilimo cha power tiller, hii ni moja ya mipngo yetu mibovu ya kilimo. Katiba mpya tuweke mfumo wa mikoa au majimbo kuwa semi automous kwa maana viongozi wachanguliwe kwa kula za wananchi na wawe na mamlaka kamili ya kusimamia maendeleo
 
Yeah, I was there in SL in 2008 wakati huo vita vikiwa vimekolea sana, nakumbuka nilikatazwa kusafiri beyond mji mmoja unaitwa Kandy kuelekea Kaskazini. Kuhusu hiyo kama sh. 45,000 wanayopata madereva wa bajaj kwa siku, pengine ni chache sana kwani kule bajaj ndio taxi, na hata wenyewe wanaziita taxi na si rahisi kupata salon car for hire as a taxi, so ukitaka kulinganisha basi angalia dereva taxi wa Bongo anapata sh. ngapi kwa siku.

Wanaweza kusifiwa kwa kujikwamua kiuchumi kwa kasi, lakini kisiasa rais wao amefanya ubabe sana kwenye uchaguzi kwa kumnyanyasa mpinzani wake ambaye ndiye jenerali aliyeongoza vikosi kuwatimua Liberaration Tigers of Tamil Eelam aka Tamil Tigers. Tuige mfano wao kiuchumi, lakini nao waboreshe demokrasia! Nadhani watakuwa wameongeza viwanda, lakini hiyo 2008 walikuwa wanaimport sana kutoka India
 
Wakuu kumbe lindi nayo ina gesi nyingi hasa kilwa?

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…