Noor
Senior Member
- Feb 5, 2012
- 146
- 49
Mimi ni mkaka mwenye miaka 27 nilikutana na mdada mwenye miaka 24 facebook tukaanza kuchat na hatimaye tukafikia uamuzi wa kua wapenzi. Aliniambia hakuna kwenye mahusiano kama nilivyokua mimi. Siku aliyokuja kwangu kulala alikuja kwenye saa tatu usiku, nikamuuliza leo imekuaje hadi amepata muda wa kuja kulala kwangu akaniambia baba yake amesafiri, nikamuuliza kuhusu mama yake akanambia nae ameenda kwa marafiki zake. Nikawa na swali linaumiza kichwa kua paka akitoka panya anajitawala? Tukiwa bado tunaendelea na maongezi ya hapa na pale mama yake akampigia simu kuwa amuandalie nguo kwa ajili ya kesho kazini, atazipitia saa kumi na mbili wakati anaenda kazini. Nikamuuliza kwa hiyo mama harudi nyumbani leo akanijibu ndio maana yake, hawezi kurudi kwa sababu baba hayupo. Ilibidi aondoke usiku huo huo maana alikua hana jinsi ya kulala wakati mama yake atapita mapema.
Je huyo anafaa kua mke maana toka nilivyojua tabia ya mama yake na yeye sihitaji hata kumuona. naomba mnishauri nifanyeje?
Je huyo anafaa kua mke maana toka nilivyojua tabia ya mama yake na yeye sihitaji hata kumuona. naomba mnishauri nifanyeje?