Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,346
- 26,138
Mahakama Kuu ya Tanzania iliyoketi leo chini ya Mtukufu Jaji Lugano Mwandambo imeahirisha kusikilizwa kwa maombi ya zuio la muda dhidi ya Mwigamba na wenzake na kupanga kusikilizwa kwa kesi ya msingi mnamo tarehe 15/4/2015. Kimsingi, Mwigamba na wenzake wataendelea na shughuli zote za chama hadi tarehe ya kusikilizwa kwa shauri hilo.
Kesi ya msingi ni kati ya Kadawi L. Limbu, Leopold Lucas Mahona na Grayson Manyori Nyakarungu dhidi ya Samson Mwigamba, Peter Mwambuja na Mohamed Masaga. Ni kesi ya madai nambari 17 ya 2015. Wadai waliwasilisha Maombi madogo nambari 21/2015 yakiomba, pamoja na mambo mengine, zuio la muda dhidi ya Wadaiwa-akina Mwigamba kutojihusisha na shughuli za ACT-Tanzania hadi kesi ya msingi itakaposikilizwa na kuamuliwa. Maombi hayo madogo yaliondolewa (were struck out) kutokana na upande wa Wadaiwa kukubali kuwa Maombi yao yalikuwa na mapungfu ya kisheria hasa katika kuifanya Mahakama itoe kinachmbwa (to move the court).
Wadai-akina Limbu waliwasilisha maombi madogo tena nambari 129/2015 wakiomba zuio la muda dhidi ya Mwigamba na wenzake na wateule wao hadi kumalizika kesi ya msingi. Maombi hayo madogo mapya yalipangwa kusikilizwa leo. Mawakili wa Mwigamba wakiongozwa na Wakili Msomi Mwandamizi John Mnaku B. Mhozya, pamoja na kupokea maombi hayo leo,walidokeza mapungufu mengine ya kisheria katika maombi madogo mapya na kupingwa kusikilizwa kwa maombi hayo madogo mapya leo.
Jaji Mwandambo amekubaliana na hoja za Mawakili wa Wadaiwa na ameamua kuwa kesi ya msingi itatajwa tarehe 15/4/2015 na hoja za kisheria kupokelewa siku hiyo. Hivyobasi,Mwigamba na wenzake ambao ni Wadaiwa/Wajibu Maombi watendelea kujihusisha na ACT-Tanzania hadi itaapoamriwa vinginevyo.
Kesi ya msingi ni kati ya Kadawi L. Limbu, Leopold Lucas Mahona na Grayson Manyori Nyakarungu dhidi ya Samson Mwigamba, Peter Mwambuja na Mohamed Masaga. Ni kesi ya madai nambari 17 ya 2015. Wadai waliwasilisha Maombi madogo nambari 21/2015 yakiomba, pamoja na mambo mengine, zuio la muda dhidi ya Wadaiwa-akina Mwigamba kutojihusisha na shughuli za ACT-Tanzania hadi kesi ya msingi itakaposikilizwa na kuamuliwa. Maombi hayo madogo yaliondolewa (were struck out) kutokana na upande wa Wadaiwa kukubali kuwa Maombi yao yalikuwa na mapungfu ya kisheria hasa katika kuifanya Mahakama itoe kinachmbwa (to move the court).
Wadai-akina Limbu waliwasilisha maombi madogo tena nambari 129/2015 wakiomba zuio la muda dhidi ya Mwigamba na wenzake na wateule wao hadi kumalizika kesi ya msingi. Maombi hayo madogo mapya yalipangwa kusikilizwa leo. Mawakili wa Mwigamba wakiongozwa na Wakili Msomi Mwandamizi John Mnaku B. Mhozya, pamoja na kupokea maombi hayo leo,walidokeza mapungufu mengine ya kisheria katika maombi madogo mapya na kupingwa kusikilizwa kwa maombi hayo madogo mapya leo.
Jaji Mwandambo amekubaliana na hoja za Mawakili wa Wadaiwa na ameamua kuwa kesi ya msingi itatajwa tarehe 15/4/2015 na hoja za kisheria kupokelewa siku hiyo. Hivyobasi,Mwigamba na wenzake ambao ni Wadaiwa/Wajibu Maombi watendelea kujihusisha na ACT-Tanzania hadi itaapoamriwa vinginevyo.