Ligi yetu inaendeshwa Kihuni

rodrick alexander

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2012
Posts
18,068
Reaction score
25,737
Hii ligi sijui wanatumia vigezo gani kuiweka ligi namba 5 kwa ubora Afrika.

Mojawapo ya adhabu ziluzotangazwa na bodi ya ligi ni adhabu ya kufungiwa shabiki wa yanga anayeandamana na benchi la ufundi.

Hivi shabiki anawezaje kukaa kwenye benchi la ufundi, ina maana mtu yoyote anaweza kukaa kwenye benchi la ufundi?

Bodi ya ligi inabidi ijitathimi kwa sababu kila siku inadhalilika.
 
Ndiyo maana amefungiwa
 
Ubora wa ligi hauna mahusiano yoyote na uendeshaji wa ligi, ubora league (coefficient) hutokana na kiasi gani club za Nchi husika zimefanikiwa kwenye mashindano ya bara kama vile Caf champions league.

Ligi ya Spain ina drama kushinda hata hii yetu na ni Katika ligi Bora zaidi Duniani. Mambo ya kipuuzi kama hayo yapo kote Duniani.
 
Ulitaka Mchawi wenu aendelee kuruhusiwa kuambatana na technical bench? Maana mlikuwa mnamwamini kuliko Kocha Pedro.
 
Vina mahusiano kuanzia uwekezaji, ushindani, wachezaji bora, waamuzi bora.
 
mimi nilisha acha.kuangalia
 
🤣🤣🤣

Bado mnafuatilia hiyo league yenu ya vichekesho Hiyo league Ina vituko balaa mwaka Jana Simba na yanga walikuwa wana bebwa mpaka wakapitiliza yaani mpaka upendeleo wao uliibuka kuwa Hoja bungeni Aiseee. Mimi siwezi kutazama vile vituko
 
Sasa hivi wameanzisha tuzo ya goli bora la mwezi eti washabiki wapigie kura kitu ambacho hakikuwepo
 
Kama Tanzania lighe yake ipo 5 bora basi ligi zilizochini yake zitakuwa na madudu kupitiliza... Hii ni ishara tosha kuwa Manigga na Warabu wetu tuna safari ndefu sana
 
Ligi yetu ina madudu mengi, lakini kwa vigezo vya caf, sisi tutakaa pale mpaka timu zetu zianze kufanya hovyo
 
[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…