kabiriga
JF-Expert Member
- Nov 18, 2012
- 1,163
- 1,213
Nina mchumba wangu (wakike) ni mwanafunzi wa chuo kikuu kimojawapo hapa nchini.Siku moja nilipata ujumbe kwenye simu yangu kutoka kwenye namba ngeni ukisomeka hivi ("Hapa huna mchumba jamaa wana mega kama nini") sikuelewa nini maana yake.Baada ya week kama mbili hivi siku moja nilimpigia simu mchumba wangu saa 3 na nusu usiku,tukaongea yetu na kisha tukatakiana usiku mwema .lakini sikukata simu yangu na sikuitoa sikioni nae pia hakukata nadhani kwa vile nilipiga mimi alidhani nitakata mimi.kisha baadae kidogo nikaanza kusikia mazungumuzo kati yake na mtu mwingine sauti ya kiume,kati ya mengine mengi niliyo yasikia ni mazungumuzo ya mahaba kati ya watu hao,siku hiyo ilikuwa jmosi ,kesho yake saa nane mchana nilipokea ujumbe kutoka kwa mchumba wangu analalamika kwanini nimechelewa kufika sehemu furani,sikuelewa nikitu gani kinaendelea kwani mimi nipo mbali nae na hatukuwa na miadi yeyote ya kukutana nae sehemu ile,kisha baadae kama dk 10 akatuma ujumbe mwingine akisema yeye amefika akiniuliza nipo wapi?nikazidi kushangaa sikujibu .nikapiga moyo konde nikangoja .kisha dk 30 baadae akatuma ujumbe wa kuniomba radhi kwani ujumbe uliokuja kwangu alikuwa anamtumia rafiki yake na kwakuwa namba yangu ya simu ndo ameizoea sana ameshtukia ameisha nitumia mimi.sikumjibu kwa wakati huo kisha nikaanza kuunganisha matukio.kichwa kinaumia nichukue uamuzi gani kwani nimeaanza kupoteza imani nae.Ushahuri wenu jamani